Mapinduzi yaja Tanzania

Masanilo

Platinum Member
Oct 2, 2007
22,286
4,493
Nguvu ya mabadiliko Tanzania inakuja kwa kasi ya ajabu. Hakuna kinachoweza kuzuia nguvu ya umma.

Kila sehemu ya maisha wananchi wa kada zote wanaonyesha kutofurahia serikali iliyopo madarakani. Ugumu wa maisha na kushamiri kwa rushwa ni kero kubwa kwa Mtanzania wa kawaida.

Unachokiona hapa JF pamoja na propaganda lakini ni wazi watetezi wa serikali ya Magamba huwa hawana hoja, nimepitia Twitter, Facebook na blog nyingi zinazoongozwa na watanzania kote huko serikali inachanwa mno. Pamoja na kuwa na watetezi wa mafisadi lakini ninaona kabisa wimbi hili litatufikisha mahali pazuri. Nimeongea na jamaa yangu yuko hazina pale wizara ya fedha kutaka kujua ukweli wa uchumi wetu, alichonijibu hakuna tofauti na anachofanya Jairos bungeni.

Uchumi wetu umeathirika sana na mgawo wa umeme. Lakini kunapropaganda eti uchumi unakuwa hii ni kumdanganya nani....hata sisi tusiojua hata zile theories of economic development tunaona inflation inavyokuwa kwa kasi. Wataalamu wanaambiwa wachakachue takwimu ili waziri aweze ongea kile ambacho serikali inapenda kukisikia.

You cant change the wind of changes .......aluta continua pamoja tunaweza epusha nchi yetu kutoka kwa mafisadi hawa.
 
JK, i nw believe that leadership is a talent...he doesn't seem to have one....i think he s missing a particular ingredient which is important to a leader....anyway, we still ve about 4 years to waste.....hopefully, we ll forget him.....he has wasted our good 10 yrs RIP Kikwete!! 5 minutes ago · Like

Hii nimeitoa facebook, jamaa wanamchana sana sana Kikwete na utawala wake
 
Hao unayoyasema ni ya ukweli kabisa, nina ndugu yangu yuko pale Magogoni anasema Watu wamemchoka Kikwete , mjeuri, kiburi na hajali mambo yanayoendelea Nchi akiambiwa anakuwa mkali. wafanyakazi wote Magogoni hawampendi wanataka leo kesho nguvu ya Umma imuondoe. Wanasema Kikwete yuko Magogoni kwa Maslai Binafsi sio Taifa
 
Ndiyo maana mimi naomba usiku na mchana haya matatizo yanayotukabili watz yaongezeka hata mara mia ili kuharakisha ukombozi, siyo kama nafurahia ki hivyo ila ni kutokana na watz wenyewe kuwa wagumu kutambua chanzo cha matatizo yao.Matatizo yetu kwa asilimia 95 yamesababishwa na uongozi mbovu, kwani Mwenyezi Mungu ametujalia kila kitu cha kutufanya watz tuwe matajiri kuliko watu wote duniani, lakini kwa uzuzu wetu tumeendelea kuikumbatia CCM ambayo ni janga la kitaifa.CCM NDIYO WAMEIFUKARISHA NCHI
 
Plz dnt blame and dnt b harsh 2 him coz hata kaul anazotoa czan kama anafikiria kabla ya kuongea the onlx thng 2 knw is that WE Tanzanians we've grant seeds 4 our own Destruction.
coz during election 2lielezwa na Dr SLAA bt wengi 2lishndwa kufanya maamuzi sahihi 2kaangukiwa kudanganywa na Tabasamu la KINAFIKI la The King of Embazzlement Mhe:FISADI JK wa pili.
 
Reverend Masanilo,

Kuna mahali nilichangia kwenye thread aliyoianzisha mkandara leo alfajiri nikasema

Mkandara,

Hoja nzuri sana umetoa.Kama demokrasia ingekuwa universally beneficial kwa mataifa yote basi tungekuwa katika nafasi nzuri zaidi ya kunufaika.Kwa hali ilivyo sasa,ni kweli kuna kila Dalili kwamba Demokrasia imetushinda tunaifanyia majaribio tu bado tena kwa mbinu na mikakati ile iliyoshindwa

Kwa kweli hii dhana tuliyoletewa ya Demokrasia,imesababisha sisi kurudi nyuma.Hatuna tofauti na mfumo wa kisultani.Leo hii maamuzi magumu ya hayawezi kuchukuliwa kwa hoja ya kipuuzi kabisa mkuu wa nchi yupo nje ya nchi.Rais akiwa nje kuna VP na wengineo,katiba yenye maono ya demokrasia inasema hivyo.

Ni bora turudi kwenye mfumo wa chama kimoja utakaozuia fikra ili sisi wengine tusiopenda kuburuzwa tutumie nguvu za kimapinduzi kwa kusukumwa na uzalendo wetu tuchukue nchi tuongeze kidikteta lakini kizalendo.Tunahitaji utawala kama wa Gaddaffi,tunahitaji mfumo kama wa kagame na Hugo Chavez.tunahitaji mfumo kama wa Evo morales,kusema kweli na siogopi kusema Democracy does not Suit us.bado hatujajiandaa,hii ni imported vice ! ! !

Kama si kuitikia wito na kukubali kuburuzwa na mfumo wa kibeberu,leo hii ningekuwa kwenye kambi,milima ya mbali na au hata msituni kujiandaa kizalendo.Ningekuwa na sababu za kutosha ! ! ! Huwezi kuwa na demokrasia ya kweli kama wananchi wako ni maskini,wanasumbuliwa na maradhi na Ujinga....Huwezi kuwa na uongozi ambao ni zao la Demokrasia bila kuwa na msingi wa imani ya kisiasa,kiuchumi na kijamii katika kiungo cha uongozi na utawala (namaanisha ideology).

Leadership tuliyo nayo ni hadaa tu,sio kwa serikali tu hata kwa vyama vingine vya siasa.Tunapata pigo kubwa sana kwa ngumi iliyovaa gloves za demokrasia(Pseudo democracy).jaribu kufikiria na kutafakari juu ya mfumo wote wa vyama vya siasa Tanzania,jaribu kufuatilia mfululizo wa matukio kwenye vyama hivyo.Kila siku tunapiga hatua kuwasukuma vijana wazalendo kuingia kambini,milimani au misituni.kila dakika ambayo tunahubiri democracy na vijana wazalendo kweli kweli kwa nchi yao hawaoni uhalisia na matunda yatokanayo na dhana hiyo basi tunawatoa kwenye Demokrasia tunawapeleka misituni.

Haya yana Mwisho,kinachohitajika ni hatua za haraka zichukuliwe ama la basi yatatimia.Carl max,alisema...'A single step in the Revolutionary movement worths a Dozen programmes'
 
Plz dnt blame and dnt b harsh 2 him coz hata kaul anazotoa czan kama anafikiria kabla ya kuongea the onlx thng 2 knw is that WE Tanzanians we've grant seeds 4 our own Destruction.
coz during election 2lielezwa na Dr SLAA bt wengi 2lishndwa kufanya maamuzi sahihi 2kaangukiwa kudanganywa na Tabasamu la KINAFIKI la The King of Embazzlement Mhe:FISADI JK wa pili.

Hapo kwenye red,huyu ni mmoja wapo waliosemwa na kada wa CCJ kuwa wanafikiri kwa kutumia matumbo yao kama sikosei.
 
sasa mchungaji unaonaje uende wewe unayejiona kichwa chako kinafanya kazi? Anza kujiandaa kugombea

Tanzania tupo zaidi ya Mil 40, ninaamini kati yetu wapo walio bora zaidi. Tunahitaji mtu mwenye uchungu na vision ya kuleta maendeleo....tumechoka na sanaa na maigizo
 
Nguvu ya mabadiliko Tanzania inakuja kwa kasi ya ajabu. Hakuna kinachoweza kuzuia nguvu ya umma. Kila sehemu ya maisha wananchi wa kada zote wanaonyesha kutofurahia serikali iliyopo madarakani. Ugumu wa maisha na kushamiri kwa rushwa ni kero kubwa kwa Mtanzania wa kawaida. Unachokiona hapa JF pamoja na propaganda lakini ni wazi watetezi wa serikali ya Magamba huwa hawana hoja, nimepitia Twitter, Facebook na blog nyingi zinazoongozwa na watanzania kote huko serikali inachanwa mno. Pamoja na kuwa na watetezi wa mafisadi lakini ninaona kabisa wimbi hili litatufikisha mahali pazuri. Nimeongea na jamaa yangu yuko hazina pale wizara ya fedha kutaka kujua ukweli wa uchumi wetu, alichonijibu hakuna na anachofanya Jairos bungeni. Uchumi wetu umeathirika sana na mgawo wa umeme. Lakini kunapropaganda eti uchumi unakuwa hii ni kumdanganya nani....hata sisi tusiojua hata zile theories of economic development tunaona inflation inavyokuwa kwa kasi. Wataalamu wanaambiwa wachakachue takwimu ili waziri aweze ongea kile ambacho serikali inapenda kukisikia.

You cant change the wind of changes .......aluta continua pamoja tunaweza epusha nchi yetu kutoka kwa mafisadi hawa.

Jamaa wa magamba wanaweza kukwambia umeiba mawazo yao ambayo yapo kwenye ilani ya uchaguzi
 
Jamaa wa magamba wanaweza kukwambia umeiba mawazo yao ambayo yapo kwenye ilani ya uchaguzi

Teh teh teh

Wameishiwa hoja imebakia kutishia wanamapinduzi wa kweli, kutumia rushwa na kuwalaghai kwa pesa na ahadi za uongozi U-DC na U-RC. Wao wanapesa sisi tuna Mungu.
 
Reverend, ni wazi kwamba JK nchi imemshinda na sioni dalili yoyote kwamba ana uwezo wa kuirejesha nchi kwenye mstari. Lakini kibaya zaidi ni kwamba HAJALI. Ni jukumu la sisi wananchi sasa kuamua. Kamwe tusikubali kuiona nchi yetu ikizidi kwenda mrama. Saa ya Ukombozi ni Sasa.
 
Kuna siku nilikuwa nimekaa na mwanajeshi mmoja mstaafu pande zile za kitunda, katika vikao vya pombe siku izi haipiti nusu saa bila kuongelea hali ya maisha ya mtanzania, sana sana kumuongelea bwana rais. Jamaa alisema anamsifu JK, wadau tukabaki midomo wazi kwamba kivipi? alidai anamsifu kwa kuonyesha uongozi wake unakotupeleka! Seriosly sa ivi mpaka watoto wadogo wanamsema huyu jamaa, kila rika sasa ni huyu baba wa nchi tu anatajwa kwasababu ya maisha kuwa magumu, si kwenye daladala, nyumbani, bar, nk. Mungu tusaidie
 
hapo kwenye red, kuna wimbo mmoja huwa nausikiliza na kupata hisia kali juu ya hii theory ya change.
Haya mambo yako wazi na hata ukiangalia jinsi hawa jamaa wanavyojibu ni wazi 'wanasikilizia'!
Alafu kujustify post yako, kuna watu wanadai eti tumuachie mkulu JK amalizie miaka yake 4.5 iliyobaki lakini ni mi9ngi mno. Nchi inaweza kuwa zaidi ya bunkrupt ...I mean kama sasa tupo negative -10 miaka minne baadae inaweza kuwa negative -55.
Nguvu ya mabadiliko Tanzania inakuja kwa kasi ya ajabu. Hakuna kinachoweza kuzuia nguvu ya umma. Kila sehemu ya maisha wananchi wa kada zote wanaonyesha kutofurahia serikali iliyopo madarakani. ....

You cant change the wind of changes .......aluta continua pamoja tunaweza epusha nchi yetu kutoka kwa mafisadi hawa.
 
sasa mchungaji unaonaje uende wewe unayejiona kichwa chako kinafanya kazi? Anza kujiandaa kugombea
Ninarudia tena na tena na tena siyo mchungaji tu yeyote kati watz mil 40 anaweza kuwa rais mzuri kuliko JK. We are fed uPPPPPPPPP!!!!!!!!!!!!!
 
Nguvu ya mabadiliko Tanzania inakuja kwa kasi ya ajabu. Hakuna kinachoweza kuzuia nguvu ya umma. Kila sehemu ya maisha wananchi wa kada zote wanaonyesha kutofurahia serikali iliyopo madarakani. Ugumu wa maisha na kushamiri kwa rushwa ni kero kubwa kwa Mtanzania wa kawaida. Unachokiona hapa JF pamoja na propaganda lakini ni wazi watetezi wa serikali ya Magamba huwa hawana hoja, nimepitia Twitter, Facebook na blog nyingi zinazoongozwa na watanzania kote huko serikali inachanwa mno. Pamoja na kuwa na watetezi wa mafisadi lakini ninaona kabisa wimbi hili litatufikisha mahali pazuri. Nimeongea na jamaa yangu yuko hazina pale wizara ya fedha kutaka kujua ukweli wa uchumi wetu, alichonijibu hakuna na anachofanya Jairos bungeni. Uchumi wetu umeathirika sana na mgawo wa umeme. Lakini kunapropaganda eti uchumi unakuwa hii ni kumdanganya nani....hata sisi tusiojua hata zile theories of economic development tunaona inflation inavyokuwa kwa kasi. Wataalamu wanaambiwa wachakachue takwimu ili waziri aweze ongea kile ambacho serikali inapenda kukisikia.

You cant change the wind of changes .......aluta continua pamoja tunaweza epusha nchi yetu kutoka kwa mafisadi hawa.


Nimependa saaana in blue.... Na ikifika hata asiyejua anagundua kua sasa

Uchumi wa nchi una matatizo.... Harufu mbaya ita explode wakati wowote

pamoja na kauli ya kusema ni Nchi ya Ukarimu na Amani....
 
Back
Top Bottom