Superman
JF-Expert Member
- Mar 31, 2007
- 5,695
- 1,696
Tatizo la mimba kutoka au kutolewa ni jambo ambalo limewakumba kina mama wengi walio katika umri wa kuzaa. Aidha mijadala kuhusu kuhalalishwa au kuendelea kuharamishwa kwa utoaji mimba ni jambo linalochukua nafasi ya mazungumzo ya kila siku katika maisha yetu. Kwa baadhi ya nchi, suala la utoaji mimba ni jambo lililohalallshwa kisheria ingawa kwa nchi kama Tanzania, suala hili halijahalalishwa isipokuwa tu pale panapokuwa na sababu za kitabibu zinazolazimisha kufanya hivyo.
Nini maana ya mimba kutoka (abortion)
Kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO), utokaji mimba (abortion) hutokea pale ambapo kiumbe (mimba) kilicho chini ya wiki 22 kinapotoka kwa sababu moja ama nyingine, au kinapotolewa kwa njia yeyote ile. Aidha shirika la Afya limekwenda mbali zaidi na kutoa maana nyingine ya utokaji mimba kuwa ni pale mtoto (kiumbe) anapozaliwa akiwa na uzito wa chini ya gram 500.
Aidha baadhi ya matabibu hupendelea kutumia neno abortion kumaanisha kitendo cha utoaji wa mimba kinachofanywa na mtu mwingine ama kwa njia sahihi au zisizo sahihi na miscarriage kumaanisha kitendo cha mimba kutoka yenyewe kwa sababu nyingine yeyote. Ukiacha tofauti hizi za jinsi ya kuharibika kwa mimba, abortion na miscarriage humanisha kitu kilekile cha mimba kutoka.
Tanzania ni Nchi ambayo haijaridhia kuwa na Sheria Ya Kutoa Mimba na hivyo Kutoa Mimba ni kosa. Hata hivyo tumeshuhudia vitendo vya abortion vikizidi kuongezeka kwa wanawake wakiwemo wanafunzi wa shule au vyuo na wasio wanafunzi. Hii inaleta changamoto yenye utata juu ya nini hasa ni sahihi katika suala zima la utoaji mimba.
Utoaji mimba kinyume cha sheria (illegal abortion)
Utoaji mimba kinyume cha sheria ni usitishwaji wa maisha ya mimba au kutolewa kwa kiumbe kinyume na sheria za nchi husika zinavyoagiza. Katika mazingira kama haya, sababu dhahiri za kitaalamu hukosekana isipokuwa wahusika hutenda kulingana na sababu zao binafsi zikiwemo za kutoitaka mimba au kama ni muhusika ni mwanafunzi huogopa kufukuzwa shule.
Utoaji mimba kisheria kwa sababu za kitabibu (therapeutic abortion)
Utoaji mimba ulioidhinishwa kitabibu ni usitishwaji wa mimba kwa ajili ya kuokoa maisha ya mama. Usitishwaji huu ni hufanywa kitaalamu na daktari. Sababu zinazoweza kufanya mimba ikasitishwa ni pamoja na:
- iwapo kiumbe kina mapungufu mengi ya kimaumbile (fetal anomally) ambayo yatamletea mtoto atakayezaliwa matatizo na hata kusababisha kifo chake
- iwapo mama mjamzito alipata ujauzito kwa kubakwa na asingependa kuzaa, au
- iwapo mama mjamzito ana kansa , kwa mfano, kansa ya kiwanda cha mayai ya kike (ovarian cancer), kansa ya damu (leukemia) au kansa ya tezi la goita (thyroid cancer)
Je, utoaji mimba kwa kukusudia uruhusiwe?
Kama ndiyo uruhusiwe ni kwa nini?
Na kama hapana usiruhusiwe ni kwa nini?
Naomba kuwakilisha.
Nini maana ya mimba kutoka (abortion)
Kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO), utokaji mimba (abortion) hutokea pale ambapo kiumbe (mimba) kilicho chini ya wiki 22 kinapotoka kwa sababu moja ama nyingine, au kinapotolewa kwa njia yeyote ile. Aidha shirika la Afya limekwenda mbali zaidi na kutoa maana nyingine ya utokaji mimba kuwa ni pale mtoto (kiumbe) anapozaliwa akiwa na uzito wa chini ya gram 500.
Aidha baadhi ya matabibu hupendelea kutumia neno abortion kumaanisha kitendo cha utoaji wa mimba kinachofanywa na mtu mwingine ama kwa njia sahihi au zisizo sahihi na miscarriage kumaanisha kitendo cha mimba kutoka yenyewe kwa sababu nyingine yeyote. Ukiacha tofauti hizi za jinsi ya kuharibika kwa mimba, abortion na miscarriage humanisha kitu kilekile cha mimba kutoka.
Tanzania ni Nchi ambayo haijaridhia kuwa na Sheria Ya Kutoa Mimba na hivyo Kutoa Mimba ni kosa. Hata hivyo tumeshuhudia vitendo vya abortion vikizidi kuongezeka kwa wanawake wakiwemo wanafunzi wa shule au vyuo na wasio wanafunzi. Hii inaleta changamoto yenye utata juu ya nini hasa ni sahihi katika suala zima la utoaji mimba.
Utoaji mimba kinyume cha sheria (illegal abortion)
Utoaji mimba kinyume cha sheria ni usitishwaji wa maisha ya mimba au kutolewa kwa kiumbe kinyume na sheria za nchi husika zinavyoagiza. Katika mazingira kama haya, sababu dhahiri za kitaalamu hukosekana isipokuwa wahusika hutenda kulingana na sababu zao binafsi zikiwemo za kutoitaka mimba au kama ni muhusika ni mwanafunzi huogopa kufukuzwa shule.
Utoaji mimba kisheria kwa sababu za kitabibu (therapeutic abortion)
Utoaji mimba ulioidhinishwa kitabibu ni usitishwaji wa mimba kwa ajili ya kuokoa maisha ya mama. Usitishwaji huu ni hufanywa kitaalamu na daktari. Sababu zinazoweza kufanya mimba ikasitishwa ni pamoja na:
- iwapo kiumbe kina mapungufu mengi ya kimaumbile (fetal anomally) ambayo yatamletea mtoto atakayezaliwa matatizo na hata kusababisha kifo chake
- iwapo mama mjamzito alipata ujauzito kwa kubakwa na asingependa kuzaa, au
- iwapo mama mjamzito ana kansa , kwa mfano, kansa ya kiwanda cha mayai ya kike (ovarian cancer), kansa ya damu (leukemia) au kansa ya tezi la goita (thyroid cancer)
Je, utoaji mimba kwa kukusudia uruhusiwe?
Kama ndiyo uruhusiwe ni kwa nini?
Na kama hapana usiruhusiwe ni kwa nini?
Naomba kuwakilisha.