Mahari na nafasi yake katika ndoa... Je, utamaduni huu umepitwa na wakati?

amani kwenu wana JF..
hivi umewah kutafakari hili suala zima la ulipaji mahari origin yake ni nn?!..na ni vigezo gain vinavyotumika ku evaluate thamani ya huyu mwanamke?. Embu fikiria, kitendo cha mwanaume kulipa mahari kina ulazima gani?, ukiangalia kwa makini ni kama mwanamke ananunuliwa vile!, na mtu akinunua kitu huwa anakitumia atakavyo,simply coz ameingia gharama!..jamani huu utamaduni (hii biashara) si unadhalilisha wanawake?
Anolds kijana wangu!
Suala la mahari ni la kimila, kidini na kimpenzi! Kwa mimi muumini wa dini ya Kiislamu mahari ni muhimu kwani ni zawadi kwa nayeolewa. Kiislamu kutokana na maandiko ya Kitabu chetu kitukufu anayeolewa ndiye hupewa mahari sio mzazi! Na mahari mara nyingi bi harusi huangalia uwezo wa mwenzi wake. Utashangaa mwanamme au anayeoa anaweza akaambiwa alipe hata kuku na kumsomea sura fulani kutoka kitabu kitakatifu. Au bi harusi anaweza kulipa kidogo kidogo katika maisha ya ndio yao. Kwa mila za Wasukuma kabila la mama yangu rangi ya bi harusi ndio ongezeko la wingi wa ng'ombe kwa mzazi! Naomba nisahihishwe pale nilipo kosea wana Jamii.
 
amani kwenu wana JF..
hivi umewah kutafakari hili suala zima la ulipaji mahari origin yake ni nn?!..na ni vigezo gain vinavyotumika ku evaluate thamani ya huyu mwanamke?. Embu fikiria, kitendo cha mwanaume kulipa mahari kina ulazima gani?, ukiangalia kwa makini ni kama mwanamke ananunuliwa vile!, na mtu akinunua kitu huwa anakitumia atakavyo,simply coz ameingia gharama!..jamani huu utamaduni (hii biashara) si unadhalilisha wanawake?
Anolds kijana wangu!
Suala la mahari ni la kimila, kidini na kimpenzi! Kwa mimi muumini wa dini ya Kiislamu mahari ni muhimu kwani ni zawadi kwa ayeolewa. Kiislamu kutokana na maandiko ya Kitabu chetu kitukufu anayeolewa ndiye hupewa mahari sio mzazi! Na mahari mara nyingi bi harusi huangalia uwezo wa mwenzi wake. Utashangaa mwanamme au anayeoa anaweza akaambiwa alipe hata kuku na kumsomea sura fulani kutoka kitabu kitakatifu. Au bi harusi anaweza kulipa kidogo kidogo katika maisha ya ndio yao. Kwa mila za Wasukuma kabila la mama yangu rangi ya bi harusi ndio ongezeko la wingi wa ng'ombe kwa mzazi! Naomba nisahihishwe pale nilipo kosea wana Jamii.
 
kuna jamaa yangu mmoja alinidokeza kuwa akikumbuka mahari aliyotoa kwa mkewe, humrukia kwa hasira kama simba aliyejeruhiwa kum-do kwa sababbu mahari yake inamuuma sana!!!!!!

nafikiri kwa isingizio hiki, wanawake wengi wenye visirani wamebakwa sana na wame zao!!!!!!!!!!!

japo lugha aliyotumia huyu kijana si muafaka sana, lakini kuna kitu cha kusoma pale.

naona mahari hi-signify commitment ya mume kwa mke na inajenga uvumilivu kwa kiasi fulani. kwani kama huyu akili kichakani alivyosema huyo mtu akikumbuka mhari hutafakari upya na kurejesha uhusiano na mwenzi wake (sikubaliani naye anaposema "humrukia" bali hujirudi na kurejesha uhusiano hasa kama uhusiano uliharibika kiasi cha kunyimana tendo la ndoa).

hivyo tunaweza kusema kuwa mahari husaida ku-control haiba ya mwanume na mwanamke pia kwani mwanmke hujsikia mwenye thamani kwani mwanaume kamgharimia kumpata na kuwa hakumchukua burebure. pia wazazi hujisika wamepata mkwe mwenye heshima na anayeheshimu commitmets za ndoa kama atalipa mahari kamilifu. zaidi ni mila zetu tu zenye mshiko muhimu kisaikologia na kidini kama mchangiaji mmoja livyosema kwenye dini ya kiislamu kuwa mahari hupewa mke

sikubaliani na mtoa mada kuwa ni biashara kwa wanawake. mwanamke ni mtu. sasa bei halali ya mtu ni kiasi gani? hakuna bei ya binadmu, hata wakati wa utumwa haikujulikana fair price ni sh aa ali kiasi gani.
 
acha ubairi mkuu mahari lazima ila aimaniishi unamnunua wife hapana ni just kujikomiti kiaina tu ila baadhi ya familia wamegeuza biashara

Inaonekana wewe nikija kuoa kwenu mtapanga mahari hata ya shilingi milioni tano halafu unasema mahari ni lazima.

Tatizo wahusika wanapanga mahari kama bidhaa au biashara ndio maana mtoa hoja anauliza ulazima wa mahari.
 
amani kwenu wana JF..
hivi umewah kutafakari hili suala zima la ulipaji mahari origin yake ni nn?!..na ni vigezo gain vinavyotumika ku evaluate thamani ya huyu mwanamke?. Embu fikiria, kitendo cha mwanaume kulipa mahari kina ulazima gani?, ukiangalia kwa makini ni kama mwanamke ananunuliwa vile!, na mtu akinunua kitu huwa anakitumia atakavyo,simply coz ameingia gharama!..jamani huu utamaduni (hii biashara) si unadhalilisha wanawake?
Suala la kulipa mahari ni la kiutamaduni ndugu! Sehemu zingine (mf. India) mwanamke ndiye analipa mahali kwa mwanaume, na analipa pesa nyingi tu. Huku TZ na sehemu zingine za afrika mwanaume ndiye analipa mahari.

Mahari siyo gharama ya mwanamke kwa sababu mtu hanunuliki kwa fedha, dhahabu au almasi. Yuko juu ya yote hayo. Kumbe mahari ni zawadi kwa wazazi kwa wazazi wa mtoto wa kike. Kwa nini awe mwanaume tu wa kufanya hivi? Ni kwa sababu yeye ndiye ANAYEOA, na binti ANAOLEWA. Anayeoa anapewa uwezo wa KUMILIKI mke. Na anayeolewa anapata uwezo wa KUMILIKIWA. Na kwa sababu ya concepts hizi ndiyo maana unakuta mwanaume (mmiliki) anapewa uwezo wa kuoa (kumiliki) hata zaidi ya mke mmoja (mitara).
Kumbe mahari inaimarisha mahusiano ya familia 2 za wanandoa, na ni heshima - kimila - kwa muolewa.
 
kikwetu, mahari ni kipimo cha mwanaume kujibidisha, kwani mwanaume anatarajiwa awe na uwezo wa kuitunza familia yake.
 
You are misleading the matter I doubt.
What are you knowledgeable with?
BOTH!....i have paid the bride-price,lakini i have seen with my naked eyes a woman paying groom-price.

lakini hizo zote kiswahili chake ni kimoja-MAHARI.hoja yangu ni kwamba walau ungeandika:
MAHARI(Bride/Groom Price)......
 
Unataka tufanyeje? Tusitoe mahari? Hapana mkuu! Mahari ina maana sana. Ni zawadi kwa wazazi wa mume/mke. Ni kikolezo cha mahusiano mapya kati ya familia 2 za wanandoa. Kumbe ina uzito ndugu. Tuendelee kulipa tu kwa wazazi wa wenye mabinti (kwa wafrika wengi) na wenye vijana wa kiume (kwa wahindi).
 
Back
Top Bottom