Mambo yanayotuunganisha watanzania ni yepi?

Shibalanga

Senior Member
Mar 1, 2011
178
93
Ndugu zangu, naomba tusaidiane kwa pamoja kutambua mambo ambayo sisi kama watanzania bila kujali itikadi za siasa, dini, Rangi, kabila,kanda na jinsia; mwisho wa siku yanaturudisha pamoja kama wananchi wazalendo wa nchi hii.

Binafsi, nimekuwa nikijiuliza sana swali hili nakosa jibu, na hii ni kutokana kushuhudia minyukano ya kisiasa, kidini, kiuchumi na kitabaka ambayo hali hii imepelekea sasa kila kukicha ni malalamiko,maandamano,tuhuma, mauaji, vitisho, ubabe; Kiasi kwamba inataka kuonekana kana kwamba Tanzania si pahala pazuri pa kuishi.

Ndugu zangu, najua humu kuna watu makini sana waliobobea katika nyanja mbalimbali na kutokana na umuhimu huo mlio nao hebu kwa pamoja tutambue ni mambo gani ambayo mwisho wa siku sitakuwa na haja ya kutambua huyu ni wa CUF, CHADEMA,CCM, MWISLAM, MKRISTO, MPAGANI, KIJANA, MZEE, MTOTO, PROFESA,MKULIMA N.K lakini tunakuwa kitu kimoja?
Nisaidieni tafadhali.
 
kISWAHILI WAKATI FULANI SASA KINAPOTEA! UTAIFA UMEPOTEA (Chenge anataka DOWAN walipwe) sioni kilicho baki cha kutuunganisha watz
 
Yapo mengi cha msingi ni kujiuliza kutuunganisha katika lipi?
Kuna wakati watu wa itikadi na vyama tofauti tunaunganishwa na mpira.
Kuna wakati watu wa timu tofauti tunaunganishwa na dini.
Kuna wakati watu wa dini tofauti tunaunganishwa na siasa.
Hayo hapo juu pia ukiamua kuyageuza unavyotaka bado yataleta maana ileile.
Pia ukiyatazama kwa upande wa pili yanayotuunganisha na huyu ndiyo yanayotutenganisha na yule.
 
Cha kutuunganisha ni "Utanzania", na kiswahili ndo fahari yetu. Tutatofautiana katika mambo mengi sana, ila mwisho wa siku sote tutabaki kuwa ni watanzania na tutaimba kwa pamoja wimbo wetu wa taifa la Tanzania katika lugha yetu ya kiswahili.
 
Kilichotuunganisha ni aina fulani ya system ya maisha ya kila siku aliyoanzisha mwalimu,maisha fulani ya ujamaa!
Hiyo ladha ilianza kupotea wakati wa Mkapa, awamu hii ya nne ndo kabisaaaaaa!!!
Nguvu za giza nyingi imetawala live.
 
njaa ndo inatuunganisha
uchaguzi pia hasa wakati wa kampeni
lakini simba na yanga vinatukusanya na kututenganisha
 
Asanteni! kama hayo mliyoyasema ndo yanatuunganisha sawa, nyie si ndo wataalam bwana niliowahitaji!
 
Back
Top Bottom