Jembe Jembe
JF-Expert Member
- Jun 9, 2016
- 750
- 1,800
Mahakama kuu Kanda ya Arusha, imemtengua msimamizi wa mirathi za marehemu Bilionea Erasto Msuya, Miriam Mrita aliyekuwa Mke wa Marehemu baada ya kushindwa kugawa Mali za marehemu Kwa wakati.
Bilionea Msuya, aliuawa Kwa kupigwa risasi zaidi ya 20 miaka tisa iliyopita katika eneo la Mijohoroni, wilayani ya Hai mkoani Kilimanjaro.
Akisoma hukumu hiyo Jana iliyokuwa ikionyeshwa kwa njia ya Video jaji wa Mahakama hiyo, Devota Kamzola alisema kuwa mahakama hiyo baada ya kupitia hoja za pande zote mbili imejiridhisha pasipo shaka kwamba mali za marehemu hazikuwahi kukusanywa ,kutolewa taarifa na kugawanywa Kwa wanufaika katika kipindi Cha miaka 9 tangu msimamizi wa mirathi ateuliwe.
Aidha mahakama hiyo imewateua watoto wawili wa marehemu Msuya, Glory Msuya na Simon Kelvin Msuya kuwa wasimamizi wa mirathi na kuagiza ndani ya miezi Sita wawe wamekusanya ,kuhakiki Madeni ,kugawanya Mali Kwa wanufaika na kutoa Taarifa mahakamani .
Shauri la kupinga msimamizi wa mirathi namba 66/2019 lilifunguliwa na Ndeshukulwa Msuya Mama wa marehemu Erasto dhidi ya mkwe wake Miriamu Msuya ambaye aliteuliwa na mahakama novemba 2013 kuwa msimamizi wa mirathi kupitia shauri la mirathi namba 8/2013.
Ndeshukulwa kupitia mawakili wake,Ismail Sharua na Fadhili Nangawe waliiomba mahakama hiyo imtengue Miriamu Mrita kuwa usimamizi wa mirathi ya mwanaye Kwa madai kwamba tangu ateuliwe hakuwahi kukusanya, kufunga na kugawanya Mali Kwa wakati.
Hoja zingine zilizowasilishwa na mawakili hao ni kwamba Miriamu Mrita anakabiliwa na kesi ya mauaji namba 5/2017 mahakamani isiyo na dhamana, pia alishindwa kumjali Kwa matumizi Mtoto wa marehemu mumewe Glory Msuya aliyekuwa nje ya nchi Kwa kumpatia fedha za ada, nauli ya kurejea nchini pamoja na matumizi binafsi.
Wakati hukumu hiyo ikisomwa na Jaji Kamzola mjibu maombi, Miriam Mrita alikuwa akiona na kusikilizwa kupitia mtandao wa mahakama(Video Conference) wakati akiwa katika Gereza la Segerea jijini Dar es salamu.
Akiongea mara baada ya kutolewa Kwa uamuzi huo, Familia ya Msuya kupitia Ndeshukulwa Msuya alishukuru mahakama hiyo Kwa kutenda haki Kwa kuwa lengo lao ni kuhakikisha watoto wa marehemu wanakuwa na haki ya kusimamia na kunufaika na Mali za baba Yao na sio mtu mwingie yoyote.
"Mimi sikuhitaji Mali yoyote ya mwanangu nilichotaka Mali zote zosimakiqe na watoto na sio mtu mwingine yeyote, tumepokea Kwa Furaha hukumu ya mahakama na haki imetendeka"alisema Msuya
Akiongea Kwa niaba ya Miriamu Mrita, Steven Mrita ambaye alikuwa msimamizi wa Mali za marehemu ikiwemo hoteli ya kitalii ya Sg baada ya kukabidhiwa na dada yake (Miriamu )alisema kwa upande wao wameridhika na uamuzi wa mahakama na hawàtakuwa na pingamizi lolote.
"Sisi tumeridhika Kwa moyo mweupe na uamuzi wa mahakama na hatutakuwa na pingamizi" alisema Mrita.
Ends
---
VIDEO: Mauaji ya Erasto Msuya, Aneth Msuya na hukumu ya Miriam Mrita
Soma Sakata la Kifo cha Bilionea Msuya
MWENENDO WA KESI MAUAJI YA BILIONEA ERASTO MSUYA
Septemba 17, 2013 watuhumiwa wakiwa kwa mganga wakijizindika wasikamatwe
Soma Waliomua Bilionea Erasto Msuya wakutwa kwa sangoma
Juni 12, 2014, Mahakama yaelezwa jinsi Erasto Msuya alivyouawa
Soma Mahakama yaelezwa bilionea wa madini Erasto Msuya alivyouawa
Oktoba 27, 2017, Shahidi adai kuahidiwa Tsh 17m kutekeleza mauaji
Soma Shahidi aelezea walivyoahidiwa kulipwa Sh 17 milioni kila mmoja kumuua bilionea Msuya
Mei 11, 2018, Shahidi alidai kuwa Mfanyabiasha wa Madini, Chusa ndiye alipanga mauaji
Soma SHAHIDI: Chusa alipanga mauaji ya Bilionea Msuya
Mei 14, 2018 Mahakama iliwakuta na kesi ya kujibu washtakiwa 6
- Kesi ya bilionea Msuya: Sita wana kesi ya kujibu huku mmoja akiachiwa huru
Julai 23, 2018 washtakiwa wahukumiwa kunyongwa hadi kufa
soma Washtakiwa watano mauaji ya bilionea Msuya wahukumiwa na Mahakama Kuu adhabu ya kunyongwa hadi kufa
Agosti 18, 2018 waliohukumiwa kunyongwa hadi kufa wakata rufani
Soma Waliohukumiwa kwa mauaji ya Bilionea Msuya wapinga kunyongwa
Jaji aliyetoa hukumu atishiwa kifo
Soma Jaji aliyesikiliza kesi ya mauaji ya Bilionea Msuya na kutoa hukumu ya kifo atishiwa kuuawa
Pia soma Aliyeachiwa kesi ya mauaji ya Bilionea Msuya aeleza mazito
MAUJI YA ANETH MSUYA NA MWENENDO WA KESI YA MAUAJI YAKE
Aneth Msuya aliuawa kinyama akiwa nyumbani kwake Kibada
Soma Aneth Msuya ambaye ni dada wa bilionea Erasto Msuya auawa kinyama Dar
AUG 23, 2016 Mirima Mrita alipandishwa kizimbani kwa tuhuma za mauji ya Aneth Msuya
Soma Mjane wa Erasto Msuya apandishwa Kizimbani Kisutu
SEPT 18, 2023 Mahakama ilimkuta Miriam Mrita na kesi ya kujibu Mauji ya Aneth Msuya
Soma Dar: Mke wa Bilionea Msuya akutwa na Kesi ya Kujibu mauaji ya wifi yake
FEB 23, 2024 Mahakama Kuu ilimuachia huru Miriam Mrita
Soma Mjane wa bilionea Msuya aachiwa huru, Mahakama haijamkuta na hatia mauaji ya Aneth Msuya
UGOMVI WA MALI ZILIZOACHA NA ERASTO MSUYA
Familia ilishindwa kuelewana suala la mirathi na kupelekea Serikali kuingilia kati
Soma Mali za Marehemu Bilionea Erasto Msuya, ndugu ngumi mkononi
Mama Mzazi wa Erasto Msuya adai kuwa mjane alikomba mali kabla ya mazishi
Soma Mama wa Bilionea Msuya: Mke alikomba mali kabla ya kumzika mwanangu
Wadau wahoji uhalali wa ndugu wa Miriam Mrita kusimamia mali za Erasto Msuya
Soma Mama wa Bilionea Msuya: Mke alikomba mali kabla ya kumzika mwanangu
Mama Mzazi wa Msuya akubali kuondoa shauri Mahakamani ili kulimaliza kifamilia
soma Mama wa Bilionea Msuya akubali kuondoa kesi kwa Muda Mahakamani
Mahakama yataka pande mbili za familia kukaa meza moja na kuondoa tofauti
Soma Ugomvi wa Mali za Marehemu Bilionea Msuya, Mahakama yanena
2021, Mahakama ilifikia uamuzi wa kumuondoa Miriam Mrita kuwa msimamizi wa Mali
Soma Mahakama yamuengua mjane wa Bilionea Erasto Msuya kusimamia Mirathi ya Mumewe
Bilionea Msuya, aliuawa Kwa kupigwa risasi zaidi ya 20 miaka tisa iliyopita katika eneo la Mijohoroni, wilayani ya Hai mkoani Kilimanjaro.
Akisoma hukumu hiyo Jana iliyokuwa ikionyeshwa kwa njia ya Video jaji wa Mahakama hiyo, Devota Kamzola alisema kuwa mahakama hiyo baada ya kupitia hoja za pande zote mbili imejiridhisha pasipo shaka kwamba mali za marehemu hazikuwahi kukusanywa ,kutolewa taarifa na kugawanywa Kwa wanufaika katika kipindi Cha miaka 9 tangu msimamizi wa mirathi ateuliwe.
Aidha mahakama hiyo imewateua watoto wawili wa marehemu Msuya, Glory Msuya na Simon Kelvin Msuya kuwa wasimamizi wa mirathi na kuagiza ndani ya miezi Sita wawe wamekusanya ,kuhakiki Madeni ,kugawanya Mali Kwa wanufaika na kutoa Taarifa mahakamani .
Shauri la kupinga msimamizi wa mirathi namba 66/2019 lilifunguliwa na Ndeshukulwa Msuya Mama wa marehemu Erasto dhidi ya mkwe wake Miriamu Msuya ambaye aliteuliwa na mahakama novemba 2013 kuwa msimamizi wa mirathi kupitia shauri la mirathi namba 8/2013.
Ndeshukulwa kupitia mawakili wake,Ismail Sharua na Fadhili Nangawe waliiomba mahakama hiyo imtengue Miriamu Mrita kuwa usimamizi wa mirathi ya mwanaye Kwa madai kwamba tangu ateuliwe hakuwahi kukusanya, kufunga na kugawanya Mali Kwa wakati.
Hoja zingine zilizowasilishwa na mawakili hao ni kwamba Miriamu Mrita anakabiliwa na kesi ya mauaji namba 5/2017 mahakamani isiyo na dhamana, pia alishindwa kumjali Kwa matumizi Mtoto wa marehemu mumewe Glory Msuya aliyekuwa nje ya nchi Kwa kumpatia fedha za ada, nauli ya kurejea nchini pamoja na matumizi binafsi.
Wakati hukumu hiyo ikisomwa na Jaji Kamzola mjibu maombi, Miriam Mrita alikuwa akiona na kusikilizwa kupitia mtandao wa mahakama(Video Conference) wakati akiwa katika Gereza la Segerea jijini Dar es salamu.
Akiongea mara baada ya kutolewa Kwa uamuzi huo, Familia ya Msuya kupitia Ndeshukulwa Msuya alishukuru mahakama hiyo Kwa kutenda haki Kwa kuwa lengo lao ni kuhakikisha watoto wa marehemu wanakuwa na haki ya kusimamia na kunufaika na Mali za baba Yao na sio mtu mwingie yoyote.
"Mimi sikuhitaji Mali yoyote ya mwanangu nilichotaka Mali zote zosimakiqe na watoto na sio mtu mwingine yeyote, tumepokea Kwa Furaha hukumu ya mahakama na haki imetendeka"alisema Msuya
Akiongea Kwa niaba ya Miriamu Mrita, Steven Mrita ambaye alikuwa msimamizi wa Mali za marehemu ikiwemo hoteli ya kitalii ya Sg baada ya kukabidhiwa na dada yake (Miriamu )alisema kwa upande wao wameridhika na uamuzi wa mahakama na hawàtakuwa na pingamizi lolote.
"Sisi tumeridhika Kwa moyo mweupe na uamuzi wa mahakama na hatutakuwa na pingamizi" alisema Mrita.
Ends
VIDEO: Mauaji ya Erasto Msuya, Aneth Msuya na hukumu ya Miriam Mrita
Soma Sakata la Kifo cha Bilionea Msuya
MWENENDO WA KESI MAUAJI YA BILIONEA ERASTO MSUYA
Septemba 17, 2013 watuhumiwa wakiwa kwa mganga wakijizindika wasikamatwe
Soma Waliomua Bilionea Erasto Msuya wakutwa kwa sangoma
Juni 12, 2014, Mahakama yaelezwa jinsi Erasto Msuya alivyouawa
Soma Mahakama yaelezwa bilionea wa madini Erasto Msuya alivyouawa
Oktoba 27, 2017, Shahidi adai kuahidiwa Tsh 17m kutekeleza mauaji
Soma Shahidi aelezea walivyoahidiwa kulipwa Sh 17 milioni kila mmoja kumuua bilionea Msuya
Mei 11, 2018, Shahidi alidai kuwa Mfanyabiasha wa Madini, Chusa ndiye alipanga mauaji
Soma SHAHIDI: Chusa alipanga mauaji ya Bilionea Msuya
Mei 14, 2018 Mahakama iliwakuta na kesi ya kujibu washtakiwa 6
- Kesi ya bilionea Msuya: Sita wana kesi ya kujibu huku mmoja akiachiwa huru
Julai 23, 2018 washtakiwa wahukumiwa kunyongwa hadi kufa
soma Washtakiwa watano mauaji ya bilionea Msuya wahukumiwa na Mahakama Kuu adhabu ya kunyongwa hadi kufa
Agosti 18, 2018 waliohukumiwa kunyongwa hadi kufa wakata rufani
Soma Waliohukumiwa kwa mauaji ya Bilionea Msuya wapinga kunyongwa
Jaji aliyetoa hukumu atishiwa kifo
Soma Jaji aliyesikiliza kesi ya mauaji ya Bilionea Msuya na kutoa hukumu ya kifo atishiwa kuuawa
Pia soma Aliyeachiwa kesi ya mauaji ya Bilionea Msuya aeleza mazito
MAUJI YA ANETH MSUYA NA MWENENDO WA KESI YA MAUAJI YAKE
Aneth Msuya aliuawa kinyama akiwa nyumbani kwake Kibada
Soma Aneth Msuya ambaye ni dada wa bilionea Erasto Msuya auawa kinyama Dar
AUG 23, 2016 Mirima Mrita alipandishwa kizimbani kwa tuhuma za mauji ya Aneth Msuya
Soma Mjane wa Erasto Msuya apandishwa Kizimbani Kisutu
SEPT 18, 2023 Mahakama ilimkuta Miriam Mrita na kesi ya kujibu Mauji ya Aneth Msuya
Soma Dar: Mke wa Bilionea Msuya akutwa na Kesi ya Kujibu mauaji ya wifi yake
FEB 23, 2024 Mahakama Kuu ilimuachia huru Miriam Mrita
Soma Mjane wa bilionea Msuya aachiwa huru, Mahakama haijamkuta na hatia mauaji ya Aneth Msuya
UGOMVI WA MALI ZILIZOACHA NA ERASTO MSUYA
Familia ilishindwa kuelewana suala la mirathi na kupelekea Serikali kuingilia kati
Soma Mali za Marehemu Bilionea Erasto Msuya, ndugu ngumi mkononi
Mama Mzazi wa Erasto Msuya adai kuwa mjane alikomba mali kabla ya mazishi
Soma Mama wa Bilionea Msuya: Mke alikomba mali kabla ya kumzika mwanangu
Wadau wahoji uhalali wa ndugu wa Miriam Mrita kusimamia mali za Erasto Msuya
Soma Mama wa Bilionea Msuya: Mke alikomba mali kabla ya kumzika mwanangu
Mama Mzazi wa Msuya akubali kuondoa shauri Mahakamani ili kulimaliza kifamilia
soma Mama wa Bilionea Msuya akubali kuondoa kesi kwa Muda Mahakamani
Mahakama yataka pande mbili za familia kukaa meza moja na kuondoa tofauti
Soma Ugomvi wa Mali za Marehemu Bilionea Msuya, Mahakama yanena
2021, Mahakama ilifikia uamuzi wa kumuondoa Miriam Mrita kuwa msimamizi wa Mali
Soma Mahakama yamuengua mjane wa Bilionea Erasto Msuya kusimamia Mirathi ya Mumewe