Maoni: Ifanyike tathmini ya Uchaguzi wa 2019/2020 kabla ya kufanyika uchaguzi 2024/2025

Rabbon

JF-Expert Member
Apr 16, 2022
15,125
22,616
Salaam, shalom.

Baada ya kumsikiliza Kwa makini Mzee WARIOBA akihojiwa katika kipindi Cha Dakika 45 kituo Cha ITV, Kuna mambo nimeyatambua Mzee anajaribu Kutoa angalizo na umuhimu wa Serikali kutathmini kilichojiri 2020 Ili kuepuka KURUDIA changamoto zile zile.

Mzee Warioba amejaribu kuongea jambo zito Kwa Ulimi wa BUSARA kubwa sana kuisaidia Serikali na chama chake kuwa makini na uchaguzi ujao ili jambo muhimu la Katiba mpya na Tume huru ya Uchaguzi lizingatiwe kabla ya kuingia uchaguzi wowote ujao.

TATHMINI HIYO ILENGE KUJUA YAFUATAYO.

1. NINI HASA KILITOKEA 2020.

Kuhusu HOJA hii, ni Rahisi kupata majibu sababu zipo hatua kadhaa zimefanyika kujaribu kuondoa sintofahamu Ile ,japo hapakuwa na Nia ya dhati.

2. FAIDA ZA KUINGIA UCHAGUZI 2024/2025 BILA TUME HURU YA UCHAGUZI NA KATIBA MPYA.

Ikiwa zipo faida, naamini zitakuwa chache sana Hasa Kwa wananchi japo UKWELI ni kuwa Kila jambo Lina pande mbili.

3. HASARA ZA KUINGIA UCHAGUZI 2024/2025 BILA TUME HURU YA UCHAGUZI NA KATIBA MPYA.

HASARA Kwa nionavyo Mimi, ni nyingi kuliko faida.


- KISIASA
Imani ya wananchi kushiriki uchaguzi Iko chini sana, tumeona mwitikio wa wananchi kushiriki uchaguzi Ukiwa chini sana, inahitajika TATHMINI ya kina nini kifanyike kuleta ongezeko la wananchi kuhusu kushiriki shughuli za kisiasa.

Kasoro na Matukio ya kura fake zilizoripotiwa Bado limeweka Imani ya wananchi kushiriki uchaguzi kuwa chini sana.

- KIUCHUMI
Uchaguzi wa HAKI, una mchango mkubwa sana Kwa wananchi katika kuinua Uchumi,

Ikiwa yaliyojiri 2020 yatajirudia, tutegemee kuona Uchumi ukidorora zaidi.

- KIJAMII
Muungano na ushirikiano wa wananchi ndani ya JAMII ulitatatizika sana Kwa yaliyojiri 2020, hivyo kuingia tena uchaguzi wa 2024/2025 kama vipofu Si sawa.

- KIUSALAMA
Si sawa kuwekeza katika kununua silaha na mabomu ya machozi nk nk nk, kuminya DEMOKRASIA.

4. ZIPI ZITAKUWA FAIDA ZA KUSOGEZA MBELE UCHAGUZI WA MITAA 2024?

Iwapo uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliopangwa kufanyika 2024 utasogezwa mbele, tutafanikiwa kukata cost ya Uchaguzi Kwa 50% sababu uchaguzi utakuwa mmoja tu 2025 , unachagua mkt, diwani, mbunge Hadi Rais.

HITIMISHO.

Ni muhimu kuhakikisha changamoto zilizojitokeza 2020 zikatatuliwa tukaingia tukiwa na Katiba mpya na Tume huru ya Uchaguzi Ili pasiwepo kitisho kikubwa Cha USALAMA, maana uchaguzi katika Nchi nyingi imekuwa chanzo Cha kutetereka Kwa USALAMA na Amani.

NB: Wazee wa Aina ya Mzee Warioba ni hazina ya Taifa letu. Kuwapuuza ni kujichimbia mashimo ambayo hatokuwepo Jirani wa kutusaidia ikiwa tutajitumbukiza.

Mungu ibariki Nchi yangu nzuri niipendayo TANZANIA 🇹🇿

Amen.
 
Wakati wa bajeti ya 2024-2025 jambo hilo litawekwa mezani, kutathminiwa kwa kina, kujadiliwa, kupendekeza marekebisho ya kisheria, sera na utaratibu wa uchaguzi ili kurekebisha kasoro mbalimbali zilizojitokeza chaguzi za huko kale na hatimae kupitisha gharama za jumla za uchaguzi wenyewe, ili uwe bora zaidi, huru zaidi, wa haki zaidi na wa uwazi zaidi ya chaguzi zozote zilizowahi kufanyika tanzania.....
 
wakati wa bajeti ya 2024-2025 jambo hilo litawekwa mezani, kutathminiwa kwa kina, kujadiliwa, kupendekeza marekebisho ya kisheria, sera na utaratibu wa uchaguzi ili kurekebisha kasoro mbalimbali zilizojitokeza chaguzi za huko kale na hatimae kupitisha gharama za jumla za uchaguzi wenyewe, ili uwe bora zaidi, huru zaidi, wa haki zaidi na wa uwazi zaidi ya chaguzi zozote zilizowahi kufanyika tanzania.....
Nani kakwambia Gharama za uchaguzi ni chanzo ya kuvurugwa uchaguzi wa 2020?
 
Sijamaanisha hivyo, na ni kitu muhimu lakini ni sawa na kumfunga paka kengele.
Ndo sasa Wazee waona mbali wanaahauri TATHMINI ya kina kufanyika maana uchaguzi ujao 2025 hautabiriki!!
 
Mkuu

Bado hukuona uchaguzi mkuu 2025!!?

Na badala yke 2026 tutakua tunaendelea kuandika katiba!!?bado unaona hivyo au maono yamebadilika!?

NB

Hakutokua na mabomu ya machozi coz watz hawawezi andamana na sio utamaduni wetu,ishu ya katiba hi ya dola ndio iamue kwaajili ya wnanchi coz wananchi tulishatoa maoni yetu na Katiba ipo ni kuipigia kura tu!!


Naona mzee warioba katumwa ujumbe na kaufikisha kuwa uchaguzi kwa katibai iliyopo haupo hadi katiba mpya!

Dola imeanza kuchanga karata zake!!
 
Kwanini Tume huru ya Uchaguzi inayomtenga Rais kuingilia uchaguzi inapigwa Dana Dana?
mchakato wa katiba mpya 2026 utakapofufuliwa, sintofahamu na mashaka juu ya jambo hili iatajadiliwa na wananchi wate kwa uhuru na uwazi na kupendekeza jambo hili liwe na sura gani ili liaminike kwa wananchi wote.

subra ya vuta kheri, hakuna danadana,
mambo ni mengi muda mchache, tupo pazuri, tunaenda pazuri, tunaelekea pazuri zaidi...
 
Nadhani suala la Katiba Mpya liendewe kimkakati kwa kuanza na reformation kwa maeneo kadhaa kabla ya kulivaa mazima. Issue za muundo wa Tume ya Uchaguzi,matokeo ya Rais kupingwa mahakamani, na maeneo mengi katiba pendekezwa ya Samwel Sitta ingefaa.
 
Ikitupendeza uchaguzi ufanywe hata October 2026,kwa kuundwa serikali ya mpito chini ya Rais huyu huyu,ili suala la KATIBA MPYA ILIYO BORA na TUME HURU ya uchaguzi vipatikane..ila kufanya uchaguzi kwa Katiba hii KUU KUU na tume hii MBOFU MBOFU,itakuwa ni sawa na kupaka Upepo RANGI...wakati wa KATIBA MPYA iliyobora ni SASA
 
mchakato wa katiba mpya 2026 utakapofufuliwa, sintofahamu na mashaka juu ya jambo hili iatajadiliwa na wananchi wate kwa uhuru na uwazi na kupendekeza jambo hili liwe na sura gani ili liaminike kwa wananchi wote...
2024 inatosha kupata Tume huru ya Uchaguzi na KATIBA mpya ikiwa RASIMU ya WARIOBA itawekwa mezani.

Rasimu ya Warioba inatosha kufanyika kitu Cha kuanzia na tukaingia uchaguzi tukiwa na Tume huru ya Uchaguzi isiyo na Mkono wa Rais.

2026 ni mwaka wa kukamilika KATIBA mpya,Si mwaka wa kufufuka mchakato.
 
Back
Top Bottom