Mashiriki ya Kati Kwachafuka

Filosofia ya Rorya

JF-Expert Member
Sep 20, 2021
3,214
3,587
Vita baina ya Israel na Vikundi vya Kihafidhina vinavyotafsiriwa na watu wa Magharibi kama vya kighaidi vya HAMAS, HEZBOLLAH na HOUTHI vinaelekea kusambaa na kuamsha INTIFADA YA DUNIA ambayo tayari imegawanyika kufuatia vita hiyo.

Vita hivi vilianza kama vya kujihami baina ya mahasimu wawili IDF na HAMAS na sasa vimebadilika kuwa vita vya maslahi ambavyo vimevutia mataifa makubwa na kambi 2 za kujihami duniani kutumia vita hivyo kama fursa.

Duniani leo vita ni biashara na fursa nyingine lukuki, kama hakuna hivyo viwili hakuna vita inaweza kupiganwa.

Wakati hayo yakiendelea ni wazi kuwa IDF inatanua wigo wa medani kujumuisha Lebanon (Hezbollah), Yemen (Houthi) na Syria inajipanga kwa sababu Hezbollah wakielemewa watakimbilia Syria na lazima IDF itawafuata huko hivyo Syria italazimika kukabiliana na IDF.

IDF ikiwaelemea Hezbollah wataokimbilia Syria ni wazi kuwa Hezbollah hao watahamia Jordan hii pia itahusu wapiganaji wa Ukingo wa Magharibi, Jordan italazimika kuingia kwenye medani na IDF. Mduara huo utafika Yemen kukabili HOUTHI.

Dunia inapaswa kujitafakari upya kwa faida, mustakabali na hatma ya vizazi vijavyo.
 
Huu uchambuzi ni kwa mujibu wa mashirika yapi ya kijasusi 🤖?
 
Mbona umeandika kirahisi hivyo.US anahaha kumaliza vita mashariki ya kati kwa mazungumzo kwa pande zote zinazosigana.vita ikisimama mashariki ya kati kisawasawa uchumi wa Dunia utakuwa mashakani.
 
Huu uchambuzi ni kwa mujibu wa mashirika yapi ya kijasusi ?
Kumbe ni Mashirika ya Kijasusi pekee ndiyo yana ukiritimba wa uchambuzi wa kimedani!?

Ninakumbuka mara nyingi chambuzi zao zimeshutumiwa kwa kujaa propaganda na proparwanda (zinaelemea itikadi zao na mirengo yao)
 
Daah umeandika kama mchambuzi wa Mpira eti Hezborah wakikimbilia Yemen IDF watawafata huko daah tuendelee kuvua dagaa tu mkuu maana wamesema zina madini sana..
 
Mbona umeandika kirahisi hivyo.US anahaha kumaliza vita mashariki ya kati kwa mazungumzo kwa pande zote zinazosigana.vita ikisimama mashariki ya kati kisawasawa uchumi wa Dunia utakuwa mashakani.
Mhe. Blinken amefanya ziara 4 na hazijazaa matokeo tarajali. Tatizo ni kuwa anaenda akiwa tayari ana upande kwenye medani hiyo kwa maana kwamba akiwa upande wa Israel, akisisitiza kwamba kama HAMAS isingeshambulia Israel Oktoba 7 hii vita isingekuwepo leo, hii inadhihirisha kwamba US inaishutumu HAMAS, hivyo US imechukuwa upande wa Israel.
 
Daah umeandika kama mchambuzi wa Mpira eti Hezborah wakikimbilia Yemen IDF watawafata huko daah tuendelee kuvua dagaa tu mkuu maana wamesema zina madini sana..
Unajuwa medani zifuatazo?
1. Six Day War 1967.
2. Intifada.
3. Global Intifada.
4. Egypt Israel War 1956, 1967, 1973?

NB.
Siyo tu Yemen hata Misri watafika.
 
Unajuwa medani zifuatazo?
1. Six Day War 1967.
2. Intifada.
3. Global Intifada.
4. Egypt Israel War 1956, 1967, 1973?

NB.
Siyo tu Yemen hata Misri watafika.
Mkuu hawana nguvu hizo hao meli za kivita za USA na ndugu zake wanaizunguka Dunia kila kukicha ushasikia pana meli ya kivita katika Nchi ulizotaja ipo baharini huko au submarine..
 
Nachelea hata kuandika.

Watanzania kwa uchambuzi wa mambo na masuala ya nje, hatujambo.

Lakini, kuna walakin mkubwa sana katika uchambuzi wa mambo na masuala ya Afrika.

Yote yanashangaza. Nashangazwa.

Haya, Pipoooooz mpo?
 
Nachelea hata kuandika.

Watanzania kwa uchambuzi wa mambo na masuala ya nje, hatujambo.

Lakini, kuna walakin mkubwa sana katika uchambuzi wa mambo na masuala ya Afrika.

Yote yanashangaza. Nashangazwa.

Haya, Pipoooooz mpo?
upumbavu tu wa kidini unawapelekesha mpaka akili zao wanaziweka pembeni
 
Back
Top Bottom