Mandela Road: Barabara iliojengwa kwa viwango stahiki

Hongera kwa kutoa kongole. Nakumbuka kuna siku niliamua nitoa uchovu wa mwili nikaamua kukanyaga kwa mguu kutoka Ubungo mpaka Mwenge, yaan nilitembea bila bughudha eneo la watembea kwa miguu. Aliyeijenga kuanzia mtoa tenda na mpokeaji wapewe ponfezi walizingatia mambo ya muhimu.

Ila mkuu samahani hiyo camera yako inaumwa mafua?
HIyo ni Sam Nujoma road sio Mandela road
 
Ilijengwa/ilikarabatiwa tena kipindi Cha Jakaya Kikwere na makandarasi MALTAURO-SPENKON kuanzia mwaka 2008- 2011 toka bandarini mpaka Ubungo mataa. Ile ya Mowlem ilibomolewa
huyo kachanganya hiyo ni Sam Nujoma road sio Mandela expressway unayoiongelea
 
Hii barabara pichani kwa jina MANDELA Road, ndio barabara yangu yenye ubora kabisa.

Kwanza, imedumu bila kubonyea bonyea, kuweka mabigijii kama ilivyo baadhi ya barabara zenye heavy traffic

Pili, imezingatia haki za watumiaji wote. Inayo sehemu ya mapitio ya dharura, waenda kwa miguu na magari pande mbili.

Ina mifereji mipana saafii inayopitisha maji vizuri.

My take:
Mkandarasi aliejenga hii apewe tena kazi ya barabara muhimu kv Moro Kibaha Express Lane nk. Heko alempa kazi na standards za kuzingatiwa.

Huu ni mfano bora.

UZI TAYARI

View attachment 2869540View attachment 2869542
Sasa mbona naona picha za sam nujoma road??
 
Mandela Road inaanzia Bandarini mpaka Ubungo Mataa.

Sam Nujoma Road inaanzia Ubungo Mata hadi Mwenge.

Picha ulizozipiga ni za Sam Nujoma Road na siyo Mandela Road
 
Hahahahaha😀😀😀
Jielimishe kwanza. Hiyo sio Mandela Rd, ni Sam Nujoma Rd.
Hiyo barabara ina mazingira mazuri tu inavutia kuendesha, lakini haina ubora. Lau magari yanayopita Mandela Rd yanayobeba macontainer na heavy traffics yangekuwa yanapita hapo usingeisifia hiyo barabara.

Aliyejenga Mandela Rd yenyewe kuanzia Ubungo hadi Kurasini naomba tumsifu, kajitahidi sana. Mabigijii yapo, hasa sehemu ambazo kuna traffic lights kwa sababu magari mazito yanasimama kwa muda kama pale Serengeti na Tabata. Ila angalau amethubutu.
Kweli Kabisa mkúu huyo mkandarasi apewe Maua Yake.

Na aliyejenga kipande cha Shinyanga hadi Mabuki hao watu walikuwa watu kwerikweri
 
Kutoka Chalinze kwenda Morogoro barabara hii naikubali sana

Moja ya kipande kizuri sana cha lami zilizopo Tanzania...mahali pabaya ni ninapokumbuka ni maeneo ya Bwawani na Mikese...
 
Kipande kingine bora na pengine kilichodumu muda mrefu kwa barabara za Dar ni barabara ya Ali Hassan Mwinyi kipande cha kuanzia Maktaba hadi Morocco (Morocco kwenda Mwenge kimejengwa upya)...

Hii barabara kwa kumbukumbu zangu nadhani ilijengwa 1993/94 hapo, sijui kama iliwahi bomolewa na kujengwa tena...
 
Hahahahaha😀😀😀
Jielimishe kwanza. Hiyo sio Mandela Rd, ni Sam Nujoma Rd.
Hiyo barabara ina mazingira mazuri tu inavutia kuendesha, lakini haina ubora. Lau magari yanayopita Mandela Rd yanayobeba macontainer na heavy traffics yangekuwa yanapita hapo usingeisifia hiyo barabara.

Aliyejenga Mandela Rd yenyewe kuanzia Ubungo hadi Kurasini naomba tumsifu, kajitahidi sana. Mabigijii yapo, hasa sehemu ambazo kuna traffic lights kwa sababu magari mazito yanasimama kwa muda kama pale Serengeti na Tabata. Ila angalau amethubutu.

Mandela road yenyewe imejengwa miaka ya 1970s.. na mpaka leo haijawai kurekebishwa rekebishwa kama zingine
 
Back
Top Bottom