Swahilian
JF-Expert Member
- Apr 28, 2009
- 591
- 66
Ukistaajabu ya arsenal wa nairobi utaona ya manchester wa nigeria, huo ndio msemo rahisi na wenye msingi kwamba dunia hii ina mambo na wingi wa vioja, miaka iliyopita tulishuhudia watu wakiuwawa au kujitolea kufa kwa ajili ya dini au imani zao, kabila au jamii zao na wengine mali,wake au chakula, lakini hivi sasa mambo yamebadilika na kuingia katika soka, ambapo mashabiki kadhaa wamejiua au kuua wenzao eti kisa kufungwa na wapinzani wao,hii kazi!