Mahakama yaamuru Cyprian Musiba kulipa faini ya Tsh. bilioni 6 kwa kumchafua Bernard Membe

venance7

JF-Expert Member
May 15, 2019
555
1,637
Mahakama kuu ya Tanzania imetoa hukumu ya kesi ya kuchafuliwa jina iliyokuwa ikimkabili mkurugenzi mkuu wa gazeti la Tanzanite na mwanaharakati huru, ndugu Musiba dhidi ya aliyekuwa Waziri wa zamani wa Mambo ya Nje na mgombea Urais kupitia ACT-Wazalendo, ndugu Bernard Membe. Mahakama hiyo imemtaka Musiba kulipa kiasi hicho cha pesa.

==========

Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam imemuamuru mwanahabari anayejitambulisha kama mwanaharakati huru, Cyprian Musiba kumlipa fidia ya Sh6 bilioni aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje katika Serikali ya Awamu ya Nne, Bernard Membe.

Hukumu hiyo imetolewa leo Alhamisi Oktoba 28,2021 na Jaji Joacquine De Mello aliyeisikiliza kesi hiyo.

Katika hukumu hiyo Musiba ametakiwa kumlipa Membe kiasi hicho cha fedha pamoja na gharama zote za uendeshaji wa kesi kwa zaidi ya miaka miwili.

Pia imeweka zuio la kudumu kwa Musiba la kutokumkashifu Membe au kusema uongo dhidi yake.

Mwananchi

Pia, soma=> Benard Membe: Musiba hasimami tena na kujifanya yeye ni Mungu Mtu. Huko uliko naomba hela zangu
 
Aanze kulipa Bukubuku kwa siku, mdogomdogo atamaliza...

Kujifanya unatetea dubwana kubwa linaloitwa au litaasisi kubwa lenye mizizi iliyojichimbia sana alafu huna koneksheni za maana ni ujinga.

ujanja wa mwanasiasa na mpambe wake huwa ni miaka mitano. Sasa unapokuwa shabiki wa mtu mwenye kinga kisheria ibadi akili iwe nyepesi sana kujiongeza na kucheza miguu yote miwili huku ukiweka akiba incase akafariki siasa au akafariki dunia kabisa.
 
Mahakama kuu ya Tanzania imetoa hukumu ya kesi ya kuchafuliwa jina iliyokuwa ikimkabili mkurugenzi mkuu wa gazeti la Tanzanite na mwanaharakati huru ,ndugu musiba dhidi ya aliyekuwa waziri wa zamani wa mambo ya nje na mgombea urais kupitia ACT ndugu Bernard membe.Mahakama hiyo imemtaka musiba kulipa kiasi hicho cha pesa
Kwa hiyo huyu mwamba kwa sasa ana madeni yapatayo 13bilion! Manake kule kuna shangazi Fatuma alipata tuzo ya 7b na huku Membe 6b. Nadhani sasa Musiba ni raia anayedaiwa madeni makubwa kuliko raia yeyote hapa nchini na anastahili sifa ya Highly Indebted Poor Person (HIPC).
 
Huyu jamaa kuna kipindi nilikuwa nafungua uzi kulalamika kwa nini anaachiwa achafue watu nilikuwa nadhihakiwa na mashabiki wake halafu baada ya muda uzi unaondolewa, naona sasa anavuna alichopanda !
20211028_115658.jpg
 
Back
Top Bottom