Mahakama yawaachia huru waumini wa Kanisa la Watch Tower waliokataa watoto wao wasipewe Chanjo ya Surua

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Feb 7, 2022
2,308
5,460
RUKWA: Mahakama Kuu, Kanda ya Sumbawanga imewaachia huru Wachungaji na Waumini saba wa Kanisa la Watch Tower Wilayani Kalambo waliohukumiwa kifungo cha mwaka mmoja jela kwa kosa la kuzuia Watoto walio chini ya umri wa miaka mitano kupewa chanjo ya Surua.

Imefahamika hukumu iliyotolewa kwa waumini hao ambao walishtakiwa katika Mahakama ya Mwanzo kisha adhabu yao ya kwenda jela mwaka mmoja ilithibitishwa na Mahakama ya Wilaya, ilikuwa na dosari kadhaa za kisheria.

Baadhi ya dosari ni kuwa Waumini walidaiwa kugomea amri lakini haikubainishwa waligomea amri ya nani na pia hawakupewa nafasi ya kujitetea.

Chanzo: Azam TV
 
RUKWA: Mahakama Kuu, Kanda ya Sumbawanga imewaachia huru Wachungaji na Waumini saba wa Kanisa la Watch Tower Wilayani Kalambo waliohukumiwa kifungo cha mwaka mmoja jela kwa kosa la kuzuia Watoto walio chini ya umri wa miaka mitano kupewa chanjo ya Surua.

Imefahamika hukumu iliyotolewa kwa waumini hao ambao walishtakiwa katika Mahakama ya Mwanzo kisha adhabu yao ya kwenda jela mwaka mmoja ilithibitishwa na Mahakama ya Wilaya, ilikuwa na dosari kadhaa za kisheria.

Baadhi ya dosari ni kuwa Waumini walidaiwa kugomea amri lakini haikubainishwa waligomea amri ya nani na pia hawakupewa nafasi ya kujitetea.

Chanzo: Azam TV
Hahaha.
 
Back
Top Bottom