BabuK
JF-Expert Member
- Jul 30, 2008
- 1,845
- 329
ZAIDI ya makontena 101, yalikamatwa hadi kufikia mwaka jana yakiwa na bidhaa bandia na bidhaa hizo kuharibiwa huku wahusika wakifikishwa mahakamani.
Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Lazaro Nyalandu, ameliambia Bunge mjini hapa kuwa kukamatwa kwa bidhaa hizo bandia ni mojawapo ya mikakati inayochukuliwa na
Serikali katika kukabiliana na uingizaji wa bidhaa bandia.
Alisema Tanzania ni mojawapo ya nchi zinazoathirika na uingizaji wa bidhaa bandia kutokana na utaalamu unaotumika kumpotosha mlaji juu ya uhalisia wa bidhaa kuwa ni wa hali ya juu hivyo ni vigumu kubaini mara moja udanganyifu huo.
Alisema ili kukabiliana na uingizaji wa bidhaa bandia nchini, Wizara ya Viwanda na Biashara
kupitia Tume ya Ushindani imechukua hatua mbalimbali ikiwemo ya kuimarisha idara ya kupambana na bidhaa bandia katika bandari zote nchini na kutoa elimu kwa waagizaji wa bidhaa.
Nyalandu alisema hatua nyingine ni kushirikiana na wamiliki wa nembo na alama za bidhaa (Brand Owners) ili kupata taarifa za uingizaji wa bidhaa kutoka nje.
Alisema mkakati mwingine ni kuimarisha utoaji wa elimu kwa umma juu ya namna ya kutambua bidhaa bandia na kuimarisha ushirikiano na wadau mbalimbali ndani na nje ya nchi ili kudhibiti uingizaji wake.
Naibu Waziri alisema mwenye kumiliki Nembo au Alama ya Bidhaa, ndiye mwenye nafasi kubwa ya kutambua udanganyifu uliofanyika katika bidhaa kuliko mtu mwingine.
Alikuwa akijibu swali la Mbunge wa Chambani, Salim Hemed Hamis (CUF), aliyeuliza je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza udhibiti wa uingizaji wa bidhaa bandia nchini?
cChanzo: Habarileo
Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Lazaro Nyalandu, ameliambia Bunge mjini hapa kuwa kukamatwa kwa bidhaa hizo bandia ni mojawapo ya mikakati inayochukuliwa na
Serikali katika kukabiliana na uingizaji wa bidhaa bandia.
Alisema Tanzania ni mojawapo ya nchi zinazoathirika na uingizaji wa bidhaa bandia kutokana na utaalamu unaotumika kumpotosha mlaji juu ya uhalisia wa bidhaa kuwa ni wa hali ya juu hivyo ni vigumu kubaini mara moja udanganyifu huo.
Alisema ili kukabiliana na uingizaji wa bidhaa bandia nchini, Wizara ya Viwanda na Biashara
kupitia Tume ya Ushindani imechukua hatua mbalimbali ikiwemo ya kuimarisha idara ya kupambana na bidhaa bandia katika bandari zote nchini na kutoa elimu kwa waagizaji wa bidhaa.
Nyalandu alisema hatua nyingine ni kushirikiana na wamiliki wa nembo na alama za bidhaa (Brand Owners) ili kupata taarifa za uingizaji wa bidhaa kutoka nje.
Alisema mkakati mwingine ni kuimarisha utoaji wa elimu kwa umma juu ya namna ya kutambua bidhaa bandia na kuimarisha ushirikiano na wadau mbalimbali ndani na nje ya nchi ili kudhibiti uingizaji wake.
Naibu Waziri alisema mwenye kumiliki Nembo au Alama ya Bidhaa, ndiye mwenye nafasi kubwa ya kutambua udanganyifu uliofanyika katika bidhaa kuliko mtu mwingine.
Alikuwa akijibu swali la Mbunge wa Chambani, Salim Hemed Hamis (CUF), aliyeuliza je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza udhibiti wa uingizaji wa bidhaa bandia nchini?
cChanzo: Habarileo