jimama26
JF-Expert Member
- Jul 30, 2013
- 2,735
- 2,808
Haya ndiyo matokeo ya kujenga ghorofa kwa kutumia nondo chakavu, kasi ya ghorofa kuporomoka imeongezeka.
Nondo chakavu sasa ni Mbowe au Lissu? Na ghorofa ni ofisi za Ufipa au?
Haya ndiyo matokeo ya kujenga ghorofa kwa kutumia nondo chakavu, kasi ya ghorofa kuporomoka imeongezeka.
Kwa taarifa yako tukio ni tukio tu, bila kujali linajadiliwa na nani. Ni mara ngapi yanatokeza matukio kwa wapinzani na wote tunajadili hayo hayo, au ccm huwa mnajadili tofauti na hayo? Cha muhimu ni kuangalia unajadiliwa katika mlengo upi. Kama zaidi ya 70% ni negativity kuhusu nafasi yako, hapo unafaidika na Nini?Wote tunajadili haya haya, na ndio hoja yangu kuwa haya yanawatoa watu kwenye hoja za msingi, na matukio hayataisha ila wapinzani kuwa spika ya matukio ya ccm ni mbaya zaidi.
Chalamila kapoa, tangu akalie kiti hajawahi hata kututisha kuwa atatuchapa vibokoHuyo pimbi Ofisi yake iko Dodoma na kama kuwatisha awatishe maccm wenzake huko mikoani, mwenye jiji ni Chalamila.
Hivi kwanini rais anapenda kujuzungushia watu wenye tuhuma na sifa mbaya katika jamii? Kuna waziri mmoja mpendwa wake anajulikana kwa wizi na ufisadi wa kutisha bado anamuacha kwenye wizara nyeti, na sasa kamfufua huyu mwenye tuhuma nzito za mauaji ya watu wasio na hatia, utekaji na utesajiKatibu mwenezi wa CCM ndugu Paul Makonda amesema amemuona Mbowe akiwa Songwe Lakini hana helicopter kama tulivyomzoea
Hivyo Makonda ameviagiza Mamlaka za Serikali zinazohusika na Utoaji wa vibali vya anga wampe Mwenyekiti wa Chadema mh Mbowe Kibali na kama hana mafuta aseme kwani ameongea na Rais Samia waweze kumsaidia
Chanzo: EATV
Helcopter ya msaada
Mafuta ya msaada
Za kuambiwa changanya na zako
CCM wanajua njia nzuri wa kuwatoa wapinzani kwenye hoja ni kuwapa vichwa vya habari, na uteuzi wa Makonda unakwenda kufanikisha hilo vizuri.
Na mfano mzuri ni jinsi ambavyo sasa hivi tunacheza ngoma yao.
Wanachama wengi wa chadema ndio wanaripoti tukio la leo la Makonda, na alikuwa sahihi kusema vyama vya upinzani ni maReporter.
Upinzani wakitaka waondoke kwenye huu mtego, waache kuwa spika ya kujadili matukio ya CCM.
Mzee wa Farasi enzi za Twanga Pepeta 😂😂Hongera kwake naona kapewa na vxr
Mupya....aendele pigwa kiyoyozi
Kaenda na boda kaondoka na vxr
Siasa bana
Ova
Mimi naanza kuona tabu kidogo. Huyu msemaji wa CCM anapotoa amri kwa Serikali anaongea kwa madaraka yapi? Kwenye hotuba yake inaonyesha kama majukumu yake hajayajua. Kimsingi yeye siyo muwajibishaji. Kazi yake kubwa ni kutetea ilani na kututangazia maamuzi ya vikao mbalimbali. Na kusambaza aliyotumwa na wakubwa zake. Sana sana, kwa upande wa mawaziri, anachoweza ni kuwachongea kwa wakubwa au ndani ya chama. Lakini si kuwawajibisha kwa hali yoyote ile. Kwa hotuba yake ya leo, yaonekana hata kazi yake hajaijua.Katibu mwenezi wa CCM ndugu Paul Makonda amesema amemuona Mbowe akiwa Songwe Lakini hana helicopter kama tulivyomzoea
Hivyo Makonda ameviagiza Mamlaka za Serikali zinazohusika na Utoaji wa vibali vya anga wampe Mwenyekiti wa Chadema mh Mbowe Kibali na kama hana mafuta aseme kwani ameongea na Rais Samia waweze kumsaidia
Chanzo: EATV
Ulifeli shule, hapa tunamzungumzia bebi wako Manenepo.Nondo chakavu sasa ni Mbowe au Lissu? Na ghorofa ni ofisi za Ufipa au?
Ndiyo hayo watamwambia Mwenyekiti apakie madumu ya mafuta aruke nayo kama walivyofanya wengine mwaka 2015Nadhani mafuta ndio ya msaada.