Mara: Mwanafunzi agoma kwenda shule kisa hana akili

omugabire

Senior Member
Jun 17, 2019
128
174
Katika hali ya kushangaza mwanafunzi mmoja mkoani Mara amegoma kuendelea na elimu ya kidato cha kwanza kwa madai kwamba hana akili.

Mwanafunzi huyo amesema anashangaa kwanini amefaulu wakati alifanya mtihani vibaya kwa makusudi. Katika hatua nyingine mwanafunzi huyo amedai yuko radhi akamatwe na jeshi la polisi kuliko kwenda shule.

Nini maoni yako?

=====
Mwanafunzi agoma kwenda kidato cha kwanza kwa madai kuwa hana akili

Mwanafunzi mwenye umri wa miaka 15 jina tunalihifadhi aliyefaulu kwenda kidato cha kwanza kwa wastani C katika matokeo ya darasa la saba mwaka huu wilaya ya Musoma mkoa wa Mara amegoma kwenda shule kwa kile anachodai hana akili ya kusoma masomo ya sekondari huku akitamka mbele ya mkuu wa wilaya kuwa yuko tayari kufungwa na si kusoma.

Akizungumza na ITV akiwa nyumbani kwao mwanafunzi huo amesema alifanya mtihani wa darasa la saba mwaka jana vibaya ili asifaulu lakini anashangazwa na matokeo yanayoonyesha amefaulu na kudai hayuko tayari kusoma huku akiomba akajifunze kushona cherehani kwani anataka kuwa mwanamitindo

ITV imewatafuta wazazi wa binti huyo na kuzungmza nao ambapo wamesema wamesikitishwa na uamuzi wa mtoto wao na kudai kuwa binti yao ametoweka kusikojulikana tangu tarehe 25 mwaka jana na kumtafuta kila mahali lakini baada ya mkuu wa wilaya juzi kutangaza kuwakamata na kuwafunga wazazi ambao watoto wao hawajaripoti shule ndipo mwanafunzi huyo alipoibuka na kuwataka wazazi wake wampeleke kwa mkuu wa wilaya ili akamueleze kuwa hataki kusoma.

Chanzo: ITV

Sent using Jamii Forums mobile app
 
zamani kufaulu kwenda sekondari ilikuwa shughuli pevu, siku hizi mtoto anafaulu hata akiwaza amefauluje hapati jibu, maisha yanabadilika!! unakuta mtoto anamaliza darasa la saba hajui hata kuandika jina lake kisha anafaulu kwenda sekondari, sayansi inayotumika hapo hata mimi sijaielewa sawa na huyo mwanafunzi wa mara!
 
Jinsi Elimu na maisha visivyoendana...


Baada ya Miaka kadhaa, utakuta Mwanafunzi anamaisha makubwaa ya maana.


Ukibisha, Jiulize wale ulowaacha Lasaba , kidatocha NNE wako wapi??


Elimu husaidia kufikia Ndoto yaan nmekua mwalimu, Daktar, Mwandisi mwanasheria n.k.... LAKINI linapokuja suala LA Kufanikiwa maisha kila MTU huwa ana tafasiri yake!!


Naungana na Dogo apelekwe kujifunza Cherehani.



Jamaa mmoja ivi, Kujikuta anapenda shule, kupata tu C tatu kidato cha NNE za kuendelea mbele alirudia rudia zaidi ya Mara NNE lkn hapati hata moja.

Aliposhauriwa aachane na shule, akaingia Garage pale Mwanza , mwana Saizi ANANIZIDI MAISHA ,yupo mbali mnooo.
 
Kama ingekuwa ni kuchagua aachiwe aendelee na anachokipenda
Wenzetu wanaanza mchakato wa kuhimiza watoto waishie miaka 16 ya umri na wakubaliwe kwenda kujifunza ufundi au technology wanayotaka badala ya kupoteza mda shule
Apewe anachopenda


Sent from my iPhone using Tapatalk
 
Kuna hitajika mjadala mpana juuu ya hili Jambo, waandishi wa habari utakuta wanaishia hapo tu, badala ya kwenda had ndani Kabisa kupata ufafanuz Kwa walimu, shule alikosoma, alama alizopata Kwa Afisa Elimu had kwa waziri maaana kuna Dalili kuwa huenda watoto wanafaulishwa na huenda wako wengi Sana waliofaulishwa, hili Jambo ni Kubwa kuliko mnavyofikiri tunahitaji mitihani yake huyu Mtoto iwekwe hadharani kuna, sintofaham kubwa Kwa hizi shule

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom