Kashaijabutege
JF-Expert Member
- Oct 20, 2010
- 2,696
- 740
Ninachowaomba wana JF Wakristu ni kujitahidi katika mfungo huu unaoanza leo kuishi maisha yanayo mpendeza Mungu. Ingawa twapashwa kuishi maisha ya utauwa kila siku, udhaifu wetu hutuvuta kutenda yaliyo mabaya. Tumwombe Roho Mtakatifu, atujalie nguvu ya kupigana na maovu ili jamii inayotuzunguka ione uwepo wa Mungu kupitia kwetu.
La muhimu sio KUFUNGA KULA TU, bali ni kumrudia Mungu katika roho na kweli kwa kusali na kuomba, huku tukiutiisha mwili kwa roho. Tulio na ziada basi tuwasaidie maskini, na hiyo ndiyo funga sahihi.
Na hapa JF katika post zetu tusitukanane, na hasa tusikejeli au kudharau imani za wenzetu.
Nawatakia mfungo mwema.
La muhimu sio KUFUNGA KULA TU, bali ni kumrudia Mungu katika roho na kweli kwa kusali na kuomba, huku tukiutiisha mwili kwa roho. Tulio na ziada basi tuwasaidie maskini, na hiyo ndiyo funga sahihi.
Na hapa JF katika post zetu tusitukanane, na hasa tusikejeli au kudharau imani za wenzetu.
Nawatakia mfungo mwema.