Mheshimiwa Makamba, uliwahi kufukuzwa kazi ukiwa kama mkuu wa wilaya, uliondolewa si kwa utendaji wako mbaya wa kazi bali wakuu wengi wa idara wilayani kwako walikuangusha. Ukiachilia mbali siasa umekuwa mchapa kazi mzuri sana. Katika kipindi cha uchaguzi kampeni za CCM zisilenge kwenye kutoa ahadi ambazo mantiki yoyote. Hii timu ya kampeni ya Raisi ina mapungufu makubwa sijui ni nani anayemshauri Raisi, inawezekana kabisa mtu huyo hana malengo mazuri na CCM na Raisi mwenyewe vitu kama ahadi za bajaj zinatokea wapi? Alichotakiwa Raisi ni kuboresha huduma za afya vijijini, kuwapatia maji safi na kuongeza huduma za kijamii kama lengo lilikuwa ni kuwasaidia wajawazito basi Raisi alipaswa kuahidi kuongeza vituo vya afya na watendaji wake, bajaji hazitatua matatizo ya wajawazito, kinga ni rahisi kuliko tiba. Hii ahadi ya meli na uwanja wa ndege Kigoma nayo mh. Makamba ni kweli tunalitaka jimbo la Zito lakini ahadi kama hizi zitatuweka pabaya 2015; si vibaya kuahidi kuboresha usafiri Kigoma lakini ahadi zimekuwa nyingi na hazitekelezeki, cha msingi washauri wa Raisi katika kampeni wanaonyesha upeo mdogo sana wa kuchanganua mambo kumbuka ahadi hazitatui matatizo kinachotakiwa ni utekelezaji sera za chama. Panga safu upya ! mambo kimbelembele