Majini, Mashetani, Mapepo na Mahayawani

Sumbalawinyo

JF-Expert Member
Sep 22, 2009
1,282
247
Hivi kuna tofauti gani kati ya Majini, Mashetani, Mapepo na Mahayawani?
Naomba msaada wenu ndugu wataalam.
Maana kanisani utasikia wakikemea pepo toka, Masheikh utawasikia wanafukuza majini.
Yaani vinanichanganyachanganya/
 
maneno hayo yote yana maana moja ila inategemeana na mahali.wabantu huita mapepo,majini au mizukan.k waarabu huita masheytwain.maruhani au majini.lakini kitheolojia yote yana maana moja tu kuwa ni roho chafu zinazoyokana na shetani.
 
Hivi kuna tofauti gani kati ya Majini, Mashetani, Mapepo na Mahayawani?
Naomba msaada wenu ndugu wataalam.
Maana kanisani utasikia wakikemea pepo toka, Masheikh utawasikia wanafukuza majini.
Yaani vinanichanganyachanganya/

Majini
ndio hao wanajulikana kwa majina mengine kama vile Mapepo, demons, Nephilim na majina mengine kadhaa wa kadhaa... they have no physical bodies.

Wameitwa MaJINNI kwa sababu ya kutokuonekana kwao na watu, na hii ni kwa sababu kila kisichoonekana kwa jicho la binadamu katika lugha ya kiarabu jina lake hutokana (hutoholewa) na herufi mbili hizi; Jiym na Nuun.


Mashetani: Hili neno linatokana na jina Shetani, na hii ni sifa mbaya na si jina.

Mahayawani: Hayawani حيوان (hayawani) neno hayawani peke yake lina maana ya Mnyama.

Ila wakati mwingine utumika kwa kuwapa watu sifa mbaya, sifa ya unyama, ndio utasikia mtu anaitwa Hayawani, wakimaanisha kuwa huyu mtu ni Mnyama. Mwenye tabia ya matendo machafu, unyama, Mazimbwezimbwe, ujinga, ukatili, n.k

Kuhusu demons, fungua viumgo hivi:

 
Majini au mapepo ni viumbe ambavyo havionekani kwa macho, ni viumbe kama malaika isipokuwa majini na mapepo yalifukuzwa mbinguni pamoja na shetani baada ya kuasi, na yalitupwa duniani yakisubiri siku ya mwisho ya hukumu.

Shetani na majini, wanajua kabisa kuwa jehanum ya moto ipo kwa ajili yao, ndiyo maana wanafanya kila mbinu wasiingie peke yao huko jehanum, shetani ni mwongo, laghai anawatumia sana wachawi, waganga wa kienyeji, wasoma nyota kupandikiza majini, kuiba nyota yako ya mafanikio, kuchukua watu misukule nk.

Kuna aina nyingi za majini baadhi yake ni kama:-

1) Murafari - hili ni jini linalozuia mafanikio ya kupata fedha, mafanikio ya elimu nk.
2) Latifu - hili jini linaloleta ufukara, mateso, hata ukipata pesa matumizi yake yanakuwa ni hovyo
3) Jahari - Jini anayetumiwa kuiba mali na kuzuia biashara kustawi
4) Hasinani - jini hili ni la fujo, ulevi wa pombe, bangi na dawa za kulevya
5) Jube - jini hili linasababisha utasa
6) Subiani - jini la ajali, linasababisha wanawake kutokupata siku zao, na kunyonya damu za akina mama siku zao za hedhi ambapo wanapata maumivu makali sana.
7) Sumil - jini hili huangamiza mimba changa
8) Waidadat - jini hili husababisha wanaume kuvaa hereni kusuka nywele na kutoga masikio.
9) Alibadiri - jini la kifo, likikupata kifo hutokea wakati wowote.
10) Anzura - Linawazuia vijana wa kike na kiume kuolewa/kuoa
11) Maimuna - linawakamata wanaume wenye ndoa zao hadi ndoa inavunjika
12) Makata - linasababisha vifo vya mfululizo kwenye familia
13) Faziur - jini la maandishi. Unaletewa barua ukiisoma tayari umelikwaa
14)Subha - jini hili linasababisha mtu kuwa na kiburi sana na kujiinua.
15) Maulan - jini linalofanya watu kuwa kichaa, au mtu ananuka wakati wowote
16) Al-maul - jini hili linamfanya mtu kuwa ombaomba
17) Zuhura au Zohari - Jini la fujo
18) Araba - Jini hili linafanya mtu apende sana ubani
19) Farkh - jini hili linatumwa hasa kwa wakristo kuangalia kama ana kinga (Wokovu)
20) Baradi - jini hili likikupata basi ndoa yako ni lazima itavunjika.
21) Shamsu - jini hili huvaa umbile la binadamu kwa sura yoyote.(sasa hivi mitaani majini haya yapo mengi sana)
22) Abuni - jini wa hasira
23) Kaimu - jini la kutambua nyota za watu
24) Tajuruni - jini la utajiri wa kichawi - ni lazima utoe kafara ya mwanao, mkeo au kufanya tendo la ndoa na mama yako mzazi
25) Al-taliki - jini hili linapoteza watu katika mazingira ya kutatanisha
26) Naluju - linasimamia lugha
27) Janatusi - linatumwa alfajiri kabla ya adhana kuleta usingizi kwa Wakristo wasifanye sala
28) Riyaron - jini hili linamfanya mtu afanye kila kazi peke yake
29) Zaitun - Jini hili linasababisha wasichana kuwa na maringo
30) Ruyati - jini linalosimamia ndoto mbaya
31) Al-rahabu - jini linalosababisha hitilafu ya umeme
32) Hadharaji - jini hili linafanya kazi ya kukata kichwa cha mtu ili wapate damu
33) Anazihaji - jini hili ndilo linachukua roho yako ukifa kwenye dhambi
34) Nghruk - linasababisha maafa
35)Munkara - jini la makaburini
36) Takadhuru - jini linaloleta mali za masharti.
37) Rabindi - jini la Waislamu pekee yao ili wafanye fujo.
38) Balishebe - jini la magonjwa yasiyopona
39) Sajiduri - jini linalokusaidia kupata pesa, kisha zinapotea kwa haraka
40) Rumiran - linasimamia uwongo
41) Lairlihabi - linasimamia hofu, kutojiamini na kukata tamaa
42) Rohani - jini la mateso na fujo
43) Betrah - jini hili linasimamia mapambo, kwa mwanamke huwa anajipamba isivyo kawaida, halikadhalika mwanaume
44)Hanshari - linatumiwa sana na waarabu kulinda maduka yao
45) Walihuni - linazunguka nyumba likilinda biashara
46) Kurasih - jini la kupoteza fahamu
47) Tarik - huondoa amani nyumbani, kazini. Linafanya watu wasielewane
48) Atha - mungu wa kiarabu wa kuabudu sanamu
49) Munakir - linapoteza watu kimiujiza
50) Malik - jini la kumiliki biashara
51) Ghatabu - jini la kulainisha macho wa wanawake. Wanakuwa wanarembua
52) Khatuh - jini la uchawi wa kuchukua kucha, nywele na nguo za ndani
53) Fanken - jini hili linasimamia mtu kuzunguza kiswahili cha pwani
54) Zamzam - jini la marashi na kusimamia mikataba ya imani. Mkristo anaposilimishwa basi hutupiwa jini hili kupofushwa akili yake.
55) Mukitala - linatumwa kuangalia kinga za watu
56) Laufili - jini la uvivu
57) Al-khah - linakula damu iliyoganda
58 Abasaa - jini la hasira wivu na jeuri
59) Aherumi - jini la homa za mara kwa mara
60) Muba - jini la maradhi ya kuambikiza
61) Kamariram - jini hili linatoa kinga kwa majambazi
62) Zubiran - jini la uongo na uzushi
63) Abadi - Jini la wizi, umalaya na ujambazi
64) Muzamili- jini la matambiko ya kiarabu
65) Ruhadi - jini la wizi, umalaya na umasikini
66 Usuran - jini la wizi, umalaya, ujambazi na umaskini
67)Tubuyali - jini hili linamfanya mtu kuiba vitu vya ndani ya nyumba. Haibi nje ya nyumba
68) Zirach - jini la wizi, umalaya, ujambazi na umaskini
69) Ashuran - jini la utasa na maradhi ya akina mama

Kinga ya majini haya ni nyepesi ni KUOKOKA na kusimama katika neno la Mungu. Kama unayo dalili yoyote iliyosababishwa na majini hayo hapo juu na umeokoka, taja jina la hilo jini, ni lazima litaitika, kisha liwashie moto.

Kama hujaokoka usiyarushie mawe au moto yatakuumiza. Mwuone kiongozi yeyote wa kanisa akuongoze sala ya toba, kisha anza kuwasha moto, hakika yatakimbia na kuacha biashara, kazi, ndoa, na watoto wako huru.
 
Back
Top Bottom