kilambimkwidu
JF-Expert Member
- Jul 21, 2017
- 6,052
- 7,057
●Watu wamebomolewa nyumba zao kwa hila, hawana makazi. Wala ww hujui siku wala saa ambayo greda litaamrishwa kuja kuchonga barabara sebuleni kwenu.
●watu wametumikia nchi yao kwa weledi, ghafla wamefukuzwa kazi na kunyimwa mafao eti wanavyeti feki wakati Bashite anafuta mabaraza ya ardhi akiwa hana hana hata hyo form4.
●Watu wanatekwa na kupigwa mapanga na wengine kutoswa baharini na polisi inatuhumiwa bado hapohapo mtutu wa bunduki unaelekezwa kwa watembea kwa miguu wanamiminiwa risasi watu (ambao wala hawaandamani ispokua wanafuata viapo vyao).
Bora kufa ukiwa mstari wa mbele ukitetea taifa lako na kizazi chako kuliko kunyamazia utawala wa kimabavu halafu zamu yako ikifika unauliwa kizembe tu hata kwa kuwekwa kwenye kiroba unatoswa baharini au kwa shoka la kichwa.
26 April 2018 inakuja na itakumbukwa!!