Masikini watanzania!

Nyange

JF-Expert Member
Mar 25, 2010
3,516
1,865
Masikini Tanzania yetu!

Masikini Tanzania yetu!

Habari za leo zimenishutua pale niliposikia Profesor Magembe ambaye ni waziri wa Elimu na mafunzo ya ufundi kuwa Elimu itakuwa kuanzia darasa la kwanza mpaka form 4 bila kufanya mtihani!!!!!!!!!!!!!!!! What? Mnataka tupate form 4 bila kujua kusoma na kuandika!!

Kweli inatosha mmezidi kutuharibia nchi yetu. nadhani hayo ni matatizo ya kutaka kukopi sera za vyama pinzani. Mtafurahi watanzania wote wakiwa waajiliwa wa kampuni za ulinzi?

Mi naona 31/10 imekuwa mbali, tunataka kuona nchi inakombolewa dhidi ya Mafisadi walio lewa madaraka. Wao walipata elimu safi lakini wanataka watanzania wawe mbumbumbu! JAMANI SERA ZA SISIEM NI ZA KUUA NCHI NA ZINATOKANA NA MAWAZO YA MTU ASIYE NA DIRA, HAZINA UTAFITI. Hebu tafakari
  • Ntanunua meli ya ziwa Victoria,
  • Ntanunua Meli ya ziwa Nyasa,
  • Ntanunua meli ziwa Tanganyika, huku Serikali ikitoa tamko kuwa haitafanya biashara bali itakusanya kodi.
  • Ntajenga machnga complex kila wilaya ya Dar,
  • Ntajenga barabara za juu kuondoa msongamano jijini Dar,
  • Tatizo la maji mnipe miaka miwili,
  • Kilimo kwanza,
  • Sasa elimu ya s/msingi hadi form 4 bila kufanya mtihani wa darasa la saba!!!!!!!! hayo ni machache tu sijataja bajaji za kubeba wajawazito huko Mvomero, na kugeuza hospitali kuwa za rufaa kwa kuzibadili majina tu!! bila kupeleka madokta, wala kuongeza vifaa vya wagonjwa!!!!
HAYA YOTE YANAONGEWA KAMA KASUKU bila andiko? THITHIEM NCHI MMESHAIMALIZA MNATAKA SASA KUIZIKA?
icon6.png
 
Back
Top Bottom