Mambo ya muhimu kuzingatia kwa wale tunaoomba kazi

A man with one idea

Senior Member
Jul 18, 2022
126
264
Kwa wanaotafuta kazi hii inawahusu sana.CV yako hakikisha haina haya makosa
_______________________
Wiki iliyopita nilipata nafasi ya kuchakata maombi ya kazi ya taasisi moja binafsi hapa nchini. Maombi takribani 450 yalipokelewa ya wahitimu wa vyuo mbali mbali.

Ninashauri tufikirie namna tunavyoweza kujipanga na kuelimishana namna sahihi ya kufanya maombi ya ajira. Yapo makosa madogo madogo yaliyofanya tuwatoe katika ushindani takribani 50% ya waombaji wote bila hata kuangalia CV au vyeti vyao.

Baadhi ya makosa niliyoyaona ni kama ifuatavyo;

1. Emails nyingi zilitumwa bila heading. Yani email haisemi ni ya nini. Au mtu anaandika "Application", au anaandika "My cv", au "Dear sir". Hayo yote ni makosa. Kwa kawaida unapaswa kuandika heading ya email yako in a title cased format ikitaja nafasi unayoomba. Kwa mfano "Application for Tutorial Assistant in Mathematics"

2. Emails nyingi zilizokosewa heading. Yani heading na kilichomo ni tofauti. Mtu ameandika "Application for Tutorial Assistant in Mathematics" lakini ukifungua barua yake ya maombi ameomba nafasi ya Estate Manager. Mara nyingi hutokea ikiwa ofisi imetangaza nafasi zaidi ya moja.

3. Kulikua na "blank emails". Yani mtu ametuma email anasema "please see the attachments" lakini hajaambatanisha attachment hata moja.

4. Kuna mtu ametuma email yenye attachments tu bila kuandika chochote sehemu ya ujumbe. Hilo ni kosa. Andika sentensi mbili au tatu. Kwa mfano "Dear sir/Madam, please see my attached credentials applying for the Tutorial Assistant post"

5. Weka attachment ulizoelekezwa tu. Kama mwajiri anataka CV na Cover letter usiattach certificate unless awe anataka na certificate pia. Na hata ukiambiwa attach certificate weka zile za muhimu tu. Sio unaweka cheti cha primary, cha ubatizo au Living certificate ya form four/six.

6. Attachments zote lazima uzipe majina kabla ya kuattach. Mfano cv inatakiwa isomeke Peter Elia CV - Tutoria Assistant Post au vinginevyo ili mradi mtu akiidownload asihitaji kulazimika kui-rename. Elewa kwamba waombaji ni wengi na anayefungua hizo attachment ni mtu mmoja au wawili. Fanya maisha yawe mepesi. Hakuna mtu ana muda wa kufungua attachment yako na kuirename wakati wapo walioattach kwa kuzipa majina attachment zao.

7. Poor scanned documents. Tuache uvivu. Usiscan kwa kutumia simu ya mkononi. Andaa copy nzuri ya nakala ya vyeti vyako tumia scanner nzuri, na ikiwezekana save kabisa kwenye "email" yako ili siku yoyote ukivihitaji uvipate.

8. CV format. Kuna watu wanafanya utani na CV zao. Yani unakutana na CV ina font size tofauti kila section, font types tofauti, spelling errors hadi kwenye majina yako. Hapa ukikosa kazi huna wa kumlaumu.

9. Usitumie majina tofauti na yaliyopo kwenye vyeti vyako. Kama vyeti vyako vimeandikwa Peter Elia Mosha usiandike Peter Elia au Peter Mosha. Hao ni watu wawili tofauti.

10. Acha kutumia email uliyofungua ulipokuwa "teenager" enzi ukiwa na miaka 16. Unakuta mtu anaitwa Peter Elia lakini email yake ni snakeboy@yahoo.com AU mafisi77@yahoo.co.uk. Tengeneza email yenye majina yako na isajili kwa majina yako halisi. Kwa mfano kama unaitwa Peter Elia unaweza kutumia peterelia@gmail.com

11. Usitumie email ya mtu mwingine kutuma maombi. Tuache uzembe. Yaani kama natafuta mtu mmoja kati ya watu 450 niambie kwa nini nimchukue mtu ambaye hana hata email address? Tengeneza email yako na hakikisha unatuma maombi kwa email yako mwenyewe, sio email ya mtu. Siku hizi dakika 5 tu zinatosha kutengeneza email account.

12. Epuka kuchanganya herufi. Hata kama una shida ya lafudhi, jitahidi iwe kwenye kuongea tu lakini sio kwenye kuandika. Mfano hela - ela, rejea - lejea, afadhali - afazali. Sasa hivi kuna mtindo mpya wa xa badala ya sa. Na hawakubali kurekebishwa. Mwisho wa siku utasikia "my wangu nimekutumia ujumbe mpaka xaxa ujanijibu jomoni"
_____
TAKE A SERIOUS NOTE. Maombi ya kazi ni jambo serious sio mambo ya JOMONI.!
 
Kwa wanaotafuta kazi hii inawahusu sana.CV yako hakikisha haina haya makosa
_______________________
Wiki iliyopita nilipata nafasi ya kuchakata maombi ya kazi ya taasisi moja binafsi hapa nchini. Maombi takribani 450 yalipokelewa ya wahitimu wa vyuo mbali mbali.

Ninashauri tufikirie namna tunavyoweza kujipanga na kuelimishana namna sahihi ya kufanya maombi ya ajira. Yapo makosa madogo madogo yaliyofanya tuwatoe katika ushindani takribani 50% ya waombaji wote bila hata kuangalia CV au vyeti vyao.

Baadhi ya makosa niliyoyaona ni kama ifuatavyo;

1. Emails nyingi zilitumwa bila heading. Yani email haisemi ni ya nini. Au mtu anaandika "Application", au anaandika "My cv", au "Dear sir". Hayo yote ni makosa. Kwa kawaida unapaswa kuandika heading ya email yako in a title cased format ikitaja nafasi unayoomba. Kwa mfano "Application for Tutorial Assistant in Mathematics"

2. Emails nyingi zilizokosewa heading. Yani heading na kilichomo ni tofauti. Mtu ameandika "Application for Tutorial Assistant in Mathematics" lakini ukifungua barua yake ya maombi ameomba nafasi ya Estate Manager. Mara nyingi hutokea ikiwa ofisi imetangaza nafasi zaidi ya moja.

3. Kulikua na "blank emails". Yani mtu ametuma email anasema "please see the attachments" lakini hajaambatanisha attachment hata moja.

4. Kuna mtu ametuma email yenye attachments tu bila kuandika chochote sehemu ya ujumbe. Hilo ni kosa. Andika sentensi mbili au tatu. Kwa mfano "Dear sir/Madam, please see my attached credentials applying for the Tutorial Assistant post"

5. Weka attachment ulizoelekezwa tu. Kama mwajiri anataka CV na Cover letter usiattach certificate unless awe anataka na certificate pia. Na hata ukiambiwa attach certificate weka zile za muhimu tu. Sio unaweka cheti cha primary, cha ubatizo au Living certificate ya form four/six.

6. Attachments zote lazima uzipe majina kabla ya kuattach. Mfano cv inatakiwa isomeke Peter Elia CV - Tutoria Assistant Post au vinginevyo ili mradi mtu akiidownload asihitaji kulazimika kui-rename. Elewa kwamba waombaji ni wengi na anayefungua hizo attachment ni mtu mmoja au wawili. Fanya maisha yawe mepesi. Hakuna mtu ana muda wa kufungua attachment yako na kuirename wakati wapo walioattach kwa kuzipa majina attachment zao.

7. Poor scanned documents. Tuache uvivu. Usiscan kwa kutumia simu ya mkononi. Andaa copy nzuri ya nakala ya vyeti vyako tumia scanner nzuri, na ikiwezekana save kabisa kwenye "email" yako ili siku yoyote ukivihitaji uvipate.

8. CV format. Kuna watu wanafanya utani na CV zao. Yani unakutana na CV ina font size tofauti kila section, font types tofauti, spelling errors hadi kwenye majina yako. Hapa ukikosa kazi huna wa kumlaumu.

9. Usitumie majina tofauti na yaliyopo kwenye vyeti vyako. Kama vyeti vyako vimeandikwa Peter Elia Mosha usiandike Peter Elia au Peter Mosha. Hao ni watu wawili tofauti.

10. Acha kutumia email uliyofungua ulipokuwa "teenager" enzi ukiwa na miaka 16. Unakuta mtu anaitwa Peter Elia lakini email yake ni snakeboy@yahoo.com AU mafisi77@yahoo.co.uk. Tengeneza email yenye majina yako na isajili kwa majina yako halisi. Kwa mfano kama unaitwa Peter Elia unaweza kutumia peterelia@gmail.com

11. Usitumie email ya mtu mwingine kutuma maombi. Tuache uzembe. Yaani kama natafuta mtu mmoja kati ya watu 450 niambie kwa nini nimchukue mtu ambaye hana hata email address? Tengeneza email yako na hakikisha unatuma maombi kwa email yako mwenyewe, sio email ya mtu. Siku hizi dakika 5 tu zinatosha kutengeneza email account.

12. Epuka kuchanganya herufi. Hata kama una shida ya lafudhi, jitahidi iwe kwenye kuongea tu lakini sio kwenye kuandika. Mfano hela - ela, rejea - lejea, afadhali - afazali. Sasa hivi kuna mtindo mpya wa xa badala ya sa. Na hawakubali kurekebishwa. Mwisho wa siku utasikia "my wangu nimekutumia ujumbe mpaka xaxa ujanijibu jomoni"
_____
TAKE A SERIOUS NOTE. Maombi ya kazi ni jambo serious sio mambo ya JOMONI.!
umenipa somo kubwa sana. ngoja nizifanyie kazi zile point zinazonihusu
 
Kwa wanaotafuta kazi hii inawahusu sana.CV yako hakikisha haina haya makosa
_______________________
Wiki iliyopita nilipata nafasi ya kuchakata maombi ya kazi ya taasisi moja binafsi hapa nchini. Maombi takribani 450 yalipokelewa ya wahitimu wa vyuo mbali mbali.

Ninashauri tufikirie namna tunavyoweza kujipanga na kuelimishana namna sahihi ya kufanya maombi ya ajira. Yapo makosa madogo madogo yaliyofanya tuwatoe katika ushindani takribani 50% ya waombaji wote bila hata kuangalia CV au vyeti vyao.

Baadhi ya makosa niliyoyaona ni kama ifuatavyo;

1. Emails nyingi zilitumwa bila heading. Yani email haisemi ni ya nini. Au mtu anaandika "Application", au anaandika "My cv", au "Dear sir". Hayo yote ni makosa. Kwa kawaida unapaswa kuandika heading ya email yako in a title cased format ikitaja nafasi unayoomba. Kwa mfano "Application for Tutorial Assistant in Mathematics"

2. Emails nyingi zilizokosewa heading. Yani heading na kilichomo ni tofauti. Mtu ameandika "Application for Tutorial Assistant in Mathematics" lakini ukifungua barua yake ya maombi ameomba nafasi ya Estate Manager. Mara nyingi hutokea ikiwa ofisi imetangaza nafasi zaidi ya moja.

3. Kulikua na "blank emails". Yani mtu ametuma email anasema "please see the attachments" lakini hajaambatanisha attachment hata moja.

4. Kuna mtu ametuma email yenye attachments tu bila kuandika chochote sehemu ya ujumbe. Hilo ni kosa. Andika sentensi mbili au tatu. Kwa mfano "Dear sir/Madam, please see my attached credentials applying for the Tutorial Assistant post"

5. Weka attachment ulizoelekezwa tu. Kama mwajiri anataka CV na Cover letter usiattach certificate unless awe anataka na certificate pia. Na hata ukiambiwa attach certificate weka zile za muhimu tu. Sio unaweka cheti cha primary, cha ubatizo au Living certificate ya form four/six.

6. Attachments zote lazima uzipe majina kabla ya kuattach. Mfano cv inatakiwa isomeke Peter Elia CV - Tutoria Assistant Post au vinginevyo ili mradi mtu akiidownload asihitaji kulazimika kui-rename. Elewa kwamba waombaji ni wengi na anayefungua hizo attachment ni mtu mmoja au wawili. Fanya maisha yawe mepesi. Hakuna mtu ana muda wa kufungua attachment yako na kuirename wakati wapo walioattach kwa kuzipa majina attachment zao.

7. Poor scanned documents. Tuache uvivu. Usiscan kwa kutumia simu ya mkononi. Andaa copy nzuri ya nakala ya vyeti vyako tumia scanner nzuri, na ikiwezekana save kabisa kwenye "email" yako ili siku yoyote ukivihitaji uvipate.

8. CV format. Kuna watu wanafanya utani na CV zao. Yani unakutana na CV ina font size tofauti kila section, font types tofauti, spelling errors hadi kwenye majina yako. Hapa ukikosa kazi huna wa kumlaumu.

9. Usitumie majina tofauti na yaliyopo kwenye vyeti vyako. Kama vyeti vyako vimeandikwa Peter Elia Mosha usiandike Peter Elia au Peter Mosha. Hao ni watu wawili tofauti.

10. Acha kutumia email uliyofungua ulipokuwa "teenager" enzi ukiwa na miaka 16. Unakuta mtu anaitwa Peter Elia lakini email yake ni snakeboy@yahoo.com AU mafisi77@yahoo.co.uk. Tengeneza email yenye majina yako na isajili kwa majina yako halisi. Kwa mfano kama unaitwa Peter Elia unaweza kutumia peterelia@gmail.com

11. Usitumie email ya mtu mwingine kutuma maombi. Tuache uzembe. Yaani kama natafuta mtu mmoja kati ya watu 450 niambie kwa nini nimchukue mtu ambaye hana hata email address? Tengeneza email yako na hakikisha unatuma maombi kwa email yako mwenyewe, sio email ya mtu. Siku hizi dakika 5 tu zinatosha kutengeneza email account.

12. Epuka kuchanganya herufi. Hata kama una shida ya lafudhi, jitahidi iwe kwenye kuongea tu lakini sio kwenye kuandika. Mfano hela - ela, rejea - lejea, afadhali - afazali. Sasa hivi kuna mtindo mpya wa xa badala ya sa. Na hawakubali kurekebishwa. Mwisho wa siku utasikia "my wangu nimekutumia ujumbe mpaka xaxa ujanijibu jomoni"
_____
TAKE A SERIOUS NOTE. Maombi ya kazi ni jambo serious sio mambo ya JOMONI.!
Andiko zuri sana vp suala la connection maana unaweza timiza yote hayo bila connection wanasema ni kazi bure, nini maoni yako
 
Kwa wanaotafuta kazi hii inawahusu sana.CV yako hakikisha haina haya makosa
_______________________
Wiki iliyopita nilipata nafasi ya kuchakata maombi ya kazi ya taasisi moja binafsi hapa nchini. Maombi takribani 450 yalipokelewa ya wahitimu wa vyuo mbali mbali.

Ninashauri tufikirie namna tunavyoweza kujipanga na kuelimishana namna sahihi ya kufanya maombi ya ajira. Yapo makosa madogo madogo yaliyofanya tuwatoe katika ushindani takribani 50% ya waombaji wote bila hata kuangalia CV au vyeti vyao.

Baadhi ya makosa niliyoyaona ni kama ifuatavyo;

1. Emails nyingi zilitumwa bila heading. Yani email haisemi ni ya nini. Au mtu anaandika "Application", au anaandika "My cv", au "Dear sir". Hayo yote ni makosa. Kwa kawaida unapaswa kuandika heading ya email yako in a title cased format ikitaja nafasi unayoomba. Kwa mfano "Application for Tutorial Assistant in Mathematics"

2. Emails nyingi zilizokosewa heading. Yani heading na kilichomo ni tofauti. Mtu ameandika "Application for Tutorial Assistant in Mathematics" lakini ukifungua barua yake ya maombi ameomba nafasi ya Estate Manager. Mara nyingi hutokea ikiwa ofisi imetangaza nafasi zaidi ya moja.

3. Kulikua na "blank emails". Yani mtu ametuma email anasema "please see the attachments" lakini hajaambatanisha attachment hata moja.

4. Kuna mtu ametuma email yenye attachments tu bila kuandika chochote sehemu ya ujumbe. Hilo ni kosa. Andika sentensi mbili au tatu. Kwa mfano "Dear sir/Madam, please see my attached credentials applying for the Tutorial Assistant post"

5. Weka attachment ulizoelekezwa tu. Kama mwajiri anataka CV na Cover letter usiattach certificate unless awe anataka na certificate pia. Na hata ukiambiwa attach certificate weka zile za muhimu tu. Sio unaweka cheti cha primary, cha ubatizo au Living certificate ya form four/six.

6. Attachments zote lazima uzipe majina kabla ya kuattach. Mfano cv inatakiwa isomeke Peter Elia CV - Tutoria Assistant Post au vinginevyo ili mradi mtu akiidownload asihitaji kulazimika kui-rename. Elewa kwamba waombaji ni wengi na anayefungua hizo attachment ni mtu mmoja au wawili. Fanya maisha yawe mepesi. Hakuna mtu ana muda wa kufungua attachment yako na kuirename wakati wapo walioattach kwa kuzipa majina attachment zao.

7. Poor scanned documents. Tuache uvivu. Usiscan kwa kutumia simu ya mkononi. Andaa copy nzuri ya nakala ya vyeti vyako tumia scanner nzuri, na ikiwezekana save kabisa kwenye "email" yako ili siku yoyote ukivihitaji uvipate.

8. CV format. Kuna watu wanafanya utani na CV zao. Yani unakutana na CV ina font size tofauti kila section, font types tofauti, spelling errors hadi kwenye majina yako. Hapa ukikosa kazi huna wa kumlaumu.

9. Usitumie majina tofauti na yaliyopo kwenye vyeti vyako. Kama vyeti vyako vimeandikwa Peter Elia Mosha usiandike Peter Elia au Peter Mosha. Hao ni watu wawili tofauti.

10. Acha kutumia email uliyofungua ulipokuwa "teenager" enzi ukiwa na miaka 16. Unakuta mtu anaitwa Peter Elia lakini email yake ni snakeboy@yahoo.com AU mafisi77@yahoo.co.uk. Tengeneza email yenye majina yako na isajili kwa majina yako halisi. Kwa mfano kama unaitwa Peter Elia unaweza kutumia peterelia@gmail.com

11. Usitumie email ya mtu mwingine kutuma maombi. Tuache uzembe. Yaani kama natafuta mtu mmoja kati ya watu 450 niambie kwa nini nimchukue mtu ambaye hana hata email address? Tengeneza email yako na hakikisha unatuma maombi kwa email yako mwenyewe, sio email ya mtu. Siku hizi dakika 5 tu zinatosha kutengeneza email account.

12. Epuka kuchanganya herufi. Hata kama una shida ya lafudhi, jitahidi iwe kwenye kuongea tu lakini sio kwenye kuandika. Mfano hela - ela, rejea - lejea, afadhali - afazali. Sasa hivi kuna mtindo mpya wa xa badala ya sa. Na hawakubali kurekebishwa. Mwisho wa siku utasikia "my wangu nimekutumia ujumbe mpaka xaxa ujanijibu jomoni"
_____
TAKE A SERIOUS NOTE. Maombi ya kazi ni jambo serious sio mambo ya JOMONI.!
Asante kwa somo. Ingawa haya yote nimeyazingatia sana na ni mwaka wa 6 sasa hivi hakuna matumaini ya kupata ajira.
 
Kwa wanaotafuta kazi hii inawahusu sana.CV yako hakikisha haina haya makosa
_______________________
Wiki iliyopita nilipata nafasi ya kuchakata maombi ya kazi ya taasisi moja binafsi hapa nchini. Maombi takribani 450 yalipokelewa ya wahitimu wa vyuo mbali mbali.

Ninashauri tufikirie namna tunavyoweza kujipanga na kuelimishana namna sahihi ya kufanya maombi ya ajira. Yapo makosa madogo madogo yaliyofanya tuwatoe katika ushindani takribani 50% ya waombaji wote bila hata kuangalia CV au vyeti vyao.

Baadhi ya makosa niliyoyaona ni kama ifuatavyo;

1. Emails nyingi zilitumwa bila heading. Yani email haisemi ni ya nini. Au mtu anaandika "Application", au anaandika "My cv", au "Dear sir". Hayo yote ni makosa. Kwa kawaida unapaswa kuandika heading ya email yako in a title cased format ikitaja nafasi unayoomba. Kwa mfano "Application for Tutorial Assistant in Mathematics"

2. Emails nyingi zilizokosewa heading. Yani heading na kilichomo ni tofauti. Mtu ameandika "Application for Tutorial Assistant in Mathematics" lakini ukifungua barua yake ya maombi ameomba nafasi ya Estate Manager. Mara nyingi hutokea ikiwa ofisi imetangaza nafasi zaidi ya moja.

3. Kulikua na "blank emails". Yani mtu ametuma email anasema "please see the attachments" lakini hajaambatanisha attachment hata moja.

4. Kuna mtu ametuma email yenye attachments tu bila kuandika chochote sehemu ya ujumbe. Hilo ni kosa. Andika sentensi mbili au tatu. Kwa mfano "Dear sir/Madam, please see my attached credentials applying for the Tutorial Assistant post"

5. Weka attachment ulizoelekezwa tu. Kama mwajiri anataka CV na Cover letter usiattach certificate unless awe anataka na certificate pia. Na hata ukiambiwa attach certificate weka zile za muhimu tu. Sio unaweka cheti cha primary, cha ubatizo au Living certificate ya form four/six.

6. Attachments zote lazima uzipe majina kabla ya kuattach. Mfano cv inatakiwa isomeke Peter Elia CV - Tutoria Assistant Post au vinginevyo ili mradi mtu akiidownload asihitaji kulazimika kui-rename. Elewa kwamba waombaji ni wengi na anayefungua hizo attachment ni mtu mmoja au wawili. Fanya maisha yawe mepesi. Hakuna mtu ana muda wa kufungua attachment yako na kuirename wakati wapo walioattach kwa kuzipa majina attachment zao.

7. Poor scanned documents. Tuache uvivu. Usiscan kwa kutumia simu ya mkononi. Andaa copy nzuri ya nakala ya vyeti vyako tumia scanner nzuri, na ikiwezekana save kabisa kwenye "email" yako ili siku yoyote ukivihitaji uvipate.

8. CV format. Kuna watu wanafanya utani na CV zao. Yani unakutana na CV ina font size tofauti kila section, font types tofauti, spelling errors hadi kwenye majina yako. Hapa ukikosa kazi huna wa kumlaumu.

9. Usitumie majina tofauti na yaliyopo kwenye vyeti vyako. Kama vyeti vyako vimeandikwa Peter Elia Mosha usiandike Peter Elia au Peter Mosha. Hao ni watu wawili tofauti.

10. Acha kutumia email uliyofungua ulipokuwa "teenager" enzi ukiwa na miaka 16. Unakuta mtu anaitwa Peter Elia lakini email yake ni snakeboy@yahoo.com AU mafisi77@yahoo.co.uk. Tengeneza email yenye majina yako na isajili kwa majina yako halisi. Kwa mfano kama unaitwa Peter Elia unaweza kutumia peterelia@gmail.com

11. Usitumie email ya mtu mwingine kutuma maombi. Tuache uzembe. Yaani kama natafuta mtu mmoja kati ya watu 450 niambie kwa nini nimchukue mtu ambaye hana hata email address? Tengeneza email yako na hakikisha unatuma maombi kwa email yako mwenyewe, sio email ya mtu. Siku hizi dakika 5 tu zinatosha kutengeneza email account.

12. Epuka kuchanganya herufi. Hata kama una shida ya lafudhi, jitahidi iwe kwenye kuongea tu lakini sio kwenye kuandika. Mfano hela - ela, rejea - lejea, afadhali - afazali. Sasa hivi kuna mtindo mpya wa xa badala ya sa. Na hawakubali kurekebishwa. Mwisho wa siku utasikia "my wangu nimekutumia ujumbe mpaka xaxa ujanijibu jomoni"
_____
TAKE A SERIOUS NOTE. Maombi ya kazi ni jambo serious sio mambo ya JOMONI.!
Umenitoa tongo tongo na nondo hii hakika iko smart imenifanya nijiweke sawa vitu fulani.
 
Asante kwa somo. Ingawa haya yote nimeyazingatia sana na ni mwaka wa 6 sasa hivi hakuna matumaini ya kupata ajira.
Kaza buti tu mkuu hakuna namna ni kusonga mbele imeshakuwa vitu ukirudi nyuma umeuwawa.
Hiki kilio tunalia wengi sio wewe pekee.
 
Kuhusu haya makosa ni kweli huwa yanatokea mengine sio makusudi ni bahati mbaya! Nimesoma sijaona kipengele nilichowahi kufanya kosa, hata kuscan ni kwa SIMU na niliitwa kwenye interview maeneo mengi na makubwa kama Taasisi za serikali na taasisi binafsi n.k means waliona ziko vizuri.

Sijawahi kutumia computer kuscan, kitendo cha kuitwa interview maana ake wameona documents zote na wameridhika labda bahati ni kukosa kazi.

Kujuana sana siku hizi, hata kama umekosea ukiwa mlengwa utaitwa tu.

Unataka mtu mmoja, utaitaje watu 40???

 
Asante kwa somo. Ingawa haya yote nimeyazingatia sana na ni mwaka wa 6 sasa hivi hakuna matumaini ya kupata ajira.
Mkuu hawa wenye kazi kila siku wanatafuta na kuja na udhaifu wa kuwaambia jobless ili tu ionekane jobless ni wazembe wakati hata wao cv zao ukiziona hazina maajabu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom