Mahari bila bi harusi

Siri Sirini

JF-Expert Member
Mar 12, 2012
547
198
Habari wana jamvi, jamani leo mida ya jioni tunaenda kutoa mahari maeneo fulani kwa kabila la wamakonde, kijana anayetaka kuoa ni mhaya, sasa kituko ni kwamba, huyo mtolewa mahari hayupo, yupo chuo, ukiwauliza ndugu zake kwanini acje hata cku 2 wanasema ana mitihani, sasa me najiuliza, hyo mahari kwanini wasiihairishe mpaka binti arudi? Mana nivyojua cku ya kutoa mahari ndio cku ya kuvishwa pete ya uchumba.
Wana jamvi hii imekaaje? Na wamakonde washajiandaa kupokea ugeni, au unaweza toa mahari bila mhucka kuwepo? Akija kukataa je kuwa hakuiona hyo mahari itakuwaje? Na bwana haruc mtarajiwa amekubali hivyohivyo mana anayempelekesha ni mama yake mdogo, na ndiye mwenye pesa, anaogopa akikataa wanaweza wacende tena, mchango wenu plz, mana me cna hata ham ya kwenda.
 
Mahari si lazima bibi harusi mtarajiwa awepo anaweza kuwakilisha wazee wake au watu anawaamini, pete ya uchumba sio lazima ni function mnaweza kufanya baadaye.
 
Navyo fahamu mahari haitolewi mpaa bi harusi awe kisha mkubali mwanaume, kuwepo kwake kusiwepo kwake time inatolewa sio lazima awepo, lakini ukienda ki deep sana inatakiwa bi harusi awepo, sababu hizo ni pesa zake.

Lakini kuna wazee wengine huwa mahari wao wanafanya kama mtaji wanazichukua wao zinakuwa zao ambapo ni kosa, mtoa mada mimi niko na wewe kwenye hio point yako, inafaa bi harusi awepo, lakini ukweli ulivyo sio lazima awepo yeye kuzipokea.
 
sio lazima awepo.

na bwana harusi si bora afurahie kuwa binti anaangalia future yao kufaulu na sio kuja kuwa house wife.

wahaya mtakuwa mmeongea kikwenu na kumsema binti wa watu hadi amejing'ata ulimi labda.
 
Kama mazingira hayaruhusu bi harusi awepo mnaweza kuendelea. Halafu msisahau kuwa mahari hailipwi yote. Lol. Mchukue video na maphoto ya kutosha kwa ukumbusho.
 
Kama mazingira hayaruhusu bi harusi awepo mnaweza kuendelea. Halafu msisahau kuwa mahari hailipwi yote. Lol. Mchukue video na maphoto ya kutosha kwa ukumbusho.

Niliisikia hii sikuamini labda sijui, unalipwa in instalment akizaa ndio final settlement inatolewa, duuh kama bidhaa hivi!
 
Back
Top Bottom