Ng'wanza Madaso
JF-Expert Member
- Oct 21, 2008
- 2,268
- 333
Makamba atumia Biblia kuwalaani Chadema
Thursday, 06 January 2011
Mwandishi Wetu
KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Yusuph Makamba amekilaumu Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kwa kile alichoeleza kuwa kimekaidi amri ya mamlaka halali na kufanya maandamano yaliyoleta vurugu na maafa.
Akizungumza na gazeti hii jana, Makamba alisema kitendo kilichofanywa na Chadema ni cha kinyama na kinapaswa kulaaniwa na watu wote wanaoitakia mema nchi hii "Ukisoma Biblia katika kitabu cha Warumi Sura 13, imeandikwa " Itiini Mamlaka inayowazidi nguvu; hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu," alisena Makamba na kuaongeza: "Sasa mamlaka imesema msiandamane, ninyi mnaandamana.
Nasema hawakufanya vizuri. Sasa tumlaumu nani kama sio Chadema." Makamba alisema haoni sababu Chadema kuandamana kwa sababu ya suala la Umeya, kwani kama hilo ndio sababu, alipaswa kwenda mahamani kudai haki wanayoeleza kuwa imeporwa na CCM badala ya kufanya maandamano yenye madhara kama hayo.
"Kama hoja ni umeya, huwezi kudai unayoamini imeporwa kwa maandamano, haki inapatikana mahakamani.
Sasa Mimi (Makamba) nawapa pole walioathirika na maandamano hayo lakini pia nalilia mali za CCM zilizoharibiwa. Gari la katibu wangu wa Mkoa limevunja vioo na ofisi yetu imeharibiwa vibaya," alisema Makamba mwisho
Source: Mwananchi
Huyu mzee kalaaniwa watu wamepoteza maisha yeye anasikitikia mali zilizoharibika.Upuuzi tu.
Thursday, 06 January 2011
Mwandishi Wetu
KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Yusuph Makamba amekilaumu Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kwa kile alichoeleza kuwa kimekaidi amri ya mamlaka halali na kufanya maandamano yaliyoleta vurugu na maafa.
Akizungumza na gazeti hii jana, Makamba alisema kitendo kilichofanywa na Chadema ni cha kinyama na kinapaswa kulaaniwa na watu wote wanaoitakia mema nchi hii "Ukisoma Biblia katika kitabu cha Warumi Sura 13, imeandikwa " Itiini Mamlaka inayowazidi nguvu; hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu," alisena Makamba na kuaongeza: "Sasa mamlaka imesema msiandamane, ninyi mnaandamana.
Nasema hawakufanya vizuri. Sasa tumlaumu nani kama sio Chadema." Makamba alisema haoni sababu Chadema kuandamana kwa sababu ya suala la Umeya, kwani kama hilo ndio sababu, alipaswa kwenda mahamani kudai haki wanayoeleza kuwa imeporwa na CCM badala ya kufanya maandamano yenye madhara kama hayo.
"Kama hoja ni umeya, huwezi kudai unayoamini imeporwa kwa maandamano, haki inapatikana mahakamani.
Sasa Mimi (Makamba) nawapa pole walioathirika na maandamano hayo lakini pia nalilia mali za CCM zilizoharibiwa. Gari la katibu wangu wa Mkoa limevunja vioo na ofisi yetu imeharibiwa vibaya," alisema Makamba mwisho
Source: Mwananchi
Huyu mzee kalaaniwa watu wamepoteza maisha yeye anasikitikia mali zilizoharibika.Upuuzi tu.