Rev. Kishoka
JF-Expert Member
- Mar 7, 2006
- 4,526
- 1,529
Leo hii nimesoma habari inayosema kuwa Tanzania imeshindwa kupunguza vifo vya watoto walio chini ya miaka mitano ambao wanatoka kwenye familia masikini na fukara.
Nimejiuliza, tumeweka juhudi kubwa kama Taifa kujenga mfumo wa maisha ya anasa na hata katika kampeni hizi za uchaguzi, tunaahidiwa vitamanisha macho, viwanja vya ndege, meli, simu, majumba na ahadi zingine lukuki, lakin sijasikia ahadi hasa kutoka Chama tawala au kuona utekelezaji kwa ufanisi kupunguza umasikin wa lile kundi la watu ambao ni mafukara.
Sijasikia leo CCM katika kujisifu na utawala wao bora uliowaletea neema Watanzania kuwa wameweka juhudi za kulinda uhai wa Mtanzania ambaye hana uwezo wa kujitegemea na ni fukara. Leo Mtanzania huyu, atapewa kadi ya chama, kofia na fulana akipigie chama kura kwa kuwa kimeliongoza Tanzania kwa miaka 50 na Rais wetu kamleta Rais wa Marekani lakin chama hikihiki, hakiwezi mhakikishia Mtanzania huyu uhakika wa uhai wake dhidi ya magonjwa na lishe kwake na kwa watoto wake!
Natumaini habari hii vyama vya upinzani vitaziona na kuzifanyia kazi.
Nimejiuliza, tumeweka juhudi kubwa kama Taifa kujenga mfumo wa maisha ya anasa na hata katika kampeni hizi za uchaguzi, tunaahidiwa vitamanisha macho, viwanja vya ndege, meli, simu, majumba na ahadi zingine lukuki, lakin sijasikia ahadi hasa kutoka Chama tawala au kuona utekelezaji kwa ufanisi kupunguza umasikin wa lile kundi la watu ambao ni mafukara.
Sijasikia leo CCM katika kujisifu na utawala wao bora uliowaletea neema Watanzania kuwa wameweka juhudi za kulinda uhai wa Mtanzania ambaye hana uwezo wa kujitegemea na ni fukara. Leo Mtanzania huyu, atapewa kadi ya chama, kofia na fulana akipigie chama kura kwa kuwa kimeliongoza Tanzania kwa miaka 50 na Rais wetu kamleta Rais wa Marekani lakin chama hikihiki, hakiwezi mhakikishia Mtanzania huyu uhakika wa uhai wake dhidi ya magonjwa na lishe kwake na kwa watoto wake!
Natumaini habari hii vyama vya upinzani vitaziona na kuzifanyia kazi.
Tanzania yashindwa kupunguza vifo vya watoto maskini
na Andrew Chale
TANZANIA imeelezwa ni miongoni mwa nchi ambazo imeshindwa kutekeleza kupunguza vifo vya watoto walio chini ya miaka mitano kwa familia maskini na fukara kwa kipindi cha miaka kumi iliyopita.
Katika ripoti mpya iliyotolewa na Shirika la Save the Children linaloshughulikia misaada ya kibinadamu kwa watoto duniani, kwa vyombo vya habari jana, ilieleza Tanzania ni miongoni mwa nchi za Afrika zilizopoteza watoto 2,800,000 katika kipindi cha miaka kumi kutokana na kutokuwa na usawa.
Mkurugenzi wa shirika hilo hapa nchini, Rachel Pounds, alisema kuwa kama kutakuwa na usawa kwa jamii, ikiwemo kusaidia familia maskini kupata huduma muhimu za afya na kupunguza gharama za matibabu na dawa kunaweza kupunguza tatizo hilo kwa familia masikini na fukara.
Ni kwa kulenga suala la usawa tu serikali ikiwemo ile ya Tanzania zitaweza kupunguza vifo vya watoto miongoni mwa makundi yote katika jamii. Kila mtoto ana haki ya kuishi na kila serikali ina wajibu wa kuwalinda, alisema Rachel.
Katika ripoti yake hiyo maalumu, inayojulikana kama Fursa Sawa Katika Maisha imebainisha kuwa juhudi sawa za kupunguza vifo vya watoto miongoni mwa matajiri na maskini zinamaanisha mafanikio ya haraka ya kufikia lengo namba nne la maendeleo ya milenia.