Maini ya mnyama ni matamu sana lakini...

Unaacha kula maini, unatoka nje unapigwa na radi unakufa..... wwe kula bana ndo maana mnyamwa kabla ya kuchinjwa anyama inapimwa
 
Maini yanachuja sumu ila hayahifadhi sumu, yanaichuja kisha inapelekwa kuhifadhiwa kwenye bile duct (nyongo).

Kuna member mmoja ameshauri wakati wa kuyaandaa uyaloweke kwenye maziwa, kitaalam naweza sema hiyo ni ramli chonganishi labda kama unataka kupata taste ya maziwa kwenye pishi lako. Kingine ni kwamba sio kila sumu inakua neutralised na maziwa.

Endelea kula maini mkuu, pia ni mazuri sana kwa watu wenye upungufu wa damu kwasababu yana madini ya chuma kwa wingi yanayo usaidia mwili kutengeneza red blood cells.
 
Tupo kwenye ulimwengu wa GMO hakuna cha kukwepa, Kuna daktari aliniambia kuvaa viatu ni hatari kwa afya, nikamuuliza kwanin akanipa maelezo marefu ambayo sikuyaelewa mara kuna vinyweleo fulan vinahitaji hewa, mara unyayo unaathirika kwa namna flan, mara kucha zinavyoota zinahitaji space na vitu vingi,

nilitamani kumpima kama amepiga ghambe au lah ila sikuwa na kipimo nikamuacha nikasepa
 
Mmeandika. Ukweli utabaki kuwa elimu inazidi kuongezeka. Sayansi inazidi kupanuka. Uelewa unazidi kuwepo.
Kwa sasa yanayosemwa ni ukweli kuwa ndio uchunguzi wa kisasa.
Nani alijua miaka 50 iliyopita kuwa ugali, wali, viazi vinasababiaha mishipa ya damu kuziba? Nani alijua zamani kuwa chumvi inaongeza presha?
Zamani kukikuwa na vidonda ndugu. Kumbe ni kansa.
Ukweli utabaki ukweli kwamba twende na sayansi ya leo.
Ugali na viazi mishipa kuziba?
 
Ni kweli yana sumu lakini pia ndo kiungo chenye virutubisho vingi sana. Sababu kuna vimeng'enya vya kutosha kwenye ini. Chagua sasa mwenyewe.
 
Mmeandika. Ukweli utabaki kuwa elimu inazidi kuongezeka. Sayansi inazidi kupanuka. Uelewa unazidi kuwepo.
Kwa sasa yanayosemwa ni ukweli kuwa ndio uchunguzi wa kisasa.
Nani alijua miaka 50 iliyopita kuwa ugali, wali, viazi vinasababiaha mishipa ya damu kuziba? Nani alijua zamani kuwa chumvi inaongeza presha?
Zamani kukikuwa na vidonda ndugu. Kumbe ni kansa.
Ukweli utabaki ukweli kwamba twende na sayansi ya leo.
Simple logic kama kazi ya maini mwilini ni kuchuja sumu kwenye vyakula, basi ukila maini yenye sumu nayo si yanakuwa chakula, hivyo basi maini yako yataichuja tu hiyo sumu.
 
Back
Top Bottom