Binafsi ninasikitishwa sana na jinsi mambo yanavyoendelea katika Bunge Maalumu la Katibu (BMK) huko Dodoma. Kwa wale mnaofuatilia mwenendo wa Bunge hilo mtakubaliana nami kuwa haitapakikana Katiba iliyotokana na mawazo ya wananchi. Huwa ninaumia sana ninaposikia kuwa mawazo ya wananchi yanasiginwa na badala yake wajumbe wanaweka mawazo yao.
Kwa mfano Rasimu ya Katiba mpya imependekeza kuwa mawaziri wote wasitokane na wabunge kwa lengo la kuwaacha wabunge kuwajibika vizuri zaidi kwa wapiga kura wao. Lakini kutokana na ubinafsi wa wajumbe waliopo Bungeni wamekataa wazo hilo na kutaka mawaziri waendelee kuteuliwa miongoni mwa wabunge. Pia Rasimu ilipendekeza kuwa katiba iwape mamlaka wananchi ya kumuondoa mbunge wao kwa kukosa kuwajibika au kushindwa kuwatumikia wananchi ipasavyo. Nalo hili limekataliwa na wabunge wa BMK waliopo Dodoma kwa sababu ambazo hazina mashiko kabisa.
Si hivyo tu Rasimu ya katiba pia ilipendekeza kuwe na ukomo wa mtu kuwa mbunge tofauti na ilivyo hivi sasa ambapo kuna watu wamo bungeni kama vile katika majimbo hayo hakuna watu wenye uwezo wa kuwatumikia wananchi zaidi yao. Pendekezo hili pia limepingwa vikali na wajumbe wa BMK waliopo Dodoma. Sasa kama mawazo ya msingi ya wananchi yanaondolewa katika Rasimu ya Katiba mpya kulikuwa na sababu gani ya kupoteza fedha za wananchi kukusanya maoni? Hayo maoni yalikuwa ya nini na kwa faida ya nani?
Kwa mfano Rasimu ya Katiba mpya imependekeza kuwa mawaziri wote wasitokane na wabunge kwa lengo la kuwaacha wabunge kuwajibika vizuri zaidi kwa wapiga kura wao. Lakini kutokana na ubinafsi wa wajumbe waliopo Bungeni wamekataa wazo hilo na kutaka mawaziri waendelee kuteuliwa miongoni mwa wabunge. Pia Rasimu ilipendekeza kuwa katiba iwape mamlaka wananchi ya kumuondoa mbunge wao kwa kukosa kuwajibika au kushindwa kuwatumikia wananchi ipasavyo. Nalo hili limekataliwa na wabunge wa BMK waliopo Dodoma kwa sababu ambazo hazina mashiko kabisa.
Si hivyo tu Rasimu ya katiba pia ilipendekeza kuwe na ukomo wa mtu kuwa mbunge tofauti na ilivyo hivi sasa ambapo kuna watu wamo bungeni kama vile katika majimbo hayo hakuna watu wenye uwezo wa kuwatumikia wananchi zaidi yao. Pendekezo hili pia limepingwa vikali na wajumbe wa BMK waliopo Dodoma. Sasa kama mawazo ya msingi ya wananchi yanaondolewa katika Rasimu ya Katiba mpya kulikuwa na sababu gani ya kupoteza fedha za wananchi kukusanya maoni? Hayo maoni yalikuwa ya nini na kwa faida ya nani?