Eeka Mangi
JF-Expert Member
- Jul 27, 2008
- 3,173
- 481
Ndugu zangu, huyu kakosea nini hata ashambuliwe hivyo. Kama kosa lilikuwa ku-post thread yake pasipo basi angeelimishwa tu. Sijaona sababu ya kushambuliwa hivi. Maimaratha na PD wake ni watu kama tulivyo sisi, sasa kama wametapeli wasisemwe. labda huyo mlalamikaji hajui pa kwenda baada ya kutumia hata polisi na ikashindikana! Amekimbilia huku labda ama apate upanuzi wa mawazo anaishiwa kutupiwa maneno. JF inatakiwa iwe kimbilio la wote na sio kwa watu maalumu tu. Hata JK anachambuliwa hapa sembuse Maimaratha! Tusaidiane kuelimishana wana-JF. Mchango wangu na wako na wa mwingine unahitajika. Tusianze ujuaji wa kukemeana, SIO wote wanajua kupost huku maana nao wamejifunza humu humu tu, haipendezi. Hata kama mtu ana mwezi mmoja huku hata siku, tujmsaidie, bado ni sehemu ya familia na si vinginevyo.
UPENDO, UMOJA NA AMANI VITAWALE MIYOYO YETU.
UPENDO, UMOJA NA AMANI VITAWALE MIYOYO YETU.