Rubi
JF-Expert Member
- Oct 5, 2009
- 1,615
- 326
MWANAMKE Hadija Nzali [30] mkazi wa Kimara King'ong'o anashikiliwa na jeshi la polisi kwa kudaiwa kufanya ukatili kumuingiza mtoto wa mume wake mwiko sehemu za siri na kumchoma moto sehemu zake za mwili
Jeshi la polisi nchini limesema linamshikilia mama huyo kwa ajili ya kufanya uchunguzi wa kina dhidi ya kitendo hicho cha ukatili dhidi ya mtoto huyo.
Awali ilidaiwa na baadhi ya majirani wanaoishi karibu na familia hiyo kuwa, wao walikuwa wakimuona mtoto huyo na makovu lakini kila walipokuwa wakijaribu kumhoji kwanini anakuwa hivyo aligoma kuelezea kwa kumuogopa mama huyo ambaye alimwambia akisema kwa watu anamuua kabisa.
Wamesema kuwa, mwanamke huyo alikuwa akidiriki hata kumnyima chakula mtoto huyo ambapo afya yake ilikuwa ikizidi kudorora siku hadi siku zinavyoenda.
Amesema kuwa mateso ya mtoto huyo walianza kuyasikia kupitia kwa watoto wenzake ambao alikuwa akicheza nao na binti huyo kuugulia maumivu makali aliyokuwa akiyapata kutokana na majeraha ya kipigo kutoka kwa mwanamke huyo.
Imedaiwa kuwa mtoto huyo alikuwa akielezea kuwa mama yake huyo amekuwa akiweka kijiko kwenye moto kisha kuanza kumbandika nacho mwilini mwake huku akimuingiza mwiko sehemu za siri.
Binti huyo (jina limehifadhiwa), aliliambia jeshi la polisi kuwa alikuwa akipata mateso makali kutoka kwa mama huyo hali ambayo ilimsababishia kukaa ndani muda mwingi bila ya baba yake mzazi kujua na aliogopa kumwambia baba yake kwa kuwa alikuwa hamuamini.
Amesema kuwa majirani zetu walipoona hali yangu inazidi kudidimia na huku mwendo wangu ukibadilika na kukosa furaha kila kukicha ndipo waliponihoji na walipogundua mateso hayo na kwenda kutoa taarifa kituo cha polisi ili niweze kusaidiwa .
Hata hivyo mwanamke huyo alipohojiwa kuhusiana na tukio hilo alikana kuhusika ingawa mtoto huyo amekuwa na alama za majeraha mwilini mwake.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Mark Kalunguyeye amesema kuwa, Jeshi lake linaendelea kumshikilia mwanamke huyo na atafikishwa Mahakamani baada ya upelelezi kukamilika.
Binti huyo anapatiwa matibabu katika hospitali ya Mwananyamala chini ya ulinzi wa jeshi la polisi.
source www.nifahamishe.com
Jeshi la polisi nchini limesema linamshikilia mama huyo kwa ajili ya kufanya uchunguzi wa kina dhidi ya kitendo hicho cha ukatili dhidi ya mtoto huyo.
Awali ilidaiwa na baadhi ya majirani wanaoishi karibu na familia hiyo kuwa, wao walikuwa wakimuona mtoto huyo na makovu lakini kila walipokuwa wakijaribu kumhoji kwanini anakuwa hivyo aligoma kuelezea kwa kumuogopa mama huyo ambaye alimwambia akisema kwa watu anamuua kabisa.
Wamesema kuwa, mwanamke huyo alikuwa akidiriki hata kumnyima chakula mtoto huyo ambapo afya yake ilikuwa ikizidi kudorora siku hadi siku zinavyoenda.
Amesema kuwa mateso ya mtoto huyo walianza kuyasikia kupitia kwa watoto wenzake ambao alikuwa akicheza nao na binti huyo kuugulia maumivu makali aliyokuwa akiyapata kutokana na majeraha ya kipigo kutoka kwa mwanamke huyo.
Imedaiwa kuwa mtoto huyo alikuwa akielezea kuwa mama yake huyo amekuwa akiweka kijiko kwenye moto kisha kuanza kumbandika nacho mwilini mwake huku akimuingiza mwiko sehemu za siri.
Binti huyo (jina limehifadhiwa), aliliambia jeshi la polisi kuwa alikuwa akipata mateso makali kutoka kwa mama huyo hali ambayo ilimsababishia kukaa ndani muda mwingi bila ya baba yake mzazi kujua na aliogopa kumwambia baba yake kwa kuwa alikuwa hamuamini.
Amesema kuwa majirani zetu walipoona hali yangu inazidi kudidimia na huku mwendo wangu ukibadilika na kukosa furaha kila kukicha ndipo waliponihoji na walipogundua mateso hayo na kwenda kutoa taarifa kituo cha polisi ili niweze kusaidiwa .
Hata hivyo mwanamke huyo alipohojiwa kuhusiana na tukio hilo alikana kuhusika ingawa mtoto huyo amekuwa na alama za majeraha mwilini mwake.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Mark Kalunguyeye amesema kuwa, Jeshi lake linaendelea kumshikilia mwanamke huyo na atafikishwa Mahakamani baada ya upelelezi kukamilika.
Binti huyo anapatiwa matibabu katika hospitali ya Mwananyamala chini ya ulinzi wa jeshi la polisi.
source www.nifahamishe.com