Maisha yangu nimeyaharibu mwenyewe

SEHEMU YA SABA (7)

Tulipoishia…


Asubuhi niliondoka na Clara alisubiri hadi bus liondoke ndo akaondoka ila alikua na maumivu makali mno na hata tembea yake haikua kawaida.
Wakati niko njiani tulikua tukichat na alinijulisha kuwa anaumwa sana, amepata hadi homa. Nilimpa pole nyingi na kumwambia ajikaze home wasijue.

Kwa upande wa Jane baada ya kumaliza form 4 alienda Dar kwa mpenzi wake baadae akaenda mwanza kwa dada yake (niliambiwa na mwenzake) lakini taarifa niliyokuwa nayo wakati naenda Advance ni kuwa Jane tayari ana mimba kubwa tu.

Tunaendelea….


Nilifika dar majira ya saa tano usiku, na hii ndo ilikua mara yangu ya kwanza kuja Dar. Aunt alituma mtu aje kunipokea na joto ndo lilinipokea vizuri.

Aunt wa Dar ana maisha yake mazuri tu na sitotaka kuongelea chochote kuhusu maisha ya kwa Aunt ila kwa ufupi sana ni maisha poa na kila mtu na time zake, mtakutana jioni muda wa kuangalia habari na kula labda

Kesho yake kuna Dada yangu alinipeleka Mwenge na Kariakoo kununua vitu vya Shule. Nilikaa Dar kama siku 4 then safari ya Mbey ikaanza.
Wakati natoka Dar nilikua na kila kitu cha shuleni. Aunt wa Dar alininunulia ( aunt wa Dar tumwite B. Mkubwa ili kutofautisha na wa Bukoba)
Account yangu ya CRDB iliwekwa laki 2 na B. mkubwa kama Pocket money ya shule then nikapewa nauli na pesa ya kula njiani. Nilinunuliwa counter Book 12, vitabu 6 na kila hitaji nilipewa. Mzee mwanza pia alinipa hela ila nilikula bata yote nilivyofika Dar ikiwemo kununua nguo mpya.

Safari ya Mbeya ilikua safi tu na nilifika Mbeya Tukuyu majira ya saa nne na nusu hivi usiku. Wakati niko njiani kuna mbaba nilikaa nae alikua ni doctor huko Kyela na alitokea kunikubali sana na tulibadilishana namba.

Changamoto ilikuja pale nilipofika Tukuyu na kujikuta nimebaki na Cash kama elfu 17 tu. Sasa nikauliza bank iko wapi, Dreva tax alinijibu “huku hakuna CRDB, kuwa linakuja gari (Mobile Bank) sijui kama niko sahihi linavyoitwa. Hilo gari huwa linakuja siku ya jumatatu tu na linatoa huduma na kuondoka”. Asee nilichanganyikiwa na sikuwa na mwenyeji yoyote Mbeya kwa wakati huo. Niliomba dreva Tax anipeleke lodge yoyote ya bei ndogo. Jamaa alinifanyia uhuni, Lodge ilikua sehemu ya kutembea kwa dak 2 tu ila jamaa akanizungusha njia ya mbali na akanipela hapo Lodge nikampa buku 3. Pale Lodge nililipa elfu 10 nikalala huku nikiwaza asubuhi naendaje Mbeya mjini maana nilikua mgeni kabisa na mfukoni nna kama elfu 4 tu.

Niliamka asubuhi nikajiandaa then nikaenda mapokezi nikamwomba jamaa aniangalizie mizigo yangu.
Nilipanda costa za Tukuyu - Mbeya nauli ilikua buku 3 kama sikosei. Safari ikaanza nami macho yangu yote yalikua barabarani nikijisemea ntakapoona ATM ya CRDB basi nashukua.
Nilishuka Mwanjelwa pale baada ya kuona ATM then nikatoa pesa kama laki hivi. Nilinunua godoro, blanketi na koti jeusi. Ile shule tulikua tunavaa full black… Yani shati white, suruali black na koti Black… suit kabisa yani.

Nikarudi Tukuyu na kubeba vitu vyangu tayari kwenda shule. Yule dreva tax nilichukua namba yake na tulikuja kuwa washkaji baadae. Alinipeleka hadi stand ya kwenda huko ndani ndani (Mbambo, Itete hadi shuleni penyewe)
Sasa pake stand nilikutana na wanafunzi kibao wanaoenda shuleni ila cha kushangaza usafiri ulikua Canter na sio mabasi… Yani mnaning’inia huko juu kwenye canter.. wanawake ndo wanakaa chini. Asee niliishiwa nguvu baada ya kusikia hivyo.
Canter inajaza balaa na mizigo ni mingi mnoo kwani watu huja Tukuyu kununua mahitaji mengi na wengi ni wafanyabiashara kule kijijini.

Safari ilianza kama baada ya masaa mawili hivi na wanafunzi tulikua tunapiga story nyingi mnoo na swali kubwa ilikua ni kuulizana we umetokea wapi. Peke yangu ndo nilikua natoka Bukoba.
Ile safari ilikua ya mateso sana. Barabara ni vumbi, madaraja ya mbao alafu barabara ina milima na kona balaa (watu wa Mbeya hususani Tukuyu wananielewa vizuri hapa)

Ilikua Gari ikilalia upande wetu nasali sana maana ukiachia zile bomba ndo uko chini hivyo
Nilianza kujuta kwanini sikusoma Bukoba tu. Baada ya masaa matatu na nusu hivi tulifika shuleni… Asee nilihisi kuna kitu kimenikaba kooni kama nataka kulia kama nimebanwa (hii hali mnaijua wengi) kwa ufupi ningekua mtoto ningelia
Shule ilikua mwisho kabisa. Yani kata ya mwisho kabisaa baada ya hapo kuna Mlima Living stone so hakuna namna utaenda kokote.

Tulipokelewa shuleni tukaonyeshwa mabweni then tukaenda kula mtaani siku hiyo maana tulifika watu washapewa chakula cha jioni shuleni pale.
Nilifanikiwa kupata marafiki wengi na maisha ya kuishi mbali na wazazi yakaanza rasmi


Tuishie hapa kwa leo

See you kesho
Najaribu kufikiria shule iliyo chini ya safu ya milima ya Livingston ni Luteba Mwakaleli
 
Nakupa elimu ndogo kabisa, Ni baba yenu ndie alikuwa anatafuta hela za kuwalipia ada shuleni, nguo, chakula, n.k. mama yenu alikuwa anapewa ila mkimuona anavyowalipia / kuwapa mnadhani ni zake.

Nani kama mama ni misemo ya watoto / vijana ambao bado hawana familia zao kujua mfumo kamili wa jinsi mambo yanavyokwenda
Sikupingi tunajionea sasa tulivyokua na familia..na always huwa nawaambia watt ni baba ndo katoa ada..ni baba ndo kawanunulia hiki mumwambie asante wasije baadae waone mimi ndo nafanya kila kitu..ni kitu muhimu hii...
 
Yes bro, wana moyo wa kipekee sana
@Adriel Vin shukuru Mungu mkuu mlipata ndugu wema waliowavusha salama baada ya msiba wa mama yenu mzazi,aidha ulisomea Bukoba sec shule maarufu na yenye totozi nyingi sana pale Bukoba,sisi wazee wa Kahororo tulikua tunawamezea mate sana totozi zahapo kwenu hasa wakati wa joint mass,na makanisani huko.
 
Habari wanaJF, bila shaka kila anayesoma hapa ni mzima na afya, na kama sio Mungu akupe lililo hitaji la moyo wako

Mimi ni kijana wa miaka 30. Nimezaliwa mkoa wa mwanza, nimepata elimu yangu ya msingi huko mkoani mwanza. Nilimaliza kwa ufaulu wa kawaida lakini nilifanikiwa kuchaguliwa na kuendelea na elimu ya sekondari huko huko mkoani mwanza.

Mimi ni mtoto wa 2 kati ya 3 ambao tumelelewa kwa pamoja, japo nna dada zangu wengine wawili ambao hatukukua pamoja muda mwingi (Baba alikua na watoto wawili kabla hajaoa) so jumla yetu tuko watano (5)

Maisha ya nyumbani yalikua ya kawaida tu sio matajiri na sio masikini. Na nimekua kwenye malezi ya maadili ya kiafrika kabisa.

To cut it short

Kwenye kukua kwetu hatukuwa tukiomba hela kwa baba maana tulikua tunamwogopa, mzee alikua mkali balaa so kila kitu tulikua tukiongea na mama. Mama alikua mtu mwenye upendo sana kwa wanae na alipambana kwa namna yoyote kuhakikisha watoto wake tunasoma na kuwa vijana bora. Pesa ya kula shule, nauli, madaftari na kila kitu tulikua tukipewa na mama. Sio kwamba Baba hakua anatoa chochote kabisa lakini najaribu tu kuonyesha kwamba Mama ndo alikua rafiki yetu sana kuliko mzee. Japo fimbo na vibao vingi tumepigwa na mama kuliko mzee.

Nilipomaliza darasa sa saba, Kaka yangu alikua form 2 kwa wakati huo na alikua akisoma shule ya private. Kwa upande wangu matokeo ya darasa la saba sikuweza kuchaguliwa first selection. (Sikua na alama za kutosha) kama nilivyosema hapo juu nilifaulu kawaida ntafafanua mbele.

Mama alinipeleka shule ya private ambayo kaka yangu anasoma kwa wakati huo na nilifanya interview na kupewa majibu ndani ya siku 2 kuwa nimefaulu naweza kujiunga na shule hiyo ili kuendelea na elimu ya sekondari.

Nakumbuka baada ya mwezi hivi (sina uhakika sana) second selection ilitoka na nilikua nimechaguliwa shule flani iko wilaya ya ilemela (Jina nahifadhi). Ilikua ni shule mpya kabisaa kwa kipindi hicho zilkua na jina maarufu zikiitwa shule za kata. So nilichaguliwa shule ya kata.

Mama alisema niendelee kusoma kwenye shule hiyo ya private lakini niliona kama hayuko sahihi maana hali yake ya uchumi haikua nzuri hata ada najua alikopa. Ila kwa umri ule nisingeweza kumshauri kitu zaidi ya kusema sawa mama. Na maisha yaliendelea.

Mama yangu alikua mtu wa upendo sana na mchakarikaji. Niseme tu nilikua nampenda sana mama na nilikua ni yule mtoto wa mama (mamaz boy). Ilipita wiki kadhaa na mama alianza kuumwa serious. Alikua akilalamika siku za nyuma lakini wakati huu alisisitiza kuwa hajisikii vizuri hivyo alituaga na kuondoka kwenda hospital kwa matibabu.

Aliondoka majira kama ya saa sita nakumbuka na aliahidi angerejea baada ya matibabu.
Kuna hospital moja ipo Mwanza kwa kipindi hicho ilikua ikiitwa Mission, iko maeneo ya Ghana kama sikosei, sina hakika kama bado iko pale hadi leo.

Taarifa za mama kuumwa hazikua nzuri kwangu maana Mama hakufanikiwa kurejea nyumbani siku hiyo.
Mimi (Nijiite Amani…Sio jina halisi) nilikua yule mtoto ambaye hata mama akitoka ikifika saa 3 usiku hajarudi basi wasiwasi na uoga ulikua unakua mwingi.

Sasa hii siku mama hakurudi kabisa na nilikua na wasiwasi sana hadi hapo mama mdogo alipokuja home majira ya jioni ya kutupa habari kuwa mama amelazwa katika hospital hiyo ya Mission. Kama kumbukumbu zangu ziko vizuri ilikua ni weekend.

Maisha yaliendelea na tulikua tukienda kumwona mama. Jumatatu tulienda shule kama kawaida, nilikua nikiondoka na kaka yangu kwani alikua ananizidi madarasa 2 hivyo alikua ananiongoza vyema tu. Kaka yangu aliwahi sana kujitambua hivyo hakuwa msumbufu sana kwa mama kama mimi.

Mimi nilikua hata nikitoka shule sina muda wa kusoma, ni michezo hadi usiku so hata maendeleo yangu shule hayakua mazuri sana ukiringanisha na kaka yangu.

Mama aliendelea kupatiwa matibabu kama siku 3 hivi lakini hakuonyesha nafuu hivyo alipewa rufaa kwenda Hospital ya Bugando.

Nilikua na ratiba kila nikitoka shule naunga moja kwa moja hadi Bugando kwenda kumsalimia mama. Nilikua natoka shule saa nane na nusu hvyo hadi kufika saa kumi muda wa kuona nilikua nimeshafika pale Hospital.

Kuna muda nilikua nazuiliwa na walinzi maana kwa kipindi hicho walikua na utaratibu wa kuzuia watoto kwenda kuona wagonjwa. Sasa mimi na umbo langu dogo dogo nilikua naonekana mdogo so kuna muda sikua nafanikiwa kuingia hadi niwe na mtu mzima

Hali ya mama haikua nzuri kwakweli maana baada ya kama siku kumi hivi, Nakumbuka hiyo siku nilienda kumwona mama nikakuta amewekewa mashine ya Oxygen, ndo ilikua mara yangu ya kwanza naona mtu kawekewa ile mirija puani.

Nakumbuka nilianza kulia pale na mama mdogo alinitoa nje maana nilikua nalia alafu mama ananiangali wakati huo alikua hawezi hata kutoa sauti ukaisikia so alikua ananiangalia na nilikua naona kabisa anaumia kuona nalia.

Tulirudi nyumbani siku hiyo na usingizi ulikua wa shida sana nawaza mama amekuwaje. Hali ya home pia haikua nzuri kwani kwa kipindi chote hicho mama hakuwepo nyumbani.

Pale nyumbani tulikua na kiduka ambacho kilikua kinaendeshwa na mama na ndipo hapo tulikua tukipata hela ya nauli pamoja na ile ya kula shule. So wakati wote ambao mama hakuwepo hata mapato dukani yalipungua kwani bidhaa nyingi zilikua zimeisha usimamizi hakua mzuri.

Ni baada ya kama siku 2 tu nikiwa nimetoka hospital kumwona mama. Wakati huo sikua naruhusiwa tena kwenda kumwona kutokana na kile kitendo cha kulia.

Hii siku nilitoka shule nikaenda moja kwa moja home lakini ilipofika jioni baadhi wa watu waliotoka hospital walinipa taarifa kuwa hali ya mama bado si nzuri.

Usiku wake baba alipigiwa simu akiambiwa mama hali yake ni mbaya na alienda moja kwa moja hospital.
Baaba ya masaa kama mawili nilishtuka kwa kelele za vilio kutoka kwa mama zangu wadogo.
Mama alikua amefariki tayari

NITAENDELEA… Leo Leo


Usiku wake baba alipigiwa simu akiambiwa mama hali yake ni mbaya na alienda moja kwa moja hospital.
Baaba ya masaa kama mawili nilishtuka kwa kelele za vilio kutoka kwa mama zangu wadogo.
Mama alikua amefariki tayari
Polee Sana..

I can Feel your pain Through Narrative Words..
Polee sana..
Umenikumbusha Nilivompoteza baba Yangu..
Maumivu ya kupoteza mzazi ambaye pia ni Rafiki yako na anayekuelewa Nayajua vizuri..

Maumivu hayo yalinichukua Muda sana kukaa In Normal States. Sikuwa naamini Kuwa Dunia ni Kitu halisia nilihisi Ni Illusion tu..

Nilikosa huruma,Nilipoteza Muelekeo Ilinichukua Miaka minne Kurealise kwamba Kila kitu Kinapangwa na kinatokea kwa Sababu..

Through nakukumbuka Mzee wangu ila umenifunza Vingi sana Baada ya kifo chako..
Uendelee kupumzika kwa Amani
 
SEHEMU YA SABA (7)

Tulipoishia…


Asubuhi niliondoka na Clara alisubiri hadi bus liondoke ndo akaondoka ila alikua na maumivu makali mno na hata tembea yake haikua kawaida.
Wakati niko njiani tulikua tukichat na alinijulisha kuwa anaumwa sana, amepata hadi homa. Nilimpa pole nyingi na kumwambia ajikaze home wasijue.

Kwa upande wa Jane baada ya kumaliza form 4 alienda Dar kwa mpenzi wake baadae akaenda mwanza kwa dada yake (niliambiwa na mwenzake) lakini taarifa niliyokuwa nayo wakati naenda Advance ni kuwa Jane tayari ana mimba kubwa tu.

Tunaendelea….


Nilifika dar majira ya saa tano usiku, na hii ndo ilikua mara yangu ya kwanza kuja Dar. Aunt alituma mtu aje kunipokea na joto ndo lilinipokea vizuri.

Aunt wa Dar ana maisha yake mazuri tu na sitotaka kuongelea chochote kuhusu maisha ya kwa Aunt ila kwa ufupi sana ni maisha poa na kila mtu na time zake, mtakutana jioni muda wa kuangalia habari na kula labda

Kesho yake kuna Dada yangu alinipeleka Mwenge na Kariakoo kununua vitu vya Shule. Nilikaa Dar kama siku 4 then safari ya Mbey ikaanza.
Wakati natoka Dar nilikua na kila kitu cha shuleni. Aunt wa Dar alininunulia ( aunt wa Dar tumwite B. Mkubwa ili kutofautisha na wa Bukoba)
Account yangu ya CRDB iliwekwa laki 2 na B. mkubwa kama Pocket money ya shule then nikapewa nauli na pesa ya kula njiani. Nilinunuliwa counter Book 12, vitabu 6 na kila hitaji nilipewa. Mzee mwanza pia alinipa hela ila nilikula bata yote nilivyofika Dar ikiwemo kununua nguo mpya.

Safari ya Mbeya ilikua safi tu na nilifika Mbeya Tukuyu majira ya saa nne na nusu hivi usiku. Wakati niko njiani kuna mbaba nilikaa nae alikua ni doctor huko Kyela na alitokea kunikubali sana na tulibadilishana namba.

Changamoto ilikuja pale nilipofika Tukuyu na kujikuta nimebaki na Cash kama elfu 17 tu. Sasa nikauliza bank iko wapi, Dreva tax alinijibu “huku hakuna CRDB, kuwa linakuja gari (Mobile Bank) sijui kama niko sahihi linavyoitwa. Hilo gari huwa linakuja siku ya jumatatu tu na linatoa huduma na kuondoka”. Asee nilichanganyikiwa na sikuwa na mwenyeji yoyote Mbeya kwa wakati huo. Niliomba dreva Tax anipeleke lodge yoyote ya bei ndogo. Jamaa alinifanyia uhuni, Lodge ilikua sehemu ya kutembea kwa dak 2 tu ila jamaa akanizungusha njia ya mbali na akanipela hapo Lodge nikampa buku 3. Pale Lodge nililipa elfu 10 nikalala huku nikiwaza asubuhi naendaje Mbeya mjini maana nilikua mgeni kabisa na mfukoni nna kama elfu 4 tu.

Niliamka asubuhi nikajiandaa then nikaenda mapokezi nikamwomba jamaa aniangalizie mizigo yangu.
Nilipanda costa za Tukuyu - Mbeya nauli ilikua buku 3 kama sikosei. Safari ikaanza nami macho yangu yote yalikua barabarani nikijisemea ntakapoona ATM ya CRDB basi nashukua.
Nilishuka Mwanjelwa pale baada ya kuona ATM then nikatoa pesa kama laki hivi. Nilinunua godoro, blanketi na koti jeusi. Ile shule tulikua tunavaa full black… Yani shati white, suruali black na koti Black… suit kabisa yani.

Nikarudi Tukuyu na kubeba vitu vyangu tayari kwenda shule. Yule dreva tax nilichukua namba yake na tulikuja kuwa washkaji baadae. Alinipeleka hadi stand ya kwenda huko ndani ndani (Mbambo, Itete hadi shuleni penyewe)
Sasa pake stand nilikutana na wanafunzi kibao wanaoenda shuleni ila cha kushangaza usafiri ulikua Canter na sio mabasi… Yani mnaning’inia huko juu kwenye canter.. wanawake ndo wanakaa chini. Asee niliishiwa nguvu baada ya kusikia hivyo.
Canter inajaza balaa na mizigo ni mingi mnoo kwani watu huja Tukuyu kununua mahitaji mengi na wengi ni wafanyabiashara kule kijijini.

Safari ilianza kama baada ya masaa mawili hivi na wanafunzi tulikua tunapiga story nyingi mnoo na swali kubwa ilikua ni kuulizana we umetokea wapi. Peke yangu ndo nilikua natoka Bukoba.
Ile safari ilikua ya mateso sana. Barabara ni vumbi, madaraja ya mbao alafu barabara ina milima na kona balaa (watu wa Mbeya hususani Tukuyu wananielewa vizuri hapa)

Ilikua Gari ikilalia upande wetu nasali sana maana ukiachia zile bomba ndo uko chini hivyo
Nilianza kujuta kwanini sikusoma Bukoba tu. Baada ya masaa matatu na nusu hivi tulifika shuleni… Asee nilihisi kuna kitu kimenikaba kooni kama nataka kulia kama nimebanwa (hii hali mnaijua wengi) kwa ufupi ningekua mtoto ningelia
Shule ilikua mwisho kabisa. Yani kata ya mwisho kabisaa baada ya hapo kuna Mlima Living stone so hakuna namna utaenda kokote.

Tulipokelewa shuleni tukaonyeshwa mabweni then tukaenda kula mtaani siku hiyo maana tulifika watu washapewa chakula cha jioni shuleni pale.
Nilifanikiwa kupata marafiki wengi na maisha ya kuishi mbali na wazazi yakaanza rasmi


Tuishie hapa kwa leo

See you kesho

Ulipotaja Livingstone Mountain nikakumbuka Shule ya Matema Beach.
Nimesoma hapo Advance nusu muhula
 
SEHEMU YA SABA (7)

Tulipoishia…


Asubuhi niliondoka na Clara alisubiri hadi bus liondoke ndo akaondoka ila alikua na maumivu makali mno na hata tembea yake haikua kawaida.
Wakati niko njiani tulikua tukichat na alinijulisha kuwa anaumwa sana, amepata hadi homa. Nilimpa pole nyingi na kumwambia ajikaze home wasijue.

Kwa upande wa Jane baada ya kumaliza form 4 alienda Dar kwa mpenzi wake baadae akaenda mwanza kwa dada yake (niliambiwa na mwenzake) lakini taarifa niliyokuwa nayo wakati naenda Advance ni kuwa Jane tayari ana mimba kubwa tu.

Tunaendelea….


Nilifika dar majira ya saa tano usiku, na hii ndo ilikua mara yangu ya kwanza kuja Dar. Aunt alituma mtu aje kunipokea na joto ndo lilinipokea vizuri.

Aunt wa Dar ana maisha yake mazuri tu na sitotaka kuongelea chochote kuhusu maisha ya kwa Aunt ila kwa ufupi sana ni maisha poa na kila mtu na time zake, mtakutana jioni muda wa kuangalia habari na kula labda

Kesho yake kuna Dada yangu alinipeleka Mwenge na Kariakoo kununua vitu vya Shule. Nilikaa Dar kama siku 4 then safari ya Mbey ikaanza.
Wakati natoka Dar nilikua na kila kitu cha shuleni. Aunt wa Dar alininunulia ( aunt wa Dar tumwite B. Mkubwa ili kutofautisha na wa Bukoba)
Account yangu ya CRDB iliwekwa laki 2 na B. mkubwa kama Pocket money ya shule then nikapewa nauli na pesa ya kula njiani. Nilinunuliwa counter Book 12, vitabu 6 na kila hitaji nilipewa. Mzee mwanza pia alinipa hela ila nilikula bata yote nilivyofika Dar ikiwemo kununua nguo mpya.

Safari ya Mbeya ilikua safi tu na nilifika Mbeya Tukuyu majira ya saa nne na nusu hivi usiku. Wakati niko njiani kuna mbaba nilikaa nae alikua ni doctor huko Kyela na alitokea kunikubali sana na tulibadilishana namba.

Changamoto ilikuja pale nilipofika Tukuyu na kujikuta nimebaki na Cash kama elfu 17 tu. Sasa nikauliza bank iko wapi, Dreva tax alinijibu “huku hakuna CRDB, kuwa linakuja gari (Mobile Bank) sijui kama niko sahihi linavyoitwa. Hilo gari huwa linakuja siku ya jumatatu tu na linatoa huduma na kuondoka”. Asee nilichanganyikiwa na sikuwa na mwenyeji yoyote Mbeya kwa wakati huo. Niliomba dreva Tax anipeleke lodge yoyote ya bei ndogo. Jamaa alinifanyia uhuni, Lodge ilikua sehemu ya kutembea kwa dak 2 tu ila jamaa akanizungusha njia ya mbali na akanipela hapo Lodge nikampa buku 3. Pale Lodge nililipa elfu 10 nikalala huku nikiwaza asubuhi naendaje Mbeya mjini maana nilikua mgeni kabisa na mfukoni nna kama elfu 4 tu.

Niliamka asubuhi nikajiandaa then nikaenda mapokezi nikamwomba jamaa aniangalizie mizigo yangu.
Nilipanda costa za Tukuyu - Mbeya nauli ilikua buku 3 kama sikosei. Safari ikaanza nami macho yangu yote yalikua barabarani nikijisemea ntakapoona ATM ya CRDB basi nashukua.
Nilishuka Mwanjelwa pale baada ya kuona ATM then nikatoa pesa kama laki hivi. Nilinunua godoro, blanketi na koti jeusi. Ile shule tulikua tunavaa full black… Yani shati white, suruali black na koti Black… suit kabisa yani.

Nikarudi Tukuyu na kubeba vitu vyangu tayari kwenda shule. Yule dreva tax nilichukua namba yake na tulikuja kuwa washkaji baadae. Alinipeleka hadi stand ya kwenda huko ndani ndani (Mbambo, Itete hadi shuleni penyewe)
Sasa pake stand nilikutana na wanafunzi kibao wanaoenda shuleni ila cha kushangaza usafiri ulikua Canter na sio mabasi… Yani mnaning’inia huko juu kwenye canter.. wanawake ndo wanakaa chini. Asee niliishiwa nguvu baada ya kusikia hivyo.
Canter inajaza balaa na mizigo ni mingi mnoo kwani watu huja Tukuyu kununua mahitaji mengi na wengi ni wafanyabiashara kule kijijini.

Safari ilianza kama baada ya masaa mawili hivi na wanafunzi tulikua tunapiga story nyingi mnoo na swali kubwa ilikua ni kuulizana we umetokea wapi. Peke yangu ndo nilikua natoka Bukoba.
Ile safari ilikua ya mateso sana. Barabara ni vumbi, madaraja ya mbao alafu barabara ina milima na kona balaa (watu wa Mbeya hususani Tukuyu wananielewa vizuri hapa)

Ilikua Gari ikilalia upande wetu nasali sana maana ukiachia zile bomba ndo uko chini hivyo
Nilianza kujuta kwanini sikusoma Bukoba tu. Baada ya masaa matatu na nusu hivi tulifika shuleni… Asee nilihisi kuna kitu kimenikaba kooni kama nataka kulia kama nimebanwa (hii hali mnaijua wengi) kwa ufupi ningekua mtoto ningelia
Shule ilikua mwisho kabisa. Yani kata ya mwisho kabisaa baada ya hapo kuna Mlima Living stone so hakuna namna utaenda kokote.

Tulipokelewa shuleni tukaonyeshwa mabweni then tukaenda kula mtaani siku hiyo maana tulifika watu washapewa chakula cha jioni shuleni pale.
Nilifanikiwa kupata marafiki wengi na maisha ya kuishi mbali na wazazi yakaanza rasmi


Tuishie hapa kwa leo

See you kesho
Lufilyo secondary bro walikutupa mbali sana.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom