Kishongo
JF-Expert Member
- May 4, 2010
- 932
- 64
PAMOJA na dhamana kuwa haki ya msingi ya mshitakiwa, katika kesi ya Mbunge wa Arusha
Mjini, Godbless Lema (Chadema), Mahakama ina haki ya kuizuia dhamana hiyo.
Wakizungumza na gazeti hili hivi karibuni baadhi ya Majaji wa Mahakama Kuu walionya kuwa
Mahakama si gari bovu, kwamba kila mshitakiwa au jamaa zake, wanaweza kuisukuma itende
watakavyo, kwa kuwa inafanya kazi kwa kuzingatia sheria na misingi ya haki.
Walifafanua kuwa nafasi ya Mahakama kutoa dhamana kabla ya siku ya kesi iliyopangwa kwa
mshitakiwa aliyeikataa awali, haipo kisheria si tu kwa aliyeikataa kwa makusudi bali hata kwa aliyekosa wadhamini kwa bahati mbaya.
Walikuwa wakizungumzia sakata la dhamana ya Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema
(Chadema) ambaye wiki iliyopita aling'ang'ania kwenda rumande katika Gereza Kuu la Mkoa wa Arusha la Kisongo licha ya dhamana yake kuwa wazi kwa kile alichodai kuwa anaandamwa
na Polisi kwa kufunguliwa mashitaka mengi.
Pia Lema katika uamuzi huo wa kutokubali dhamana alisema ni bora aendelee kukaa rumande
kama ishara ya kutetea wanyonge kabla ya kubadilisha uamuzi wake akitaka dhamana baada ya kilichoitwa kushauriwa na Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe lakini akanyimwa
na Mahakama.
Majaji hao wa Kanda ya Dar es Salaam ambao hawakutaka kutajwa majina yao walisema
hakimu aliyemkatalia Lema dhamana, alitoa msimamo sahihi kisheria, utakaowafanya watu
wengine kuheshimu taratibu za Mahakama.
Wakati mmoja wao akisisitiza kuwa dhamana ni haki ya mshitakiwa pale atakapokuwa
ameikubali, mwingine alisema si kazi ya Mahakama kulazimisha mshitakiwa kukaa nje ya Mahakama endapo yeye mwenyewe (mshitakiwa) haoni umuhimu wa kufanya hivyo.
Lakini alifafanua kuwa mahakimu wanapokubali kutoa dhamana kwa washitakiwa wanaokuwa wamekosa wadhamini wakati kesi zao zinapofikishwa mahakamani, ni ubinadamu tu na wala si matakwa ya kisheria.
"Inawezekana watu wanadhani kinachofanywa na mahakimu wengi kwa sababu ya ukarimu kutokana na washitakiwa kukosa wadhamini wakati ule kesi zao zinaposomwa mahakamani ni maelekezo ya sheria. Ule ni utu tu wa hakimu na hakuna sheria inayolazimisha hilo litendeke.
"Sasa sembuse mshitakiwaanayegomea haki yake ya dhamana? Huyu hana njia ya mkato ya kuwa nje, ni lazima asubiri kesi inapoletwa tena mahakamani, ndipo aombe dhamana yake kwa kufuata taratibu za kimahakama," alifafanua Jaji huyo.
Jaji mwingine aliongeza kwamba Lema alipaswa kufikiria kuwa ana majukumu mengine bungeni na hivyo kukataa dhamana kwa sababu yoyote, kusingeweza kuisukuma Mahakama kumbembeleza afanye vinginevyo, eti kwa sababu ni kiongozi.
"Kesi hupangwa kila baada ya siku 14, sasa Lema alipaswa afikirie na kukumbuka hilo kabla ya kugomea dhamana, kwa sababu Hakimu yeyote hawezi kukubali kupindisha sheria na kuandika hati ya dhamana kwa mtu aliyetingisha kiberiti, wakati muda wa kesi yake uliopangwa haujafika. Kwanza kugomea dhamana ni makusudi na sheria haiendelezi makusudi hayo," alisema.
Source: GAZETI HABARILEO
Mjini, Godbless Lema (Chadema), Mahakama ina haki ya kuizuia dhamana hiyo.
Wakizungumza na gazeti hili hivi karibuni baadhi ya Majaji wa Mahakama Kuu walionya kuwa
Mahakama si gari bovu, kwamba kila mshitakiwa au jamaa zake, wanaweza kuisukuma itende
watakavyo, kwa kuwa inafanya kazi kwa kuzingatia sheria na misingi ya haki.
Walifafanua kuwa nafasi ya Mahakama kutoa dhamana kabla ya siku ya kesi iliyopangwa kwa
mshitakiwa aliyeikataa awali, haipo kisheria si tu kwa aliyeikataa kwa makusudi bali hata kwa aliyekosa wadhamini kwa bahati mbaya.
Walikuwa wakizungumzia sakata la dhamana ya Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema
(Chadema) ambaye wiki iliyopita aling'ang'ania kwenda rumande katika Gereza Kuu la Mkoa wa Arusha la Kisongo licha ya dhamana yake kuwa wazi kwa kile alichodai kuwa anaandamwa
na Polisi kwa kufunguliwa mashitaka mengi.
Pia Lema katika uamuzi huo wa kutokubali dhamana alisema ni bora aendelee kukaa rumande
kama ishara ya kutetea wanyonge kabla ya kubadilisha uamuzi wake akitaka dhamana baada ya kilichoitwa kushauriwa na Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe lakini akanyimwa
na Mahakama.
Majaji hao wa Kanda ya Dar es Salaam ambao hawakutaka kutajwa majina yao walisema
hakimu aliyemkatalia Lema dhamana, alitoa msimamo sahihi kisheria, utakaowafanya watu
wengine kuheshimu taratibu za Mahakama.
Wakati mmoja wao akisisitiza kuwa dhamana ni haki ya mshitakiwa pale atakapokuwa
ameikubali, mwingine alisema si kazi ya Mahakama kulazimisha mshitakiwa kukaa nje ya Mahakama endapo yeye mwenyewe (mshitakiwa) haoni umuhimu wa kufanya hivyo.
Lakini alifafanua kuwa mahakimu wanapokubali kutoa dhamana kwa washitakiwa wanaokuwa wamekosa wadhamini wakati kesi zao zinapofikishwa mahakamani, ni ubinadamu tu na wala si matakwa ya kisheria.
"Inawezekana watu wanadhani kinachofanywa na mahakimu wengi kwa sababu ya ukarimu kutokana na washitakiwa kukosa wadhamini wakati ule kesi zao zinaposomwa mahakamani ni maelekezo ya sheria. Ule ni utu tu wa hakimu na hakuna sheria inayolazimisha hilo litendeke.
"Sasa sembuse mshitakiwaanayegomea haki yake ya dhamana? Huyu hana njia ya mkato ya kuwa nje, ni lazima asubiri kesi inapoletwa tena mahakamani, ndipo aombe dhamana yake kwa kufuata taratibu za kimahakama," alifafanua Jaji huyo.
Jaji mwingine aliongeza kwamba Lema alipaswa kufikiria kuwa ana majukumu mengine bungeni na hivyo kukataa dhamana kwa sababu yoyote, kusingeweza kuisukuma Mahakama kumbembeleza afanye vinginevyo, eti kwa sababu ni kiongozi.
"Kesi hupangwa kila baada ya siku 14, sasa Lema alipaswa afikirie na kukumbuka hilo kabla ya kugomea dhamana, kwa sababu Hakimu yeyote hawezi kukubali kupindisha sheria na kuandika hati ya dhamana kwa mtu aliyetingisha kiberiti, wakati muda wa kesi yake uliopangwa haujafika. Kwanza kugomea dhamana ni makusudi na sheria haiendelezi makusudi hayo," alisema.
Source: GAZETI HABARILEO