Maisha yangu nimeyaharibu mwenyewe

SeHEMU YA TISA (9)

Tulipoishia…

Tabia ya kwenda porini ikakua na tukaanza kucheza kamali kule. Tulikua tukicheza kamali ya karata na dau nakumbuka lilikua 100 au siku nyingine 200. Ilikua pesa nyingi kwa maisha ya shule kwani ukipigwa kama elfu 3 hivi basi wiki nzima utakunywa uji mkavu…

Nikawa na ukaribu wa mdada flani (tumwite Tina) alikua mwanafunzi wa O-level… Asee kumbe yule dada kuna mwalimu anamtaka…. Hapa nikawa nimeyatimba

Tuendelee sasa…

Tina alinijuza kuwa kuna mwalimu huwa anamtaka sana na sasa ananiulizia.

Ngoja nipunguze maelezo naona watu wamesema hayana umuhimu

Huyu Tina alinipa msala, alikuja kupata mimba shuleni alafu kila mtu akawa anasema lazima mimba ni yangu. Tulikua form 6 tayari hapo na maisha ya kucheza kamali na kutoroka shule nilishayazoea

Nilishauza zile counterbook zote 12, nilibaki na moja tu la masomo yote. Niliuza vitu vyangu vingi mnoo

Katika yooote sikuacha kwenda kanisani jumapili. Na kuna mzee mmoja alikua na mwanae yuko form 4 pale shuleni. Yule mzee alinipenda sana, akawa kila jumapili lazima aniletee matunda pale kanisani, sikunyingine samaki au dagaa. Mzee alikua akinisisitiza nisome lakini mwanae pia asome kwani wana maisha duni na ni mtu pekee kwao walikua wakimtegemea (huyu dogo nilikuja kutana nae baada ya miaka 6 hivi mbele, pia story yake nimeiachia hapa)

*Kuna kipande muhimu sana cha dada kiongozi wa Dini haswaaa, nilijikuta kwenye mahusiano nae na hata nilivyoenda chuo bado nilikua nae. Huyu Dada nilimfanyia vitu vya ajabu sana kwakweli na niseme nilipoteza mtu muhimu basi tu. Ila sasa nikileta story yake watu watasema najizungusha story iwe ndefu.

Tuendelee kwa ufupi yule Tina alikuja gundulika ana mimba na mwenye mimba sio mimi, kuna jamaa flani alipewa msala huo. Maisha yakaendelea
Mtahani wa mock wa form 6 nilifeli tena… Nilipata 3 ya mwisho…

Kwa kipindi kilichobaki niliona nikomae na shule tu. NECTA ilifika nikafaulu na baadae nilichaguliwa kwenda SAUT Mwanza


TUENDELEE, NTASOMA MAONI YA WENGI KAMA TWENDE NA SUMMARY AU NIELEZE KWA KINA MATUKIO MUHIMU HADI NIMALIZE MKASA WANGU

ASANTENI
 
SEHEMU YA TISA (9) Part 2 (in details)

Habari ndugu zangu wanaJF
Nimesoma maoni ya wengi na ntaendelea na story bila kuacha detail zote muhimu

Sasa nitaendelea na sehemu ya yule binti wa kanisani sambamba na yule bwana mdogo ambaye Baba yake alitokea kunikubali sana.

Tuendelee sasa….

Wakati nikiwa najiandaa na mtihani wa NECTA (ilikua imebaki kama miezi miwili hivi) kuna siku niko bwenini simu yangu iliita na ilikua namba ngeni lakini baadae niliitambua sauti kuwa ilikuwa ya yule binti wa kanisani (Tumwite mama mchungaji) hili jina hata shule walikua wakimuita hivyo.

Alipiga simu akimuulizia mdogo wake flan wa O-level kama ntaweza onana nae kesho nimpe simu waongee. Mama mchungaji alikua kashamaliza form four kwa wakati huo ( System ya zamani olevel walikua wanamaliza mwezi wa 10 hivi then advance tulikua tunamaliza mwezi wa 5) naamini wengi mnakumbuka.
So mama mchungaji hakuwepo shule tena ila nilikua nafahamiana nae vizuri tu kama nilivyowaambia nilikua church boy wakati fulani shuleni.

Kwa kunitazama hivi nilikua kijana mstaarabu sana, hii nasikia hadi leo watu huwa wanasema. Sasa mama mchungaji alikua anapenda kunishirikisha sana mambo ya biblia sana na nilikua nikimsikiliza, alikua pia na ushawishi mkubwa sana kwa wanafunzi kutokana na tabia yake njema sana.
Kukazia tu, mama mchungaji alikua mzuri jamani, Mchaga flani aliyekulia Mbeya.

Turudi kwenye simu yake sasa, tuliongea sana siku hiyo na nikamuuliza alitoa wapi namba nae akaniambia aliiomba kwa binti fulani walimaliza nae (nilikua mtu wa totoz so namba zangu wengi walikua nazo). Baada ya maongezi mengi na mama mchungaji basi tulikubaliana tutakua tukiwasiliana.

Mawasiliano yaliendelea na mama mchungaji alionyesha kunielewa na mimi nilikuwa na hisia hizo pia. Nilivutiwa sana na tabia yake. Ni aina ya mwanamke ukiwa nae huwezi kuwa na stress. She is amaizing kwakweli.

Baada ya wiki kadhaa mbele, mimi na mama mchungaji tukawa wapenzi ila ndo kwenye simu sana maana alikua home mimi niko shule. Tulipanga ntakapomaliza mitihani basi kabla sijarudi Dar tutaonana tushinde siku nzima. (Mama mchungaji alikua anakaa Tukuyu mjini). Amelelewa na baba yake mzazi na mama wa kambo. (Mama yake alifariki miaka mingi nyuma). Baba yake ni mchungaji kweli.

Maisha ya shule yaliendelea na wakati huu nilikuwa busy sana na masomo nikiwa na ndoto ya kufika chuo kikuuu. Matokeo ya Mock yalifanya nijitambue na kuanza kukaza buti.

Niwarudishe nyuma kidogo maana kuna mdau aliuliza kama nilikua narudi Bukoba.
Maisha yote ya Advance sikuwahi kurudi Bukoba. Ilikua likizo nakuja Dar na wakati wote huo B.mkubwa alikua anahakikisha nasoma tuition wakati wa likizo.
So nilipokua narudi shule, almost topic zote mi nilikua nishasoma huko likizo. Advance napo sikuwahi teseka kwa kukosa mahitaji ya muhimu, isipokuwa nilikua natumia oesa vibaya kwenye kamali, Disco vumbi na mara chache sana nilikua nikinywa pombe wakati wa disco.
So nilikua nishakua kijana wa Dar na Mbeya

Kula tulipokua tukifunga basi lazima twende Mbeya mjini, tukale maisha club alafu kesho ndo safari kwenda Dar.


Turudi kwa mama mchungaji, penzi letu lilikua la moto sana, simu nyingi usiku na sms kibao na nilimpenda yule binti.

Tulifanya mtihani salama na vitu vyangu kama Godoro, Blanketi na vingine vyote nilimwachia yule bwana mdogo ambaue baba yake ananikubali sana.
Yule Baba aliniletea kuku watatu kama asante ya kukaa na mwanae vizuri na pua kama zawadi kutokana na maisha ambayo niliishi na yule mzee ( nilikua weekend nnapoenda mtaani lazima nipite kwake nimsalimie yeye na familia, niaga kuondoka lazima anifungie maparachichi na vitu vingine vya kula) niliipenda sana ile familia sanaaaa. Bwana mdogo yule alikua kijana asiye na mambo mengi, alipenda sana shule na kila nilipokua napata nafasi tulishauriana mengi kuhusu maisha.

Ntatoa code ya shule niliyosoma maana naona wengi washaijua. Nimesoma shule iko ndani ndani sana inaitwa Lufilyo

Niliondoka shule baada ya siku 2 nilipomaliza mtihani wa NECTA, tukaoanda canter kama kawaida safari moja kwa moja tukuyu.

Nilishapanga na mama mchungaji kuwa siku hiyo ntalala tukuyu na ntaondoka kesho kuelekea mbey mjini ili keshi kutwa nirudi Dar.

Nilifika Tukuyu kama saa nne hivi asubuhi na mama mchungaji alikuja pale lodge nilipofikia ila kuingia aligoma. Nilitoka nikaenda kumwona, tuliongea sana na baadaye nikamsindikiza then nikarudi lodge.

Pale lodge sikuwa mwenyewe, nilikua na marafiki zangu kadhaa tushaoanga lazima jioni tukamwagilie moyo.
Yule dreva tax kama mnakumbuka alinipiga nauli day 1 nimefika Tukuyu alishakua mshikaji wangu sana na kila nilikua nikifika Tukuyu yeye ndo anakuwa mwenyeji wetu wa kutuonyesha machimbo.

Saa tisa mama mchungaji alikuja tena na this time nilimwomba aingie ndani. Tuliongea mengi, tulikiss sana na hatimaye aliamua kunitunuku tunda (baada ya mtafutano mwingi)

Mama mchungaji alikua bikra kabisaa kama ilivyokua kwa Clara. Jioni nilimsindikiza home hakua na hali nzuri sana lakini hakukuwa na namna. Tulipeana ahadi nyingi za kuoana mbeleni na kiukweli sikua namdanganya, nilimpenda sana yule binti.

Maisha ya kwao mama mchungaji yalikua na challenge kidogo, hakuwa anatokea familia bora alafu yule mama wake wa kambo alikua akimpiga matukio mengi sana. Hivyo mama mchungaji alikua akiniona kama mfariji wake mkuu, na nilikua nikifanya hivyo. Nilimpenda sana na kumjali sana.

Wakati nikiwa advance nilijiunga na mtandao wa facebook na kiukweli nilijipatia umaarufu mkubwa sana facebook, kipindi kile ukikuta mtu ana friends 5000 huyo ni noma na ndo ilikua limit. Baada ya hapo hata friend request zilikua zinagoma unaambiwa mtu huyu kafikia limit.

So upendo wangu kwa mama mchungaji ukafanya hadi nimpost facebook.
Ilikua kosa maana wale watumishi sasa (wanafunzi waliokuwa wakusali sana na mama mchungaji) wakaanza kumjaza maneno kuwa umekuaje awe na mtu kama mimi, Wale jamaa walikua wanajua code zangu nyingi akiwemo HP (Kiranja mkuu)

Nakumbuka wakati tuko shule HP alishatuita akasema sisi ndo tutaaibisha shule kwenye matokeo ya NECTA sababu ya tabia zetu.
HP pua alikua mwenyekiti wa CASFETA ambapo mama mchungaji alikua akisali hivyo wanajuana vizuri sana maana mama mchungaji alikua kiongozi pia.

Presha ilikua kubwa kwa mama mchungaji kwamba aache kuwa karibu na wahuni (Mimi) kwa ufupi alipokea simu nyingi zikinielezea vibaya

Personality yangu ni kijana flani mpole sana unless ujue mambo yangu kiundani, ila watu wengi ukiwaambia hata nakunywa pombe watabisha.

Mama mchungaji hakuniacha na nilimuhakikishia kwamba wanayosema mengine ni kweli mengine sio na niliahidi kujirekebisha, na yeye hakuwa na shida alikubaliana na mimi.

Matokeo ya form 4 yalishatoka wakati hui na mama mchungaji hakufanya vizuri sana, alipata 4 ya 26 ila combination hazikubalance. So alikua na option ya kwenda kusoma chuo cha ustawi Iringa pale.

Mchakato wa kwenda chuo ulimchosha sana kwani nyumbani kwao uchumi haukua mzuri na mimi sikua na msaada zaidi ya kumpa pole na kumfariji.
Wakati huo wote mi nilikua Dar na maisha yalikua yanaenda vizuri tu nikiwa nasubiri matokeo.

Mama mchungaji alifanikiwa kwenda chuo japo kwa kuunga unga sana na mzee wake alimwona lecture mmoja pale awe anakaa kwake (hakuwa na uwezo wa kulipa Hostel).
Yule lecture alikua ni mwanamke kwakweli alimpa shida sana mama mchungaji, kazi nyingiii na matatizo mengine (mnaelewa ambao mmeishi kwa watu).


Mama mchungaji alikua mvumilivu sana na hakuwahi kusema hata kwa Baba yake, alikua akiniambia mimi tu. Nilikua faraja yake na kwakweli kwa aliyopitia pale, inahitaji ujasiri sana kuendelea kuishi na yule Lecture.

Kwa upande wangu matokea yalitoka na nilifaulu kwenda chuo. Nilichagua course ya Mass communication ingawa home B. Mkubwa hakunielewa kabisaa alisema ntakosa mkopo bora nisome education.
Sikua na wito wa ualimu at all so niliwatafuta kaka zangu wale wa UDSM (mtoto wa aunt wa bukoba) na kaka yangu kabisa wakati huo yeye alikua UDOM anasoma shahada ya kwanza ya Udaktari wa binadamu.
Tulifanikiwa kumshawishi aunt na kwenye kuchagua vyuo education niliweka ya mwisho kabisaa. Nikachagua Mass Comm~SAUT MWANZA then Health system management~Mzumbe na kuendelea

Nilichaguliwa SAUT Mwanza na nilifurahi sana maana nilikua napenda kusoma mambo ya uandishi wa habari.

Mama mchungaji alifurahi sana japo alikua na huzuni kwamba naenda mbali zaidi lakini nilimwambia hakuna shida tupambanie future yetu.

Siku zilisonga na nilitakiwa kwenda chuo sasa, wakati huo nawaza kurudi mwanza nikawa namkumbuka mpenzi wangu wa mwanza Clara.
Nilitakiwa kwenda Bukoba kwanza kufata cheti changu cha o-level (transcript) kwa ajili ya kuapply mkopo.


Safari ya Dar - Bkb ilianza na nilifika salama kesho yake mchana, nilipata cheti changu, aunt wa Bk alifurahi sana kuona naenda chuo lakini kiherehere kikanituma niulize kuhusu Jane na nikaambiwa ana kama wiki 2 amerudi kwao na anakaribia kujifungua mtoto wa 2 (Jane alikua ameolewa na yule jamaa anayefanya kazi dar ila kwao ni Bukoba)

Nilienda kwao na Jane na mdogo wake alinofungulia mlango, nikakaa sebuleni kumsubiri Jane. Alikuja baada kama ya dak 5 na alikua anaonekana kuchoka, mimba yake ilikua kubwa. Hakuwa na hasira na mimi tena, tulipiga story nyingi nikampongeza kwa hatua aliyofikia nae akanipongeza sana aliposikia naenda chuo.
Niliondoka kwao na kurudi home na mambi mengine yaliendelea..

Nilifanikiwa kurudi dar salama na nikaendelea na mchakato wa kuapply mkopo. Siku zikasonga hatimaye nikaenda chuo. Ada ya kuanzia na matumizi yoote alinipa b.mkubwa hela (majibu ya mkopo kwa kipindi hiki yalikua yanatoka wakati watu washaanza kureport vyuoni)

Safari to Mwanza ikaanza na nilifikia kwa mzee pale Mwanza, kesho yake nikaenda chuo kufanya reg na utaratibu mwingine.
Nilitafuta hostel za nje (SAUT MWANZA ni miongoni mwa vyo vyenye hostel za nje nzuri kuliko vyuo karibia vyote Tz) hapa watu waliosoma SAUT watadhibitisha hili.

Kuna rafiki yangu mmoja nilisoma nae advance nae alichaguliwa Mass comm ila alikua hajafika chuo. Tulikubaliana kukaa wote na pesa ya awali nililipa mimi then yeye atakuja amalizie.

Nilikamilisha taratibu za malipo yote chuoni, hostel na kila kitu kilikua poa na nilikua tayari sasa kuanza maisha mapya ya chuo.
Mzee alinipa pesa kidogo pia.


TUTAENDELEA…

Maoni yako ni muhimu na nasoma yote ili niweze kuendelea na story yangu
 
SEHEMU YA KUMI (10)
Tulipoishia…

Nilikamilisha taratibu za malipo yote chuoni, hostel na kila kitu kilikua poa na nilikua tayari sasa kuanza maisha mapya ya chuo.
Mzee alinipa pesa kidogo pia.

Tuendelee sasa

Maisha ya chuo yaliendelea na ndani ya wiki mbili majibu ya waliopata mkopo yalitoka.
MUNGU mkubwa nilikua kwenye list ya waliopata mkopo na nilikua nna asilimia 90+ nilifurahi sana hii siku.

Sasa nakumbuka mzee alinitext akasema kama niko free niende home kuna harusi ambayo amechanga na ana kadi 2, so moja ntaenda mimi na bro (Bro alikua likizo wakati huo na alikuja mwanza kusalimia, likizo za watu wanaosoma medical zilikua kidogo tofauti na sisi wengine)

Nilienda home kwa bashasha na mbwembwe sana maana niliona kitendo cha kupata mkopo basi maisha yangu chuo yatakua poa.
Tulijiandaa tukaenda harusini ilikua mwanza town pale, ukumbi ulikua ghorofani ila sikumbuki vizuri unaitwaje.

Tumeingia ukumbini mi hata maharusi siwajui ila nilishangaa kukutana na watu wengi tuliosoma wote primary na baadhi secondary kule mwanza (Rejea epsode 1& 2)
Nilifurahi sana kuonana na sura zile na story zilikua nyingi ikiwemo now unafanya nn, mi jibu langu lilikua straight, niko SAUT nasoma.

Tulipata meza katikati ya ukumbi na tulikaa hapo mimi na bro pamoja ma watu wengine nisiowafahamu (mzee hakua na muda na sisi, alikua na marafiki zake)
Ile furaha ya kupata mkopo ikanituma ninywe pombe. Sasa hadi wakati huu sikua nime-master unywaji wa pombe maana nilikua nakunywa mara chache sana.
Hii siku nilikunywa pombe sana na nilichanganya hadi inafika muda wa chakula mimi nilikua hoi na bro alitambia hilo. Basi akanifatia chakula, kitendo cha chakula kufika mezani tu mimi nilitapika sana baada ya kusikia harufu ya msosi na nikazima tena kama kule bukoba.

Kaka yangu alihangaika sana na mimi akanipa maji mengi, sasa issue ilikua kunitoa pale ukumbini hadi chini. Sikua na nguvu kabisa na yeye asingeweza peke yake. Mzee alishaona lile tukio na aliamua kulinda heshima yake, hakusogea hata nilipokua, alimtext bro kuwa anipeleke home. Bro alimpigia jirani yetu mmoja akaja na boda chap wakanipeleka home. Huko home hali haikua nzuri kwani niliendelea kutapika sana na baadae nikapitiwa na usingizi.
Asubuhi bro alienda kununua zile IV Fluids (Drip) akaniwekea canula mkononi then drip akatundika dirishani nikaanza kula dozi (bro alikua mwaka wa 3 wakati huo so alikua amemaster vitu kadhaa vya medical)
Mzee hakusema kitu kuhusu mimi kulewa na asubuhi alijiandaa akaenda kwenye shughuli zake.
Baada kama ya masaa manne nilikua naweza kupiga story na watu kabisa pale home ila nilikua weak bado.
Sasa siku hiyo ilikua ndo FIESTA Mwanza na ilikua inafanyikia CCM Kirumba pale.

Bro na marafiki zake kadhaa niliwasikia wakipanga kwenda FIESTA, Nikakumbuka kuna rafiki zangu wawili kule chuo walisema twende FIESTA. Sasa ikabidi nimwambie bro kuwa tutaenda wote jioni ila tukifika huko mi ntaachana nae na ntaungana na marafiki zangu. Bro alinikazia nikaona nikae kimya. Akaniwekea drip ya mwisho kisha sikujua wameondoka vipi, alinikwepa 😅.

Saa moja jioni nilikua fit na nikaanza kucheck na marafiki zangu wa chuo, walisema kuwa wataenda FIESTA na mimi nakawaambia tutakutana uwanjani. Saa tatu kamili nilikua nimejiandaa tayari na chap nikaondoka zangu ila sikua fit sana.

Nilifika CCM Kirumba nikalipa kingilio huyoo nikaingia ndani, katika zunguka zunguka nilikuatana na bro na marafiki zake walivyoniona wakacheka sana kisha bro akasema wao wana ratiba zao na mimi niendelee na zangu.
Nilikutana na marafiki zangu mle ndani saa nne na tukaanza kuvibe ila mi nilikua nakunywa maji tu.
Baada kama masaa mawili niliona kabisaa sina nguvu hata kusimama kuangalia wasanii ikawa issue. Nikaaga pale huyooo nikapanda boda hadi home nikalala.

Kesho jioni nilirudi chuo kuendelea na maisha ya kusoma.

Sasa wakati huu wote sikua na ukaribu sana na Mama mchungaji maana nilikua na mambo mengi lakini pia yule Clara alikua ashaanza kuwasiliana sana na mimi.
Clara ni binti aliyenipenda sana sanaaa na kwakweli mi kwa wakati huo sikua nampa muda sana.

Mama mchungaji aliendelea kupitia changamoto za pale anapokaa lakini Mungu ni mwema alifanikiwa kumaliza masomo yake ya certificate. Kwenye kuomba chuo ili asime diploma alichagua kimoja cha Mkoani Mara na chuo cha hapo Iringa kama sikosei (nnachokumbuka alichagua vyuo viwili) lengo la kuchagua mkoa wa Mara ilikua alitaka kuwa karibu na mimi. Mara na mwanza sio mbali sana hivyo aliamini tungekua tukionana sana.
Mimi nilimuunga mkono lakini niwe muwazi sikua namjali tena kama mwanzoni.

Hapo nilishaanza kuonana na Clara mara kadhaa na kushiriki nae tendo.
Mwaka wa kwanza wote sikutaka kujihusisha na mahusiano chuoni. Nilikua nakumbuka namna B.mkubwa alinishihi sana kuhusu wanawake chuo. (Nakumbuka alisema ukiona umeshindwa kujizui tumia kondomu)
Hivyo mwaka wa kwanza nilikua nikipoteza muda sana na Clara

Huyu Clara nilikua napajua kwao na kwetu wanamjua vizuri tu. Kuna wakati nilikua nikienda kumtembelea mzee home namshtua Clara anakuja na nilishafanya nae tendo pale pale home🤦🏿‍♂️

Majibu ya mama mchungaji yalitoka na alikua amechaguliwa kujiunga na chuo cha Mara kule. Hivyo alitakiwa akasome diploma yake huko.
Kwa upande wangu nilikua nishakua na ujanja ujanja wa chuo, nishajua kuvaa kama mwanachuo na nilishanunua smartphone HUAWEI Y300 kama sikosei.

Siku zilienda na tulikua tunakaribia kumaliza mwaka wa kwanza.

Kuna kitu nimesahau. Wakati niko first year nilianza mahusiano na binti ambaye alikua anasoma Moshi (MUCCOBs). Tulikuana kupitia instagram.
Kwa wakati huo nilikua situmii facebook sana na nilishahamia insta, Instagram pia nilikua na fan base kubwa sana. Nakumbuka nikiwa first year nilikua na 10k+ followers.

TUTAENDELEA

Huyu Binti wa MUCCOBs ana story yake mbeleni huko
 
SEHEMU YA KUMI (10)
Tulipoishia…

Nilikamilisha taratibu za malipo yote chuoni, hostel na kila kitu kilikua poa na nilikua tayari sasa kuanza maisha mapya ya chuo.
Mzee alinipa pesa kidogo pia.

Tuendelee sasa

Maisha ya chuo yaliendelea na ndani ya wiki mbili majibu ya waliopata mkopo yalitoka.
MUNGU mkubwa nilikua kwenye list ya waliopata mkopo na nilikua nna asilimia 90+ nilifurahi sana hii siku.

Sasa nakumbuka mzee alinitext akasema kama niko free niende home kuna harusi ambayo amechanga na ana kadi 2, so moja ntaenda mimi na bro (Bro alikua likizo wakati huo na alikuja mwanza kusalimia, likizo za watu wanaosoma medical zilikua kidogo tofauti na sisi wengine)

Nilienda home kwa bashasha na mbwembwe sana maana niliona kitendo cha kupata mkopo basi maisha yangu chuo yatakua poa.
Tulijiandaa tukaenda harusini ilikua mwanza town pale, ukumbi ulikua ghorofani ila sikumbuki vizuri unaitwaje.

Tumeingia ukumbini mi hata maharusi siwajui ila nilishangaa kukutana na watu wengi tuliosoma wote primary na baadhi secondary kule mwanza (Rejea epsode 1& 2)
Nilifurahi sana kuonana na sura zile na story zilikua nyingi ikiwemo now unafanya nn, mi jibu langu lilikua straight, niko SAUT nasoma.

Tulipata meza katikati ya ukumbi na tulikaa hapo mimi na bro pamoja ma watu wengine nisiowafahamu (mzee hakua na muda na sisi, alikua na marafiki zake)
Ile furaha ya kupata mkopo ikanituma ninywe pombe. Sasa hadi wakati huu sikua nime-master unywaji wa pombe maana nilikua nakunywa mara chache sana.
Hii siku nilikunywa pombe sana na nilichanganya hadi inafika muda wa chakula mimi nilikua hoi na bro alitambia hilo. Basi akanifatia chakula, kitendo cha chakula kufika mezani tu mimi nilitapika sana baada ya kusikia harufu ya msosi na nikazima tena kama kule bukoba.

Kaka yangu alihangaika sana na mimi akanipa maji mengi, sasa issue ilikua kunitoa pale ukumbini hadi chini. Sikua na nguvu kabisa na yeye asingeweza peke yake. Mzee alishaona lile tukio na aliamua kulinda heshima yake, hakusogea hata nilipokua, alimtext bro kuwa anipeleke home. Bro alimpigia jirani yetu mmoja akaja na boda chap wakanipeleka home. Huko home hali haikua nzuri kwani niliendelea kutapika sana na baadae nikapitiwa na usingizi.
Asubuhi bro alienda kununua zile IV Fluids (Drip) akaniwekea canula mkononi then drip akatundika dirishani nikaanza kula dozi (bro alikua mwaka wa 3 wakati huo so alikua amemaster vitu kadhaa vya medical)
Mzee hakusema kitu kuhusu mimi kulewa na asubuhi alijiandaa akaenda kwenye shughuli zake.
Baada kama ya masaa manne nilikua naweza kupiga story na watu kabisa pale home ila nilikua weak bado.
Sasa siku hiyo ilikua ndo FIESTA Mwanza na ilikua inafanyikia CCM Kirumba pale.

Bro na marafiki zake kadhaa niliwasikia wakipanga kwenda FIESTA, Nikakumbuka kuna rafiki zangu wawili kule chuo walisema twende FIESTA. Sasa ikabidi nimwambie bro kuwa tutaenda wote jioni ila tukifika huko mi ntaachana nae na ntaungana na marafiki zangu. Bro alinikazia nikaona nikae kimya. Akaniwekea drip ya mwisho kisha sikujua wameondoka vipi, alinikwepa 😅.

Saa moja jioni nilikua fit na nikaanza kucheck na marafiki zangu wa chuo, walisema kuwa wataenda FIESTA na mimi nakawaambia tutakutana uwanjani. Saa tatu kamili nilikua nimejiandaa tayari na chap nikaondoka zangu ila sikua fit sana.

Nilifika CCM Kirumba nikalipa kingilio huyoo nikaingia ndani, katika zunguka zunguka nilikuatana na bro na marafiki zake walivyoniona wakacheka sana kisha bro akasema wao wana ratiba zao na mimi niendelee na zangu.
Nilikutana na marafiki zangu mle ndani saa nne na tukaanza kuvibe ila mi nilikua nakunywa maji tu.
Baada kama masaa mawili niliona kabisaa sina nguvu hata kusimama kuangalia wasanii ikawa issue. Nikaaga pale huyooo nikapanda boda hadi home nikalala.

Kesho jioni nilirudi chuo kuendelea na maisha ya kusoma.

Sasa wakati huu wote sikua na ukaribu sana na Mama mchungaji maana nilikua na mambo mengi lakini pia yule Clara alikua ashaanza kuwasiliana sana na mimi.
Clara ni binti aliyenipenda sana sanaaa na kwakweli mi kwa wakati huo sikua nampa muda sana.

Mama mchungaji aliendelea kupitia changamoto za pale anapokaa lakini Mungu ni mwema alifanikiwa kumaliza masomo yake ya certificate. Kwenye kuomba chuo ili asime diploma alichagua kimoja cha Mkoani Mara na chuo cha hapo Iringa kama sikosei (nnachokumbuka alichagua vyuo viwili) lengo la kuchagua mkoa wa Mara ilikua alitaka kuwa karibu na mimi. Mara na mwanza sio mbali sana hivyo aliamini tungekua tukionana sana.
Mimi nilimuunga mkono lakini niwe muwazi sikua namjali tena kama mwanzoni.

Hapo nilishaanza kuonana na Clara mara kadhaa na kushiriki nae tendo.
Mwaka wa kwanza wote sikutaka kujihusisha na mahusiano chuoni. Nilikua nakumbuka namna B.mkubwa alinishihi sana kuhusu wanawake chuo. (Nakumbuka alisema ukiona umeshindwa kujizui tumia kondomu)
Hivyo mwaka wa kwanza nilikua nikipoteza muda sana na Clara

Huyu Clara nilikua napajua kwao na kwetu wanamjua vizuri tu. Kuna wakati nilikua nikienda kumtembelea mzee home namshtua Clara anakuja na nilishafanya nae tendo pale pale home🤦🏿‍♂️

Majibu ya mama mchungaji yalitoka na alikua amechaguliwa kujiunga na chuo cha Mara kule. Hivyo alitakiwa akasome diploma yake huko.
Kwa upande wangu nilikua nishakua na ujanja ujanja wa chuo, nishajua kuvaa kama mwanachuo na nilishanunua smartphone HUAWEI Y300 kama sikosei.

Siku zilienda na tulikua tunakaribia kumaliza mwaka wa kwanza.

Kuna kitu nimesahau. Wakati niko first year nilianza mahusiano na binti ambaye alikua anasoma Moshi (MUCCOBs). Tulikuana kupitia instagram.
Kwa wakati huo nilikua situmii facebook sana na nilishahamia insta, Instagram pia nilikua na fan base kubwa sana. Nakumbuka nikiwa first year nilikua na 10k+ followers.

TUTAENDELEA

Huyu Binti wa MUCCOBs ana story yake mbeleni huko
Shusha vitu
 
SEHEMU YA NNE (4)

Tulipoishia…

Yale matokeo yakafifisha ndoto zangu za kwenda Science jumla…

Tuendelee Sasa…

Familia ya pale home kwa aunt ilikua poa tu maana hakukua na challenge sana na nisingependa kugusia part hii maana sio muhimu sana.

Baada ya matokeo yale ratiba ilibadilika, ilikua hata nikitoka tuition lazima home nisome usiku, uncle (mume wa aunt) alikua lazima aje usiku kuchungulia room kwetu kama tumeamka kusoma (Kuna mtoto wa mwisho wa aunt mwingine alikua pale ma alikua primary bado ndo tulikua tunapeana kampani kusoma)

Kwa upande mwingine maisha ya kiroho pia yalikua yanakaziwa pale, kila jumapili lazima kwenda kanisani, ilikua ni lazima so nilinyooka na kuwa kijana mzuri tu, sikua na makundi kama Mwanza kule.

Turudi kwa Jane kwanza… Wakati wote ambao niko kwenye mahusiano na Jane sikua nimewahi kufanya chochote. Kuna siku tulipanga kwamba weekend twende mlimani huko ( kulikua na mlima flani una majani na miti miti na hakukuwa na nyumba karibu na maeneo yale) ukipanda huko juu unaiona Bukoba vizuri kabisaaa, mlima uko maeneo ya Buyekera karibu na shule ya msingi Buyekera. Kwa watu walioishi Bukoba mjini wanapafahamu ingawa kwa sasa mlima huo una nyumba kibao tu.
Tuliplan twende kule tukashiriki tendo wakati huo mimi ndo mara ya kwanza na mwenzangu yeye alikua ashapiga show kadhaa huko nyuma.
Maisha yaliendelea na weekend ilifika tukaenda zetu juu huko mi nilibeba maji ya kunywa tu. Tulikutana mahali na tukaanza safari.
Baafa ya muda kama 20 min tulikua kule juu tukajichimbia mahali ma story ziliendelea huku nisijue naanzia wapi.
Kufupisha, tulishiriki tendo na ndo ilikua mara yangu ya kwanza. Siwezi sema nilienjoy sana maana sikua najua mambo mengi na niliishia bao la kwanza wala sikutaka kuendelea.

Sasa baada ya yote Jane alizidi kunipenda na mimi nilikua nampenda sana kwakweli. Kule shuleni walikua wanasema tu mi napata story ila hatukuwahi kuweka wazi mapenzi yetu mbele za watu. Baadhi ya washikaji walikua na chuki na mimi kisa Jane. Jane alikua na mwili mkubwa kidogo kunizidi na alionekana kunizidi kama mwaka hivi (nilijua baadae kuwa ananizidi)
Sasa wakati penzi likikolea Jane alikua na Kaka yake ambaye nilikua tu namwona na kwa kipindi kile jamaa alikua anakula moshi (anavuta Bangi) yule Kaka yake sikuwahi kuwa karibu nae ila nilikua najua anamtaka mtoto wa aunt yule aliyefanya nijuane na Jane.
Siku natoka tuition mida ya saa 12 jioni nilikutana na kaka yake akiwa na kundi lake na wanilisimamisha nilikua naendesha baiskeli kwenda home. Jamaa alinipiga beat na kusema natoka na dada yake, atanitafuta, pale asingeweza kufanya kitu kwani tulikua road.
Asee niliogopa sana nikaenda home straight kwa Dada (yule mtoto wa aunt tumwite Tiva)
Tiva alimind sana akanambia twende, kufika kule alimfokea sana jamaa na jamaa akasema hajasema kitu kibaya kwangu na hawezi kunigusa maana sijamkosea kitu.

Kun siku tuko shuleni, muda wa break Jane alikua ananifata kwenye dawati langu na kuongozana hadi jikoni kupata chai (BUKOBA SEC ilikua na utaratibu wa kugawa maandazi na chai kwa kila mwanafunzi na ilikua buree, utaratibu uliwekwa kwa members yaani wanafunzi mnakua na makundi ya watu 12 na kiongozi ndo anafata maandazi na chai then anawagawia)
Sasa huu utaratibu sikua nimeuzoea sababu kule Mwanza hamna mambo hayo, pili sikua nimezoea sana kuongea na watu, tatu kulikua na vurugu flani hivi. Jane ndo mtu pakee alikua ananichukulia maandazi na kuniletea kwenye Table yetu pale canteen then tunakula. Siku nyingine nilikua siendi kabisa Canteen. Sasa kuna siku nilimwambia siendi yeye akatangulia then baadae akili ikanambia niende nikanunue Karanga za bubu (zilikua maarufu sana na muuzaji alikua bubu). Wakati nanunua karanga nikamwona Jane yuko Posta (Bukoba sec iko karibu na ofisi za posta) anaongea na jamaa hivi ambaye sio mwanafunzi. Wivu ukanijaa na nikachukia sana na aliniona.
Nikarudi class na sikusema kitu, jioni muda wa kutoka akaja kunichua kwa desk yangu tuindoke nikamwambia asinifate tena na asinizoee, nilikua na ujinga mwingi asee.

Jane aliondoka hakutaka kudraw atention yoyote pale maana wengi walikua hawajui kama tunadate.
Jioni alikuja home kuniulizia na akaambiwa niko Tuition. Home hawakua na wasiwasi wanajua tunasoma wote. Usiku akaja tena na nikamkazia nikasema sitaki mahusiano tena. Aliniomba msamaha na kunidanganya yakaisha.
Nakumbuka Jane alikua akiniletea pesa na vijizawadi sana.

Sasa kumbe sakata la yule kaka yake Jane kusema atanitafuta lilikua limetengenezwa na jamaa flani alikua anamtaka sana Jane ila Jane anakaza, jamaa aligundua Jane ana mahusiano na mimi.

Nakumbuka hiyo siku nikua natoka tuition, mida ya saa moja jioni giza tayari limeingia, nikiwa njiani kabisa kufika home, ile sehemu yenye shamba la miwa ambako nilikiss mara ya kwanza na jane. Nilikutana na jamaa wawili wakanisimamisha, wakati nashuka kwenye baiskeli niwasikilize asee nilipigwa ngumi moja ya uso hadi chini… Sikujua napambana nao vipi nikajikuta nimebaki chini pale kama nimezima ili wasiendelee maana wangenipasua.. Jamaa wakakimbia (mmoja alikua yule anayemtaka Jane na nilikua namjua sababu Jane aliwahi nionyesha)

Walivyokimbia nikaamka nduki nikaenda nyumbani na nilikua na uoga sana ikabidi nimwambie Aunt kuwa watu flani wamenivamia na kunipiga kisa Jane (nilikua na utoto mwingi). Aunt alichukia na akasema twende kwao Jane ila tupite kwa balozi kwanza kutoa taarifa then tukaenda kwao na Jane

Itaendelea…
Stori yako hata haisisimui.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom