Mtumishi Wetu
JF-Expert Member
- Oct 12, 2010
- 5,712
- 1,907
Mkuu UWEZO TUNAO anahamisha mada nini, unajaribu kuzima huu moto, mbona ungeanzisha thread ya hii habari ingekuwa poa tuu??????JF NA UKOSOAJI MCHUNGU ULIOTUKUKA: RAIS KIKWETE SASA APATA DIRA MPYA KUTUPUNGUZIA MZIGO WA SAFARI ZA NJE WALIPAKODI WA TANZANIA KUFUATIA MICHARAZO BILA HURUMA YA MTANDAO HUU
MhRais Kkikwete,
Nakushukuru sana katika hili la kusoma sehemu ya ukosoaji wetu hapa JF na hatimaye kuona mantiki ya kupunguza idadi ya watu unaosafiri nao kwenda nchi za nje.
Hadi hapa naomba naye mama yetu, Mchungaji Mama Lwakatare, aliyekaririwa majuzi kutamani kuona mtandao wetu huu wa JF ikifungwa atambue kwamba hata na sisi huku TUNAFAIDI KWA WATANZANIA tena kuliko hata uwakilishi wao bungeni huku sisi tukiwa hatulipwi mshahara na mtu yeyote wala hizo posho wanazozigombania hivi sasa huko mjengoni Domz.
Nasema mama yetu huyu naye sasa aone jinsi gani Rais Kikwete anavyotumia mtandao huu wa JF kurekebisha mambo hata kule ndani mwake Magogoni.
Ni majuzi tu hapa tumemtifua kweli kweli RaisKikwete juu ya safari zake nje ya nchi na tukahoji tupewe mchanganuo wa faida na tija tulizozipata kutokana na safari zake hizo tangu aingie madarakani ikilinganishwa na thamani ya gharama tulizozitumia kama walipa kodi kufadhili safari hizo.
Isitoshe, tulikwenda mbali kidogo kwa kutahadharisha ya kwamba walipakodi wa nchi hii tusije tukajikuta tukifika mahali sawa na KUUZA ZIZI ZIMA LA NG'OMBE WETU WA PEKEE KUTUMIKA KUFADHILI SAFARI ZA RAIS NA JOPO LAKE KUBWA AMBALO MWISHO WA SIKU TUNAJIKUTA IKITULETEA FAIDA YENYE THAMANI YA YAI LA KUKU. This was a very candid and bitter criticism on President Kikwete BUT with a bottomline of AGGITATING FOR A CHANGE FOR THE BETTER.
Hadi hapa nimefarijika kugundua kwamba kumbe Mkulu hata ulivyo huko Davos kumbe bado uliweza kujipatia japo kijinafasi (kama mwana JF mwenzetu Prof Mwandosia alipokua matibabuni India) walau kuchungulia humu na kukutana na jinsi nilivyokukosoa kwa HASIRA ZOTE na wala haujachukulia chuki badala yake umeamua kuchukua hatua kurekebisha mambo.
Kimsingi Rais wetu, kama ulikua hujui, ujue leo kwamba hatufurahishwi hata chembe na uvujishaji wa kodi zetu bila kutuletea tija ya kuonekana. Madaktari wanatiji kubwa kwetu; kawaboreshee malipo yao, wabunge hasa wa CCM ni mzigo kwetu kwa tabia yao ya kugeuka muhuri wako kupitisha kila uchafu serikalini; kawapokonye posho zote, rekebisha mfumo wa mishahara na marupurupu kitaifa kuleta uwiano na kulinda morali ya watumishi wetu wa serikali
Jamii isiokua na kundi lenye kujenga mawazo tofauti yenye kukosoa kwa nia ya kujinga ni sawa na jamii iliokufa. Mimi ni mwananchi wako mkereka na mambo mengi ya hovyo pamoja na ufisadi serikalini na mkosoaji wako mwaminifui nisiyekuonea haya hata kidogo katia jambo lolote lile lenye kubeba MASLAHI MAPANA YA UMMA.
Hivyo, katika hatua yako hii ya kuwazia kutupunguzia mzigo wa safri za nje, nasema asante kwa kupokea ukosoaji wangu mchungu sana na kuligeuza kuwa ni sehemu ya ratiba yako kuturekebishia mambo.
Endelea kutarajia mashambulizi zaidi kwako na kwa serikali yako toka kwangu endapo kuna mahala mambo wala si mambo, na ninakutakia safari njema nyumbani uje ukamalize ubishi wa posho za wabunge kwa kuendana na matarajio ya umma na ukawalipe zaidi madaktari wetu.
Mwananchi Wako,
UWEZO TUNAO