Majambazi Tarime waizidi nguvu Polisi

Msharika

JF-Expert Member
May 15, 2009
947
69
MAJAMBAZI wenye silaha zinazodhaniwa kuwa za kivita wamevamia Kituo Kikuu cha Wilaya ya Kipolisi ya Nyamwaga na kumimina risasi za moto katika ofisi zake na makazi ya maofisa wa polisi wanaoishi karibu na ofisi hizo.

Kamanda wa Kanda Maalumu ya Kipolisi Tarime, Constantine Masawe, amesema majambazi hao walivamia nyumba tatu tofauti zilizopo meta 20 kutoka kituo cha Polisi juzi saa tano usiku na kuwaweka watu chini ya ulinzi na kisha kuiba idadi kubwa ya ng’ombe na mbuzi wa eneo hilo.


Akiwafariji wananchi wa kijiji cha Nyamwaga jana asubuhi, Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Frank Uhalula ambaye aliitisha mkutano wa hadhara wa dharura, alisema ni jambo la kumshukuru Mungu kwamba hakuna aliyejeruhiwa katika tukio hilo kwa sababu risasi hazina macho.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti katika mkutano wa dharura, baadhi ya wananchi waliomba serikali kutafuta mbinu mbadala ya kukabiliana na wimbi la uhalifu katika Wilaya ya Tarime.

Baadhi ya wanakijiji hao walimwambia Uhahula kuwa polisi waliopo katika eneo hilo wana umri mdogo na hawana uwezo wa kubeba silaha nzito na kupambana na majambazi.

“Hao askari waliopo hapa ni watoto wadogo. Tunaomba askari waliokomaa na wenye uzoefu kupambana na majambazi,” alisema mwananchi aliyejitambulisha kwa jina la Francis Ghati.

Wengine waliomba serikali ipeleke Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) katika wilaya hiyo na kutangaza hali ya hatari katika eneo hilo.

“Tunaomba hata wanajeshi wastaafu wapewe bunduki watusaidie,” Mathias Juvinali ambaye ni mwanajeshi mstaafu alisema.


Mwananchi mwingine aliyejitambulisha kwa jina la Wankio Wambura alisema: “Huu ni ujumbe kwa Kanda Maalum ya Kipolisi …Serikali inapaswa kuweka kambi ya kijeshi hata Tarime kwa sababu inaonekana polisi wameshindwa."

Akijibu hoja hizo, Uhahula alikiri kuwa kuna haja ya vyombo vya dola kujipanga upya kukabiliana na hali hiyo. “Hili sio jambo jepesi. Ni kituo cha polisi kilivamiwa na polisi wetu hawakutoka hata kujibu. Ushauri wenu nimeuchukua na nitamwambia IGP”, alisema Uhahula.

Hadi jana polisi walikuwa katika msako wa kutafuta mifugo iliyoibwa bila mafanikio.
Kifaa cha mawasiliano ya kipolisi (radio call) kiliokotwa na wananchi na kurudishwa Polisi huku kikidaiwa kuwa mmoja wa polisi hao alikidondosha alipokuwa akikimbia.

Tukio hilo la kuteka kituo cha polisi na kuiba mifugo limetokea ikiwa ni chini ya mwezi mmoja tangu watu wasiojulikana walipovamia familia tatu za ukoo mmoja na kuua watu 17 na siku chache baadaye kuvamia harusi na kuua watu watano kwa risasi.

 
Kama mkoa mmoja tu au niseme ni wilaya moja au mbili tu zinazosumbua na serikali inashindwa kudhibiti, hali itakuwa kama mikoa mitatu au minne ikaingia kwenye hali kama hiyo?
 
Kikwete needs to go back to his library asome jinsi nyerere alivyodhibiti huu mkoa, sio kuchekacheka tu napa na ahadi hewa!!
 
hapo umri mdogo wa askari sio ishu,sababu hakuna askari anayeajiriwa chini ya miaka 18,na mpaka uwe askari lazima upige range bunduki zote unazotakiwa kufanyia kazi.Tatizo linaweza kuwa namba ndogo ya askari,mipango mibovu ya jeshi la police,sababu tatizo la tarime linajulikana cku nyingi.
 
MAJAMBAZI wenye silaha zinazodhaniwa kuwa za kivita wamevamia Kituo Kikuu cha Wilaya ya Kipolisi ya Nyamwaga na kumimina risasi za moto katika ofisi zake na makazi ya maofisa wa polisi wanaoishi karibu na ofisi hizo.


Wakizungumza kwa nyakati tofauti katika mkutano wa dharura, baadhi ya wananchi waliomba serikali kutafuta mbinu mbadala ya kukabiliana na wimbi la uhalifu katika Wilaya ya Tarime.

Wengine waliomba serikali ipeleke Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) katika wilaya hiyo na kutangaza hali ya hatari katika eneo hilo.

"Tunaomba hata wanajeshi wastaafu wapewe bunduki watusaidie," Mathias Juvinali ambaye ni mwanajeshi mstaafu alisema.

Hicho Kituo Kikubwa cha Wilaya cha Polisi kinafafanaje?sipati picha kamili kwa Wilayani hususan nikipiga picha ya hali ya Central Polisi Makao makao makuu na vituo vingine vya Dar!.si choka sana?

Kama iliwachukua zaidi ya masaa sita Polisi kule Arusha ( Mjini) kupamabna na majambazi wasio zidi watano waliopigana toka ndani sijui huko Tarime ambapo "vita ni vita" hali inakuaje kwa polisi ambao pengine anatembea hata kirungu wala filimbi hana?

Serikali inapoombwa kupeleka JWTZ Tarime ni kwamba hawapo au kwa ajili tu ya kupambana na majambazi?..Ni kwamba wananchi wamepoteza imani kiasi hiki na ghesi la polisi? vipi kile kikosi maalumu cha ""polishi" cha Kamanda Tossi hakipo tena au kilikuwa ni maonyesho tu?.

Hawa wanajeshi wastaafu wanaotaka watumika huko Tarime wanaaminika kiasi gani kwa wananchi mpaka wanapendekezwa wapewe silaha, ni kwamba wapo makini kulko Polisi waliopo kazini?...
 
MAJAMBAZI wenye silaha zinazodhaniwa kuwa za kivita wamevamia Kituo Kikuu cha Wilaya ya Kipolisi ya Nyamwaga na kumimina risasi za moto katika ofisi zake na makazi ya maofisa wa polisi wanaoishi karibu na ofisi hizo.

Kamanda wa Kanda Maalumu ya Kipolisi Tarime, Constantine Masawe, amesema majambazi hao walivamia nyumba tatu tofauti zilizopo meta 20 kutoka kituo cha Polisi juzi saa tano usiku na kuwaweka watu chini ya ulinzi na kisha kuiba idadi kubwa ya ng'ombe na mbuzi wa eneo hilo.


Akiwafariji wananchi wa kijiji cha Nyamwaga jana asubuhi, Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Frank Uhalula ambaye aliitisha mkutano wa hadhara wa dharura, alisema ni jambo la kumshukuru Mungu kwamba hakuna aliyejeruhiwa katika tukio hilo kwa sababu risasi hazina macho.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti katika mkutano wa dharura, baadhi ya wananchi waliomba serikali kutafuta mbinu mbadala ya kukabiliana na wimbi la uhalifu katika Wilaya ya Tarime.

Baadhi ya wanakijiji hao walimwambia Uhahula kuwa polisi waliopo katika eneo hilo wana umri mdogo na hawana uwezo wa kubeba silaha nzito na kupambana na majambazi.

"Hao askari waliopo hapa ni watoto wadogo. Tunaomba askari waliokomaa na wenye uzoefu kupambana na majambazi," alisema mwananchi aliyejitambulisha kwa jina la Francis Ghati.

Wengine waliomba serikali ipeleke Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) katika wilaya hiyo na kutangaza hali ya hatari katika eneo hilo.

"Tunaomba hata wanajeshi wastaafu wapewe bunduki watusaidie," Mathias Juvinali ambaye ni mwanajeshi mstaafu alisema.


Mwananchi mwingine aliyejitambulisha kwa jina la Wankio Wambura alisema: "Huu ni ujumbe kwa Kanda Maalum ya Kipolisi …Serikali inapaswa kuweka kambi ya kijeshi hata Tarime kwa sababu inaonekana polisi wameshindwa."

Akijibu hoja hizo, Uhahula alikiri kuwa kuna haja ya vyombo vya dola kujipanga upya kukabiliana na hali hiyo. "Hili sio jambo jepesi. Ni kituo cha polisi kilivamiwa na polisi wetu hawakutoka hata kujibu. Ushauri wenu nimeuchukua na nitamwambia IGP", alisema Uhahula.

Hadi jana polisi walikuwa katika msako wa kutafuta mifugo iliyoibwa bila mafanikio.
Kifaa cha mawasiliano ya kipolisi (radio call) kiliokotwa na wananchi na kurudishwa Polisi huku kikidaiwa kuwa mmoja wa polisi hao alikidondosha alipokuwa akikimbia.

Tukio hilo la kuteka kituo cha polisi na kuiba mifugo limetokea ikiwa ni chini ya mwezi mmoja tangu watu wasiojulikana walipovamia familia tatu za ukoo mmoja na kuua watu 17 na siku chache baadaye kuvamia harusi na kuua watu watano kwa risasi.

Mkuu MOD hii Topic haiusiani na Hapa ni Mambo ya Siasa sio Ujambazi Mkuu MOD nakuomba uihamishe hii Topic uipeleke kule kwa
( Habari na Hoja mchanganyiko )
 
Jamani, Jeshi la Polisi ni la kutuliza ghasia na si kujihusisha na combat.

Hawa majangili wa Mara ni kajijeshi fulani. Wanahitaji kukabiliwa na Jeshi la combat, yaani JWTZ.

Tusipoangalia hawa watu wanaweza hata kuunda jeshi la uasi chini ya pua zetu!
 
Exactly what I was thinking. Kikwete hivi anafikiria nini na huyo waziri wake wa usalama.
Ukiiacha tarime ifanye inavyofanya kuna watu wataamini kuwa Kikwete hana uwezo wa ukakamavu.
Dear Kikwete,
DO SOMETHING AND STOP SMILING BEFORE PEOPLE DECIDE TO COME TO YOUR OWN BED IN IKULU WITH GUNS.
Sijui utaendelea ku smile tu wakimkamata mama salma!! And mind you it will be your own friends. Because they are looking for your signs of weakness and you are showing them!!!!
 
MAJAMBAZI wenye silaha zinazodhaniwa kuwa za kivita wamevamia Kituo Kikuu cha Wilaya ya Kipolisi ya Nyamwaga na kumimina risasi za moto katika ofisi zake na makazi ya maofisa wa polisi wanaoishi karibu na ofisi hizo.

Kamanda wa Kanda Maalumu ya Kipolisi Tarime, Constantine Masawe, amesema majambazi hao walivamia nyumba tatu tofauti zilizopo meta 20 kutoka kituo cha Polisi juzi saa tano usiku na kuwaweka watu chini ya ulinzi na kisha kuiba idadi kubwa ya ng’ombe na mbuzi wa eneo hilo.


Akiwafariji wananchi wa kijiji cha Nyamwaga jana asubuhi, Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Frank Uhalula ambaye aliitisha mkutano wa hadhara wa dharura, alisema ni jambo la kumshukuru Mungu kwamba hakuna aliyejeruhiwa katika tukio hilo kwa sababu risasi hazina macho.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti katika mkutano wa dharura, baadhi ya wananchi waliomba serikali kutafuta mbinu mbadala ya kukabiliana na wimbi la uhalifu katika Wilaya ya Tarime.

Baadhi ya wanakijiji hao walimwambia Uhahula kuwa polisi waliopo katika eneo hilo wana umri mdogo na hawana uwezo wa kubeba silaha nzito na kupambana na majambazi.

“Hao askari waliopo hapa ni watoto wadogo. Tunaomba askari waliokomaa na wenye uzoefu kupambana na majambazi,” alisema mwananchi aliyejitambulisha kwa jina la Francis Ghati.

Wengine waliomba serikali ipeleke Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) katika wilaya hiyo na kutangaza hali ya hatari katika eneo hilo.

“Tunaomba hata wanajeshi wastaafu wapewe bunduki watusaidie,” Mathias Juvinali ambaye ni mwanajeshi mstaafu alisema.


Mwananchi mwingine aliyejitambulisha kwa jina la Wankio Wambura alisema: “Huu ni ujumbe kwa Kanda Maalum ya Kipolisi …Serikali inapaswa kuweka kambi ya kijeshi hata Tarime kwa sababu inaonekana polisi wameshindwa."

Akijibu hoja hizo, Uhahula alikiri kuwa kuna haja ya vyombo vya dola kujipanga upya kukabiliana na hali hiyo. “Hili sio jambo jepesi. Ni kituo cha polisi kilivamiwa na polisi wetu hawakutoka hata kujibu. Ushauri wenu nimeuchukua na nitamwambia IGP”, alisema Uhahula.

Hadi jana polisi walikuwa katika msako wa kutafuta mifugo iliyoibwa bila mafanikio.
Kifaa cha mawasiliano ya kipolisi (radio call) kiliokotwa na wananchi na kurudishwa Polisi huku kikidaiwa kuwa mmoja wa polisi hao alikidondosha alipokuwa akikimbia.

Tukio hilo la kuteka kituo cha polisi na kuiba mifugo limetokea ikiwa ni chini ya mwezi mmoja tangu watu wasiojulikana walipovamia familia tatu za ukoo mmoja na kuua watu 17 na siku chache baadaye kuvamia harusi na kuua watu watano kwa risasi.

Hivi ndiyo vitu amabvyo mrema alifanikiwa akiwa wizara ya mambo ya ndani.
 
Muheshimiwa Pinda aliwahi kunukuliwa kuwa atamshauri Rais kuwa Tarime iwe na utawala wa Kijeshi, Lakini nafikiri badala yake serikali ikafanya siasa na kuanzisha wanachokiita kuwa ni kanda maalum ya kipolisi. Sasa sijui ikishakuwa kanda maalum ndo ufanisi unaongezeka au la. Lakini nafikiri matokeo tunayaona ndani ya kanda maalum.
Ni ukweli usiofichika kuwa ni aibu kwa serikali kama majambazi yamefanikiwa kuvamia kituo cha polisi na kupora nyumba za jirani huku kituo kikiwa chini ya ulinzi, na wakafanikiwa kuondoka salama. Tujiulize hawa majambazi kesho wakiingia bank au sehemu yoyote wanayotaka nani atawazuia? kwa sababu wana uwezo wa kuwateka polisi wote na kuwafungia ndani
 
Back
Top Bottom