Mnhenwa Ndege
JF-Expert Member
- Dec 5, 2007
- 242
- 19
Jamani kuanzi tarehe moja mwezi ujao, mtu yeyote yule ambaye atataka kumlipa mwenzake kiasi cha fedha cha zaidi ya milioni kumi (10,000,000) kwa kutumia cheki ya benki moja ili mlipwaji a-depositi benki nyengine (benki yake), haitawezekana tena.
Mfano mwengine ni huu; Yani kama unamdai mtu hela kiasi cha zaidi ya milioni kumi (10,000,000) kisha huyo mtu akulipe kwa kutumia cheki basi wewe kataa maana ukiipeleka hiyo cheki katika benki yako itakataliwa. Lakini kama cheki ni chini ya milioni kumi haina tatizo.
Hii ina maana kuwa Clearing House ya Benki Kuu ya Tanzania haikubali malipo binasfi ya cheki zinazo zidi milioni kumi. Badala yake kama unataka kumlipa mtu hela zaidi ya milioni kumi basi njia ni hizi zifuatayo;
1. Mdumbukizie pesa kwenye akaunti yake kwa kuenda wewe binafsi au mwakilishi wako katika benki yake.
2. Nenda katika benki yako kisha uiagize benki yako itume hela kwa mfumo wa TISS (Tanzania Interbank Settlement System)
3. Mlipe taslimu (cash).
UFAFANUZI
1. Kama mtu amekupa cheki ya benki ambayo wewe pia una akaunti kwa jina hilo hilo lililoandikwa kwenye Cheki basi haina noma hataka kama imezidi milioni kumi italipwa tu ilimradi mlipaji awe na hela za kutosha kwenye akaunti husika.
2. Malipo yote ya Cheki ya chini ya milioni kumi hatakuwa kama kawaida.
3. Special Clearance ya zaidi ya milioni kumi itakuwa hakuna tena.
4. Malipo yote ya Cheki za Serikali yatakuwa kama kawaida.
Ikumbukwe kuwa ni malipo yale tu yanayohusisha benki mbili yani (bank to bank payments) ndio tunayoyaongelea.
SOURCE: Pwani Raha
Mfano mwengine ni huu; Yani kama unamdai mtu hela kiasi cha zaidi ya milioni kumi (10,000,000) kisha huyo mtu akulipe kwa kutumia cheki basi wewe kataa maana ukiipeleka hiyo cheki katika benki yako itakataliwa. Lakini kama cheki ni chini ya milioni kumi haina tatizo.
Hii ina maana kuwa Clearing House ya Benki Kuu ya Tanzania haikubali malipo binasfi ya cheki zinazo zidi milioni kumi. Badala yake kama unataka kumlipa mtu hela zaidi ya milioni kumi basi njia ni hizi zifuatayo;
1. Mdumbukizie pesa kwenye akaunti yake kwa kuenda wewe binafsi au mwakilishi wako katika benki yake.
2. Nenda katika benki yako kisha uiagize benki yako itume hela kwa mfumo wa TISS (Tanzania Interbank Settlement System)
3. Mlipe taslimu (cash).
UFAFANUZI
1. Kama mtu amekupa cheki ya benki ambayo wewe pia una akaunti kwa jina hilo hilo lililoandikwa kwenye Cheki basi haina noma hataka kama imezidi milioni kumi italipwa tu ilimradi mlipaji awe na hela za kutosha kwenye akaunti husika.
2. Malipo yote ya Cheki ya chini ya milioni kumi hatakuwa kama kawaida.
3. Special Clearance ya zaidi ya milioni kumi itakuwa hakuna tena.
4. Malipo yote ya Cheki za Serikali yatakuwa kama kawaida.
Ikumbukwe kuwa ni malipo yale tu yanayohusisha benki mbili yani (bank to bank payments) ndio tunayoyaongelea.
SOURCE: Pwani Raha
Last edited: