Maisha ya Familia na Crisis ya Beki 3

Sumba-Wanga

JF-Expert Member
Feb 2, 2011
5,349
1,224
wanajamvi wenzangu,

Habari za jioni.

Kumekuwa na shida sana ya kupata na kuishi na hawa beki 3. Ni muhimu sana kwa maisha ya familia.

Familia yangu inahangaika sana. watoto bado wadogo, maisha magumu lazima tufanye kazi ili kuweza kusukuma gurudumu mbele.

Kama hiyo haitoshi, beki 3 wa siku hizi wamekuwa hatari sana, wengine wanawafanyia watoto mambo mabaya sana, wengine ni wachawi, mradi ni shida na mkanganyiko kwenye maisha ya familia. wazazi tunahangaika, watoto wanatabika. kazini hakukaliki, basi ni shida tupu.

Wenzetu, unafanyaje?
Mnapataje hawa beki 3?
 
toka kuanzishwa kwa shule za kata
huwezi pata housegirl kama zamani.....

unless uwe tayari kuwalipa better ....na sasa mshahara wao nasikia unaanzia elfu sitini....
ukitaka fanya kama wahindi wa city centre dar...
wanawalipa vizuri but hawalali majumbani
wanakuja na kuondoka na jumapili hawaji......na ukiwataka
unamuuliza housegirl yeyote wa wahindi city centre atakuletea.....
 
wanajamvi wenzangu,

Habari za jioni.

Kumekuwa na shida sana ya kupata na kuishi na hawa beki 3. Ni muhimu sana kwa maisha ya familia.

Familia yangu inahangaika sana. watoto bado wadogo, maisha magumu lazima tufanye kazi ili kuweza kusukuma gurudumu mbele.

Kama hiyo haitoshi, beki 3 wa siku hizi wamekuwa hatari sana, wengine wanawafanyia watoto mambo mabaya sana, wengine ni wachawi, mradi ni shida na mkanganyiko kwenye maisha ya familia. wazazi tunahangaika, watoto wanatabika. kazini hakukaliki, basi ni shida tupu.

Wenzetu, unafanyaje?
Mnapataje hawa beki 3?

Ni rahisi kuwapata, but kuwapata ambao hawatakuwa na tabia ulizoorodhesha hapo juu ni kazi kweli kweli. Labda cha kukushauri, tafuta mtu unayemfahamu if possible toka kijijini kwako/mkeo, be careful na tabia zake na ikibidi mchukue akiwa na akili zake timamu. Mimi nilimchukua aliyezalishwa na kutelekezwa. Anajua machungu ya maisha na pia anajua kulea watoto, im happy.
 
Duh siku hizi ni balaa mkuu
Wasichana wameerevuka hata kule ambako kulikuwa wanasema wanapatikana imekuwa issue sana
Shule za kata nazo zinawaondoa kwenye ufanyakazi wa nyumbani na kwenda kusoma
hawataki tena kufanya kazi za nyumbani
Ni balaa sana kwa sasa
 
siku hizi taabu tupu,
hata uwape nini hawaridhiki...
Tena wengine wanafanya mambo ya ajabu ukisikia unabaki mdomo wazi?

Ila wapo wachache wametulia....

Lakini kama mama ni makini...
Yupo karibu na watoto
anasimamia nyumba kwa hali ya juu...
Kidogo inasaidia......

Na usiombe upate hg mwenye agenda mbili mbili......
Lazima amtege faza house.......................
 
toka kuanzishwa kwa shule za kata
huwezi pata housegirl kama zamani.....

unless uwe tayari kuwalipa better ....na sasa mshahara wao nasikia unaanzia elfu sitini....
ukitaka fanya kama wahindi wa city centre dar...
wanawalipa vizuri but hawalali majumbani
wanakuja na kuondoka na jumapili hawaji......na ukiwataka
unamuuliza housegirl yeyote wa wahindi city centre atakuletea.....

Mkuu umesema kweli, kuwapa msharaha kama huo sio shida, mradi afanye kazi.

Ukipata bek 3 wa kuja na kwenda, kazi ni kwa watoto wanaokwenda shule mapema sana asubuhi: mwa mtaji huo Beki 3 lazima alale hapo hapo, Maanaa baba na mama wanaondoka saa 11 asubuhi!

Life is very challenging!
 
Ni rahisi kuwapata, but kuwapata ambao hawatakuwa na tabia ulizoorodhesha hapo juu ni kazi kweli kweli. Labda cha kukushauri, tafuta mtu unayemfahamu if possible toka kijijini kwako/mkeo, be careful na tabia zake na ikibidi mchukue akiwa na akili zake timamu. Mimi nilimchukua aliyezalishwa na kutelekezwa. Anajua machungu ya maisha na pia anajua kulea watoto, im happy.

Mkuu ni kweli, lakini wakati mwingine aliyezalishwa na kutelekezwa huwa ana wasi wasi na mwanae muda wote na anaweza asitulie. Nilishakuw anaye mmoja, kila siku simu kutoka Kijijini.
Mkuu, hata hivyo, kama ukipata kama huyo please ni pm
Familia yangu iko at the cross road.
 
Duh siku hizi ni balaa mkuu
Wasichana wameerevuka hata kule ambako kulikuwa wanasema wanapatikana imekuwa issue sana
Shule za kata nazo zinawaondoa kwenye ufanyakazi wa nyumbani na kwenda kusoma
hawataki tena kufanya kazi za nyumbani
Ni balaa sana kwa sasa

Kwa maana nyingine ni maendeleo kwa wao wenyewe na familia zao, ingawa tuna suffer.
Hata hivyo, ni kuwaombea kila la heri.
 
siku hizi taabu tupu,
hata uwape nini hawaridhiki...
Tena wengine wanafanya mambo ya ajabu ukisikia unabaki mdomo wazi?

Ila wapo wachache wametulia....

Lakini kama mama ni makini...
Yupo karibu na watoto
anasimamia nyumba kwa hali ya juu...
Kidogo inasaidia......

Na usiombe upate hg mwenye agenda mbili mbili......
Lazima amtege faza house.......................



This is the worse party of it....we have to live with it, hakuna jinsi, tunawahitaji sana.
 
toka kuanzishwa kwa shule za kata
huwezi pata housegirl kama zamani.....

unless uwe tayari kuwalipa better ....na sasa mshahara wao nasikia unaanzia elfu sitini....
ukitaka fanya kama wahindi wa city centre dar...
wanawalipa vizuri but hawalali majumbani
wanakuja na kuondoka na jumapili hawaji......na ukiwataka
unamuuliza housegirl yeyote wa wahindi city centre atakuletea.....

du aisee....
 
ngoja nikupe kaeksipiensi kangu kidogo.

Unapoletafuta au kuletewa beki 3, mfanyie intavyuu hata kama ya sekunde 2.

Usichukue aliyezaa na kumwacha mtoto kwao hasa kama watoto wako ni wadogo, ni ngumu sana yeye kuwapenda.

Mtu aliyekubuhu kwenye uzinzi si mzuri, anaweza acha watoto ndani na kwenda kupigwa kizizi. Anaweza hata lala huko huko.

Mlipe hela ambayo ataridhika, kama unaweza kuvuka kidogo expectation zake inasaidia.

Mpe uhuru usiodhuru familia, sio kila saa unamfuata mgongoni. Usitake 'perfection' coz no one is that perfect.

Mpe muda wa kujifunza na kuelewa rules za familia.

Mie wangu nimekaa naye miaka 4, wala hana hata dalili za kufikiria kuondoka. Ni mie mwenyewe kanichosha maana hataki ku-grow kikazi lol
 
Back
Top Bottom