Mapquest bongo

Hivi kuna huduma yoyote inayofanana na mapquest Tanzania?

Sidhani kama itakuwepo, maana kuna mitaa mingi haina majina halafu pale uhindini wahindi wamebadilisha majina ya mitaa mingi na kuweka majina ya kihindi bila hata ya kuwa na kibali cha jiji.
 
Mitaa hipi tena BAK


Majina ya mitaa Dar yabadilishwa kinyemela

Na Happy Wamanyamba

BAADHI ya mitaa maarufu katikati ya Jiji la Dar es Salaam imebadilishwa majina, huku uongozi wa Jiji na Manispaa ya Ilala ukidai kutokuwa na taarifa za mtu aliyebadili majina hayo.

Baadhi ya mitaa iliyobadilishwa majina ni Mtaa wa Kisutu ambao hivi sasa unajulikana kwa jina la Mtaa wa Pramukh Swami, na mwingine ni mtaa uliopo jirani na mitaa ya Jamhuri na Zanaki, ambao sasa umebadilishwa jina na kuitwa Mtaa wa Hazrat Abbas (A.S).

Viongozi wa Jiji na Manispaa ya Ilala ambao walizungumza kwa njia ya simu na gazeti hili kwa nyakati tofauti jana, wote walikwepa kuzungumzia suala, wakidai kuwa si wahusika.

Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Alhaji Adam Kimbisa , alipoulizwa kuhusu taratibu zilizotumika katika kubadilisha majina ya mitaa hiyo, alisema wahusika wakuu ni Meya wa Manispaa ya Ilala na si yeye.

"Waulize mameya wa manispaa husika wao ndio wanajua wanatumia taratibu gani, kwani kila manispaa inataratibu zake, hivyo mimi sijui ni taratibu gani zimetumika katika kubadili majina hayo," alisema Kimbisa.

Mbali ya Kimbisa, Meya wa Manispaa ya Ilala, Abuu Jumaa, ambako mitaa imebadilishwa majina na kupewa majina ya wageni, naye alikwepa kuzungumzia mabadiliko hayo.

"Ni mitaa gani imebadilishwa? Mbona mimi siijui? Hata hivyo taratibu zilizotumika katika kubadili majina ya mitaa sizijui, labda watafute madiwani na wenyeviti wa mitaa husika ili waweze kueleza sababu za kubadilisha majina ya mitaa hiyo, ila mimi sifahamu," alisema Jumaa.

Kubadilishwa kwa mitaa hiyo kiholela kumekuwa kukisababishia baadhi ya watu, hasa wageni, kupata usumbufu, kutokana na majina yaliyozoeleka kubadilishwa.

Kwa kawaida, majina ya mitaa hubadilishwa na manispaa zinazohusika, na mara kwa mara, majina ya watu maarufu katika taifa au hata maeneo ya kihistoria na mambo kama hayo, hutumika kupata majina ya mitaa.
 
Majina ya mitaa Dar yabadilishwa kinyemela

Na Happy Wamanyamba

BAADHI ya mitaa maarufu katikati ya Jiji la Dar es Salaam imebadilishwa majina, huku uongozi wa Jiji na Manispaa ya Ilala ukidai kutokuwa na taarifa za mtu aliyebadili majina hayo.

Baadhi ya mitaa iliyobadilishwa majina ni Mtaa wa Kisutu ambao hivi sasa unajulikana kwa jina la Mtaa wa Pramukh Swami, na mwingine ni mtaa uliopo jirani na mitaa ya Jamhuri na Zanaki, ambao sasa umebadilishwa jina na kuitwa Mtaa wa Hazrat Abbas (A.S).

Viongozi wa Jiji na Manispaa ya Ilala ambao walizungumza kwa njia ya simu na gazeti hili kwa nyakati tofauti jana, wote walikwepa kuzungumzia suala, wakidai kuwa si wahusika.

Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Alhaji Adam Kimbisa , alipoulizwa kuhusu taratibu zilizotumika katika kubadilisha majina ya mitaa hiyo, alisema wahusika wakuu ni Meya wa Manispaa ya Ilala na si yeye.

"Waulize mameya wa manispaa husika wao ndio wanajua wanatumia taratibu gani, kwani kila manispaa inataratibu zake, hivyo mimi sijui ni taratibu gani zimetumika katika kubadili majina hayo," alisema Kimbisa.

Mbali ya Kimbisa, Meya wa Manispaa ya Ilala, Abuu Jumaa, ambako mitaa imebadilishwa majina na kupewa majina ya wageni, naye alikwepa kuzungumzia mabadiliko hayo.

"Ni mitaa gani imebadilishwa? Mbona mimi siijui? Hata hivyo taratibu zilizotumika katika kubadili majina ya mitaa sizijui, labda watafute madiwani na wenyeviti wa mitaa husika ili waweze kueleza sababu za kubadilisha majina ya mitaa hiyo, ila mimi sifahamu," alisema Jumaa.

Kubadilishwa kwa mitaa hiyo kiholela kumekuwa kukisababishia baadhi ya watu, hasa wageni, kupata usumbufu, kutokana na majina yaliyozoeleka kubadilishwa.

Kwa kawaida, majina ya mitaa hubadilishwa na manispaa zinazohusika, na mara kwa mara, majina ya watu maarufu katika taifa au hata maeneo ya kihistoria na mambo kama hayo, hutumika kupata majina ya mitaa.

ama kweli SHAMBA LA BIBI........hadi mitaa inabadilishwa watu hawana habari.......
 
Majina ya mitaa Dar yabadilishwa kinyemela

Na Happy Wamanyamba

BAADHI ya mitaa maarufu katikati ya Jiji la Dar es Salaam imebadilishwa majina, ...ni Mtaa wa Kisutu ambao hivi sasa unajulikana kwa jina la Mtaa wa Pramukh Swami, na mwingine ni mtaa uliopo jirani na mitaa ya Jamhuri na Zanaki, ambao sasa umebadilishwa jina na kuitwa Mtaa wa Hazrat Abbas (A.S)...
Basi ipo kazi, kwani wahusika haswa ni nani... Serikali za mitaa au serikali kuu.
 
Basi ipo kazi, kwani wahusika haswa ni nani... Serikali za mitaa au serikali kuu.

SASA HIVI ITAUNDWA TUME YA MADIWANI ,IKIONGOZWA NA MEYA HUSIKA,.ITAFANYA UTAFITI ILI KUJUA NI SHERIA GANI INATUMIKA KUWEZA KUBADILISHA HAYO MAJINA,..HALAFU ITAUNDWA tume NYINGINE YA KUFUATILIA SABABU YA KUBADILISHWA HAYO MAJINA,..HII ITAONGOZWA NA KAIMU MEYA ,.IKISHIRKISHA MADIWANI WA SEHEMU HUSIKA NA WAJUMBE WA NYUMBA KUMI,. BAADAYE ITAUNDWA NYINGINE YA KUBAINI NI KINA NANI WALIOFANYA HIVYO,.HII ITAONGOZWA NA MEYA, VIONGOZI WA DINI [MASHEHE,VIONGOZI WA MABOHORA,WAISHIO HUKO] WAKISHIRIKIANA NA POLISI
,..RIPOTI KAMILI IKIPATIKANA WAHUSIKA WATAPELEKWA POLISI,.
NAO POLISI WATAANZA UPELELEZI KUMBAINI MUHUSIKA....
BAADAYE WAZIRI HUSIKA ATAINGILIA KATI NA KUAMURU MAJINA YA ZAMANI YARUDISHWE...
MANISPAA HUSIKA ITASHINDWA KUTEKELEZA AGIZO LA WAZIRI SABABU HILO HALIPO KWENYE FUNGU LA BAJETI YA MWAKA HUU LABDA WASUBIRI BAJETI IJAYO,,..
MADIWANI WA SEHEMU HUSIKA WATAIOMBA POLISI IWASAIDIE KUWABANA WAHUSIKA ILI WACHORE VIBAO VIPYA,..POLISI ITAKATAA NA KUSEMA SUALA HILO LISUBIRI MAAMUZI YA MAHAKAMA.,.
HUKUMU YA KESI NAYO ITATOLEWA BAADA YA MIAKA MIWILI,..NAWASHTAKIWA WATARUHUSIWA KUJIDHAMINI,...
MPAKA HUKUMU IJE KUTOKA BAADA YA MIAKA MIWILI,.WATU WATAKUWA WAMESHAZOEA MAJINA MAPYA YA HIYO MITAA,.HIVYO YAKIBADILISHWA WAGENI NA WENYEJI WATAPOTEA TENA
,...........WAKATI MWINGINE SYSTEM YETU YA KUFANYA KAZI BONGO INANIKUMBUSHA ,HADITHI KARUMEKENGE ALIVYOKATAA KWENDA SHULE.,....hawa madiwani na meya sijui kazi yao ni nini hasa...tabu kweli kweli
 
Back
Top Bottom