Maisha ya mtanzania kitendawili

MWananyati

Senior Member
Feb 3, 2011
160
53
Ilikua leo ndo mara ya kwanza kutumia daladala baada ya ongezeko la nauli zilizotangazwa na SUMATRA kwa jiji la dar es salaam. kwa kweli nimejisikia kuumia sana kwa sababu kwa mizunguko kadhaa niliyofanya nikakuta nimetumia 3,500/- wakati wiki iliyopita ilikua takribani 2,050/- kwa route hiohio. Basi nikawa natafakari na kuwaza maisha ya Mtanzania halisi ambaye kwa sasa anaishi kwa sh. 750/- kwa siku (Nusu Dola), ataweza vipi kumudu gharama hizi zinazoongezeka bila kuwa na chanzo kingine cha kuingiza kipato?
Kwa siku moja tu, chukulia familia ya watu wa tano kwa jiji la dar es salaam;

1. Mchele kilo 1 ----------------------- 1,500
2. Maharagwe (soya) kilo 1 ------------ 1,700
3. Unga kilo 1 ------------------------- 1,100/
4. Sukari kilo 1 ------------------------ 2100/- (itatumika kwa siku 6 maximum)
5. Mishumaa 3 (hakuna umeme) ------- 750/-
6. Mkaa (asubuhi hadi jioni) ----------- 2,000/
7. Sabuni mche (jamaa soap)1 -------- 2, 500/- (itatumika kwa wiki mbili)
8. Maji ya kutumia (ndoo 5) ----------- 1,500/-
9. Usafiri ----------------------------- 2,000/ (kukadiria tu)
10. Mengineyo ----------------------- 2,500/- ( simu, panadol, rb polisi nk.)

JUMLA 17,650/-

nini cha kutegemea kutoka kwa mtu huyu?
1. msongo wa mawazo
2. afya mbovu na maradhi mbalimbali (lishe duni)
3. Hasiri kwa jamii (wakati mwenye kosa serikali)
4. kujiingiza ktk vitendo viovu km kuvuta bangi, wizi, kuuza miili(changudoa), kuuza viungo vya binadamu, lugha chafu, madawa ya kulevya nk
5. Kuchanganyikiwa

HALAFU waziri anaibuka na kusema 'kama watanzania wana matatizo , serikali itayashughulikia' (mh. sophia simba) kwa maana ya kuwa hadi sasa serikali haioni kama watanzania wana-matatizo makubwa sana. Aliye kivulini hamjui wa kwenye jua jamaniiii!

TAFAKARII!!!:angry:
 
HIVI TUMESAHAU YALE MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA TULIAHIDIWA 2005...Kwa kasi mpya,ari mpya,nguvu mpya??????????
HIVI HAWAKURUDIA TENA KUTUAHIDI MAISHA MAZURI..kwa nguvu zaidi,kasi zaidi, na ari zaidi!!!!!!!!!!!!!!!!!!

HAYO NDO MAISHA YENYEWE SASA!!!
 
Ilikua leo ndo mara ya kwanza kutumia daladala baada ya ongezeko la nauli zilizotangazwa na SUMATRA kwa jiji la dar es salaam. kwa kweli nimejisikia kuumia sana kwa sababu kwa mizunguko kadhaa niliyofanya nikakuta nimetumia 3,500/- wakati wiki iliyopita ilikua takribani 2,050/- kwa route hiohio. Basi nikawa natafakari na kuwaza maisha ya Mtanzania halisi ambaye kwa sasa anaishi kwa sh. 750/- kwa siku (Nusu Dola), ataweza vipi kumudu gharama hizi zinazoongezeka bila kuwa na chanzo kingine cha kuingiza kipato?
Kwa siku moja tu, chukulia familia ya watu wa tano kwa jiji la dar es salaam;

1. Mchele kilo 1 ----------------------- 1,500
2. Maharagwe (soya) kilo 1 ------------ 1,700
3. Unga kilo 1 ------------------------- 1,100/
4. Sukari kilo 1 ------------------------ 2100/- (itatumika kwa siku 6 maximum)
5. Mishumaa 3 (hakuna umeme) ------- 750/-
6. Mkaa (asubuhi hadi jioni) ----------- 2,000/
7. Sabuni mche (jamaa soap)1 -------- 2, 500/- (itatumika kwa wiki mbili)
8. Maji ya kutumia (ndoo 5) ----------- 1,500/-
9. Usafiri ----------------------------- 2,000/ (kukadiria tu)
10. Mengineyo ----------------------- 2,500/- ( simu, panadol, rb polisi nk.)

JUMLA 17,650/-

nini cha kutegemea kutoka kwa mtu huyu?
1. msongo wa mawazo
2. afya mbovu na maradhi mbalimbali (lishe duni)
3. Hasiri kwa jamii (wakati mwenye kosa serikali)
4. kujiingiza ktk vitendo viovu km kuvuta bangi, wizi, kuuza miili(changudoa), kuuza viungo vya binadamu, lugha chafu, madawa ya kulevya nk
5. Kuchanganyikiwa

HALAFU waziri anaibuka na kusema 'kama watanzania wana matatizo , serikali itayashughulikia' (mh. sophia simba) kwa maana ya kuwa hadi sasa serikali haioni kama watanzania wana-matatizo makubwa sana. Aliye kivulini hamjui wa kwenye jua jamaniiii!

TAFAKARII!!!:angry:


hapa nahisi pressure inashuka, nikisema kwenda kwa babu nauli tu kwenda na kurudi ni kamshahara kangu kwa mwezi!! du

kweli tunakufa tunajiona!!

nimependa sana hapo kwenye blue!!!
 
Back
Top Bottom