Mahusiano, mapenzi, urafiki

Mwiba

JF-Expert Member
Oct 23, 2007
7,607
1,744
Mahusiano, mapenzi, urafiki je mambo haya ni lazima yafuatane au ni vitu vitatu tofauti ,Je kipo kinachoweza kukosekana au kisiwepo au kikawepo kimoja tu na vingine visihusishwe ,Kivipi ?
 
Mmh! Kweli hii University Exams (UE)
Kaka mimi sijui na kudesa nilishaacha
 
Neno mahusiano ni pana sana. Lina-include urafiki na mapenzi na kwenda mbali zaidi, mf. linagusa muungano uliopo kati ya watu wa damu (wazazi na watoto wao), mahusiano ya kazi (boss na aliye chini yake), nk.

Urafiki ni kipengele katika mahusiano. Ni ridhio la moyo kati ya watu wawili au zaidi yenye lengo la kutakiana mema katika maisha. Japo upo pia urafiki mbaya wa kupotoshana na kupelekana kusiko kwenyewe.

Mapenzi ni sehemu ya urafiki kwani yanagusa uhusiano kati ya mwanaume na mwanamke (urafiki/upendo) wenye kuhusisha kujamiiana kati yao.

Mapenzi katika maana ya love-making yanaweza yakawepo bila kuwepo urafiki. Mapenzi na urafiki yote ni mahusiano kati ya watu.
 
Mahusiano, mapenzi, urafiki je mambo haya ni lazima yafuatane au ni vitu vitatu tofauti ,Je kipo kinachoweza kukosekana au kisiwepo au kikawepo kimoja tu na vingine visihusishwe ,Kivipi ?

...itawezekana vipi pawepo mapenzi bila mahusiano, au urafiki huo utakuwa una mahusiano gani kama hakuna mapenzi? Sijaona mie wapenzi wasiokuwa na mahusiano, achilia mbali urafiki! :D
 
ki ukweli hivi ni vitu vinavyotegemeana,mara chache sana utakuta watu wamekuwa wapenzi bila urafiki.But ni vyema mka form urafiki kwanza na kuweza kumtambua wenzako kitabia hilo la love affairs litafuata.Kwa mantiki hiyo hivi ni vitu vinavyohusiana kwa karibu.
 
Naona mnabangaiza tu Ila ukweli bado hamjauona katika hayo mambo matatu ,kwa upande wangu naona urafiki ni kitu kingine na uhusiano ni kitu kingine na mapenzi ndio kabisa ila kuna product ambayo ndio itajumuisha yote hayo.
Hebu yapime haya yafyatayo :-
Hamuwezi kuwa marafiki halafu mkawa wapenzi wala hamuwezi kuwa na uhusiano halafu mkawa marafiki.

Ndugu hawezi kuwa rafiki wala mpenzi ,mke hawezi kuwa rafiki wala mpenzi wako ,jamani huwezi kusema huyu ni mpenzi wangu ,ukisema hivyo tu akili ya mke inaweza ikaruka na usiku pasikalike. Endeleeni nawapa muda mtafakari ,Mwiba :D
 
Naona mnabangaiza tu Ila ukweli bado hamjauona katika hayo mambo matatu ,kwa upande wangu naona urafiki ni kitu kingine na uhusiano ni kitu kingine na mapenzi ndio kabisa ila kuna product ambayo ndio itajumuisha yote hayo.
Hebu yapime haya yafyatayo :-
Hamuwezi kuwa marafiki halafu mkawa wapenzi wala hamuwezi kuwa na uhusiano halafu mkawa marafiki.

Ndugu hawezi kuwa rafiki wala mpenzi ,mke hawezi kuwa rafiki wala mpenzi wako ,jamani huwezi kusema huyu ni mpenzi wangu ,ukisema hivyo tu akili ya mke inaweza ikaruka na usiku pasikalike. Endeleeni nawapa muda mtafakari ,Mwiba :D

hahaha, mkuu mwiba hapo ndo umekoroga kabisa, yaani umefananisha utamu wa sukari na asali, ssa mke asipokuwa mpenzi wako anakuwa nani tena, au ndo huwa mnajifaragua kuwaita binti masudi sijui mama hepi, kwa siye tulioona mwanga kidogo ni wapenzi tu, hebu chunguza chunguza mahsuiano ambayo mke ni rafiki na mpenzi, utaona yana afya bila mgogoro; eeh..:D
 
hahaha, mkuu mwiba hapo ndo umekoroga kabisa, yaani umefananisha utamu wa sukari na asali, ssa mke asipokuwa mpenzi wako anakuwa nani tena, au ndo huwa mnajifaragua kuwaita binti masudi sijui mama hepi, kwa siye tulioona mwanga kidogo ni wapenzi tu, hebu chunguza chunguza mahsuiano ambayo mke ni rafiki na mpenzi, utaona yana afya bila mgogoro; eeh..:D
Unaanza Uhusiano halafu urafiki halafu ukimaliza kunakuja kupendana na hapo kukizidi kunaweza kukatoa mke.natumai mumeiona tofauti .Naona mgomba mnauita mdizi :D:D
 
Back
Top Bottom