Makamba: Baada ya Matengenezo, Kukatika Umeme Itakuwa Historia.

Bams

JF-Expert Member
Oct 19, 2010
16,555
41,066
Watanzania yaelekea vichwa vyetu ni vizito sana kuelewa!!

Wakati January Makamba akiwa Waziri wa Nishati, aliwahi kunena kuwa kukatika kwa umeme kulikuwa kumesababishwa na mitambo ya TANESCO kutofanyiwa matengenezo wakati wa utawala wa Hayati Magufuli. Akaongeza kuwa baada ya matengenezo, kukatika kwa umeme itakuwa historia.

Sasa, naamini huenda sikumwelewa Makamba. Nilidhani Makamba alikuwa akimaanisha kuwa kukatika kwa umeme kutaisha na watu watabakia kukumbuka tu kuwa hapo awali umeme ulikuwa ukikatika. Ninyi wengine mlielewi nini?

Lakini kwa yanayoendelea sasa, nashawishika kuamini kuwa Makamba alikuwa akimaanisha kuwa baada ya kukamilika zoezi walilokuwa wakilifanya, kukatika kwa umeme kutakuwa ni kwa kiwango cha historia, yaani umeme utakatika kwa kiwango ambacho hakijawahi kutokea. Na naona baada ya kulikamilisha zoezi la kukatika umeme kwenye kiwango cha historia, Rais aliridhika kuwa kazi ameikamilisha vizuri, akazawadiwa wizara ya kimataifa.

Sasa Rais amesema kuwa mwisho wa kukatika umeme ni mwezi March 2024. Hofu yangu ni kuwa isije kuwa nimemwelewa vibaya tena. Isije ikawa baada ya mwezi wa tatu, ikawa mwisho wa umeme kukatika kwa sababu uemme hautakuwepo kabisa. Maana kadiri tunavyoisogelea March 2024, hali ya umeme inazidi kuwa mbaya zaidi.
 
Hii nchi ina ujinga mwingi.

Amini msiamini hii nchi inahitaki series ya viongozi madikteta watakaokuwa na uchungu wa Taifa hili kuliko huruma kwa wajinga wajinga.

Kuna mahala tunalazimisha nchi iongozwe na sheria pamoja na kuwa na katiba nzuri, tunasahau tunaotaka watupe hizo sheria na Katiba nzuri ndio haohao wananufaika na sheria zilizopo na hata wakikubali kutupa hizo katiba na sheria nzuri bado wao ndio watakuwa viongozi maana wao ndio wasimamizi na watekelezaji wa hizo sheria na katiba.

Walianza watu kwanza wenye maono mazuri ndio zikaja sheria na Katiba bora, hivyo vitu hupatikana kutoka kwa viongozi wenye nia na uzalendo wa dhati juu ya nchi zao, na viongozi hao ndio huweza kufagia kila aina ya takataka kwenye uongozi na kutengeneza mifumo imara yenye maslahi kwa Taifa.

Kwasasa Taifa hili linahitaji kiongozi imara mwenye maono na udikteta wa hali ya juu kuja kubadili mifumo na kutengeneza katiba bora na kuweka sheria zitakazoongoza hii nchi ikiwa pamoja na yeye mwenyewe kuwasimamia watu kwa mkono wa chuma kuzifuata hizo sheria, kuziishi na vizazi vijengwe vikijua kuna sheria na katiba zinazoongoza hii nchi lazima uvifuate na kuviishi na ukienda kinyume lazima zikuadhibu..
 
Hata kama tuna tatizo la uchakavu wa mitambo linalosababisha kukatika kwa umeme, kwanini Tanesco last time walituambia sababu ya kukatika umeme ni upungufu wa maji kwenye vyanzo vya kuzalisha umeme, mpaka zile mvua zilipokuja kuwaumbua?

Tatizo letu tunaongozwa na waongo kwa uongo, wanatuzubaisha tu, dawa yao akiwepo kiongozi mwenye msimamo asiyejali wala kumuogopa yeyote, hapo ndipo tutajua hasa chanzo cha hii migao isiyo na maana, kwa saa naamini hii migao chanzo chake ni ujanja ujanja tu wa viongozi na wafanyabiashara.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 
Hii nchi ina ujinga mwingi.

Amini msiamini hii nchi inahitaki series ya viongozi madikteta watakaokuwa na uchungu wa Taifa hili kuliko huruma kwa wajinga wajinga.

Kuna mahala tunalazimisha nchi iongozwe na sheria pamoja na kuwa na katiba nzuri, tunasahau tunaotaka watupe hizo sheria na Katiba nzuri ndio haohao wananufaika na sheria zilizopo na hata wakikubali kutupa hizo katiba na sheria nzuri bado wao ndio watakuwa viongozi maana wao ndio wasimamizi na watekelezaji wa hizo sheria na katiba.

Walianza watu kwanza wenye maono mazuri ndio zikaja sheria na Katiba bora, hivyo vitu hupatikana kutoka kwa viongozi wenye nia na uzalendo wa dhati juu ya nchi zao, na viongozi hao ndio huweza kufagia kila aina ya takataka kwenye uongozi na kutengeneza mifumo imara yenye maslahi kwa Taifa.

Kwasasa Taifa hili linahitaji kiongozi imara mwenye maono na udikteta wa hali ya juu kuja kubadili mifumo na kutengeneza katiba bora na kuweka sheria zitakazoongoza hii nchi ikiwa pamoja na yeye mwenyewe kuwasimamia watu kwa mkono wa chuma kuzifuata hizo sheria, kuziishi na vizazi vijengwe vikijua kuna sheria na katiba zinazoongoza hii nchi lazima uvifuate na kuviishi na ukienda kinyume lazima zikuadhibu..
Kwani si mlikuwa na JPM ?
 
Hata kama tuna tatizo la uchakavu wa mitambo linalosababisha kukatika kwa umeme, kwanini Tanesco last time walituambia sababu ya kukatika umeme ni upungufu wa maji kwenye vyanzo vya kuzalisha umeme, mpaka zile mvua zilipokuja kuwaumbua?

Tatizo letu tunaongozwa na waongo kwa uongo, wanatuzubaisha tu, dawa yao akiwepo kiongozi mwenye msimamo asiyejali wala kumuogopa yeyote, hapo ndipo tutajua hasa chanzo cha hii migao isiyo na maana, kwa saa naamini hii migao chanzo chake ni ujanja ujanja tu wa viongozi na wafanyabiashara.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
Kuna afisa mmoja mkubwa wa TANESCO, siku moja wakati watu wanalalamimia kukosekana kwa umeme, yeye akasema kuwa umeme utapatikana siku yoyote viongozi wakitaka upatikane. Baada ya kumdadisi, akasema mgao ni kwaajili ya kuitafutoa CCM pesa za kampeni, na kwamba kuna waingizaji wakubwa wa generators kubwa za umeme ambao wapo tayari kuigawia faida yote CCM. Majenerator hayo ni yale makubwa yanayotumika viwandani. Bado natafakari maneno yale. Na kama ni kweli, basi nchi hii kuna watu wanamzidi hata shetani kwa uovu.
 
Bado tu hujazoea uongo wa Ccm na viongozi wake ?
Tunajua kuwa viongpzi wa Setikali na CCM ni waongo sana, lakini kuna wakati unajipa imani kuwa huenda wamebadilika. Baadaye unakuja kujiona mjinga kwa kuwaamini viongozi wa chama ambacho wakati wote kina historia ya uwongo na ulaghai.
 
Kuna afisa mmoja mkubwa wa TANESCO, siku moja wakati watu wanalalamimia kukosekana kwa umeme, yeye akasema kuwa umeme utapatikana siku yoyote viongozi wakitaka upatikane. Baada ya kumdadisi, akasema mgao ni kwaajili ya kuitafutoa CCM pesa za kampeni, na kwamba kuna waingizaji wakubwa wa generators kubwa za umeme ambao wapo tayari kuigawia faida yote CCM. Majenerator hayo ni yale makubwa yanayotumika viwandani. Bado natafakari maneno yale. Na kama ni kweli, basi nchi hii kuna watu wanamzidi hata shetani kwa uovu.
Hiyo sababu uliyopewa inaelekea kuwa kweli kabisa, nikikumbuka wakati wa Magufuli hapakuwepo na mgao mkali namna hii, licha ya mitambo na vyanzo vya kuzalishia umeme kuwa hivi vya sasa, ajabu ameingia huyu mama mpenda wafanyabiashara mambo yameanza kuharibika, umeme karibia miezi tisa haueleweki.

Wafanyabiashara ambao wanaweza kuwa ndio wanasiasa wanamuangalia mtawala, wakiona anaingilika basi wanamuingia, nae kwasababu ya uwezo mdogo wa kuhoji anawakubalia hoja zao, kama alivyofanya wakati ule akidai vita ya Urusi vs Ukraine ingepandisha bei ya bidhaa, hii mindset alipewa na wafanyabiashara akaiweka akilini mwake, hajui kuchanganya na zake.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 
Tunajua kuwa viongpzi wa Setikali na CCM ni waongo sana, lakini kuna wakati unajipa imani kuwa huenda wamebadilika. Baadaye unakuja kjlujiona mjinga kwa kuwaamini viongozi wa chama ambacho wakati wote kina historia ya uwongo na ulaghai.
Kwenye kuomba kura wanapiga mpaka na magoti unakuwa na imani tunawapa
Wakipata sasa cha moto tunakuona
 
Watanzania yaelekea vichwa vyetu ni vizito sana kuelewa!!

Wakati January Makamba akiwa Waziri wa Nishati, aliwahi kunena kuwa kukatika kwa umeme kulikuwa kumesababishwa na mitambo ya TANESCO kutofanyiwa matengenezo wakati wa utawala wa Hayati Magufuli. Akaongeza kuwa baada ya matengenezo, kukatika kwa umeme itakuwa historia.

Sasa, naamini huenda sikumwelewa Makamba. Nilidhani Makamba alikuwa akimaanisha kuwa kukatika kwa umeme kutaisha na watu watabakia kukumbuka tu kuwa hapo awali umeme ulikuwa ukikatika. Ninyi wengine mlielewi nini?

Lakini kwa yanayoendelea sasa, nashawishika kuamini kuwa Makamba alikuwa akimaanisha kuwa baada ya kukamilika zoezi walilokuwa wakilifanya, kukatika kwa umeme kutakuwa ni kwa kiwango cha historia, yaani umeme utakatika kwa kiwango ambacho hakijawahi kutokea. Na naona baada ya kulikamilisha zoezi la kukatika umeme kwenye kiwango cha historia, Rais aliridhika kuwa kazi ameikamilisha vizuri, akazawadiwa wizara ya kimataifa.

Sasa Rais amesema kuwa mwisho wa kukatika umeme ni mwezi March 2024. Hofu yangu ni kuwa isije kuwa nimemwelewa vibaya tena. Isije ikawa baada ya mwezi wa tatu, ikawa mwisho wa umeme kukatika kwa sababu uemme hautakuwepo kabisa. Maana kadiri tunavyoisogelea March 2024, hali ya umeme inazidi kuwa mbaya zaidi.

..Rais alitoa ultimatum ambayo inakwisha DEC 26, 2023.

..Naona umekuja kuhamisha goli kuwa Tanesco walipewa mpaka March 2024.
 
Watanzania yaelekea vichwa vyetu ni vizito sana kuelewa!!

Wakati January Makamba akiwa Waziri wa Nishati, aliwahi kunena kuwa kukatika kwa umeme kulikuwa kumesababishwa na mitambo ya TANESCO kutofanyiwa matengenezo wakati wa utawala wa Hayati Magufuli. Akaongeza kuwa baada ya matengenezo, kukatika kwa umeme itakuwa historia.

Sasa, naamini huenda sikumwelewa Makamba. Nilidhani Makamba alikuwa akimaanisha kuwa kukatika kwa umeme kutaisha na watu watabakia kukumbuka tu kuwa hapo awali umeme ulikuwa ukikatika. Ninyi wengine mlielewi nini?

Lakini kwa yanayoendelea sasa, nashawishika kuamini kuwa Makamba alikuwa akimaanisha kuwa baada ya kukamilika zoezi walilokuwa wakilifanya, kukatika kwa umeme kutakuwa ni kwa kiwango cha historia, yaani umeme utakatika kwa kiwango ambacho hakijawahi kutokea. Na naona baada ya kulikamilisha zoezi la kukatika umeme kwenye kiwango cha historia, Rais aliridhika kuwa kazi ameikamilisha vizuri, akazawadiwa wizara ya kimataifa.

Sasa Rais amesema kuwa mwisho wa kukatika umeme ni mwezi March 2024. Hofu yangu ni kuwa isije kuwa nimemwelewa vibaya tena. Isije ikawa baada ya mwezi wa tatu, ikawa mwisho wa umeme kukatika kwa sababu uemme hautakuwepo kabisa. Maana kadiri tunavyoisogelea March 2024, hali ya umeme inazidi kuwa mbaya zaidi.
Januari Makamba alipaswa kunyongwa na siyo kuhamishwa Wizara. Ila iko soku yake atakuja kujibu alikopeleka Matrilioni ya fedha aliyopewa na Samia kwa ajili ya ukarabati mara alipoingia wizara ya nishati mwaka 2021
 
Januari Makamba alipaswa kunyongwa na siyo kuhamishwa Wizara. Ila iko soku yake atakuja kujibu alikopeleka Matrilioni ya fedha aliyopewa na Samia kwa ajili ya ukarabati mara alipoingia wizara ya nishati mwaka 2021

..sio Januari peke yake.

..hata waliomtangulia ktk uwaziri wa Nishati toka mgao wa kwanza wakati wa Mzee Mwinyi,na tulipowaleta IPTL, wanastahili lawama sawa na Januari.

..serikali mbalimbali za Ccm ndizo zilizosababisha matatizo tuliyonayo Januari akiwa sehemu ya uzembe na ufisadi huo.
 
..Rais alitoa ultimatum ambayo inakwisha DEC 26, 2023.

..Naona umekuja kuhamisha goli kuwa Tanesco walipewa mpaka March 2024.
Yawezekana nimesahau. Kauli yake nadhani hakutaja mwezi wala tarehe, ila alisema anawapa miezi 6.
 
Yawezekana nimesahau. Kauli yake nadhani hakutaja mwezi wala tarehe, ila alisema anawapa miezi 6.

..ni kweli hakuutaka tarehe.

..lakini kwa kauli yake kadhia ya ukatikaji umeme inatakiwa kukoma Dec 26 2023.

..ahadi za kutatua kadhia ya umeme nadhani zitakuwa na ujanja-ujanja kama ahadi za kuanza kutumika kwa Sgr.
 
Enzi hizo ukikosoa chochote afanyacho Kipara unaitwa Sukuma Gang!😁.
 
Back
Top Bottom