Uloi nga Machi
Member
- Jan 4, 2012
- 61
- 23
MAKOMBO
Ama kwa mlaji kweli,ambaye hapuuzii,
Asiye na mushkeli,kula afanya bidii,
Mle hujiweka mbali, kukera sidhamirii,
Nakula siyawachii,niyakutapo makombo.
Dk. Kassim Pazi Haumotile,
MWANANCHI, Septemba 27,2013
MAKOMBO(SAPOTI)
Makombo yana utamu,nikutapo sizembei,
Halani hutia timu,nafasi siichezei,
Siwezi kulaza damu, na yalipo sipotei!
Nakula siyaachii, niyakutapo makombo.
Niyakutapo makombo,mbali nayo sisogei,
Nakula nijaze tumbo,ni bure hayana bei,
Hujifunga kwa masombo,uvivu siyatendei!
Nakula siyaachii, niyakutapo makombo.
Ninapoamua kula,hapo mimi silegei,
Hujihifadhi mahala,nilengapo sikosei,
Maini au salala,kwangu yote ni "Okei!"
Nakula siyaachii, niyakutapo makombo.
Yanabana matumizi,pesa haziteketei,
Makombo siyabakizi,nipewapo simezei,
Walao "kilezilezi",kuliwa siwatetei!
Nakula siyaachii, niyakutapo makombo.
Makini wajiliao, naapa siwaendei,
Na wale kwa raha zao,macho siwakodolei,
Ila kwa wachezeao,huruma siwaonei!
Nakula siyaachii, niyakutapo makombo.
Kaditamati makombo,kuacha sitegemei,
Si kwamba nina msimbo, "kichwani hazienei",
Ndani yake kuna jambo,leo siwaelezei!
Nakula siyaachii, niyakutapo makombo.
Lambert F.Chialo( Mhadhiri wa malenga)
Magogoni, Dar es Salaam,
0713961860
Ama kwa mlaji kweli,ambaye hapuuzii,
Asiye na mushkeli,kula afanya bidii,
Mle hujiweka mbali, kukera sidhamirii,
Nakula siyawachii,niyakutapo makombo.
Dk. Kassim Pazi Haumotile,
MWANANCHI, Septemba 27,2013
MAKOMBO(SAPOTI)
Makombo yana utamu,nikutapo sizembei,
Halani hutia timu,nafasi siichezei,
Siwezi kulaza damu, na yalipo sipotei!
Nakula siyaachii, niyakutapo makombo.
Niyakutapo makombo,mbali nayo sisogei,
Nakula nijaze tumbo,ni bure hayana bei,
Hujifunga kwa masombo,uvivu siyatendei!
Nakula siyaachii, niyakutapo makombo.
Ninapoamua kula,hapo mimi silegei,
Hujihifadhi mahala,nilengapo sikosei,
Maini au salala,kwangu yote ni "Okei!"
Nakula siyaachii, niyakutapo makombo.
Yanabana matumizi,pesa haziteketei,
Makombo siyabakizi,nipewapo simezei,
Walao "kilezilezi",kuliwa siwatetei!
Nakula siyaachii, niyakutapo makombo.
Makini wajiliao, naapa siwaendei,
Na wale kwa raha zao,macho siwakodolei,
Ila kwa wachezeao,huruma siwaonei!
Nakula siyaachii, niyakutapo makombo.
Kaditamati makombo,kuacha sitegemei,
Si kwamba nina msimbo, "kichwani hazienei",
Ndani yake kuna jambo,leo siwaelezei!
Nakula siyaachii, niyakutapo makombo.
Lambert F.Chialo( Mhadhiri wa malenga)
Magogoni, Dar es Salaam,
0713961860