Mahakama kupitia Jaji Mkuu imjibu Makonda. Kukaa kimya wananchi wataamini asemayo

Jaji Mfawidhi

JF-Expert Member
Feb 20, 2016
14,047
20,411
Paul Makonda, Mwenezi wa CCM akiwa anazunguka nchi nzima kwa misafara mirefu kuliko kiongozi yeyote na kusikiliza kero na kuwalalamikia CCM wenzake kwa kutofanya kazi. Mwanzo alianza na kulalamikia CHADEMA, AKAJA KWA MBOWE SASA wana CCM wenzie.

Makonda amewaambia wananchi na kuwaagiza wasipeleke kesi Mahakmani kwakuwa hawana hela kama yeye ili kununua haki na kwamba hata yeye alidhulumiwa nyumba lakini akaona asiende mahakamani maana hatapata haki.

Juzi hapa Makonda alielimishwa na Mh AG Eliezer Feleshi ambaye kama watu hawajui FELESHI ndiye Mshauri Mkuu wa Nchi ya Tanzania. Sasa Makonda kampanda kichwani, Mahakama na AG, wamekaa kimya.

Hii kauli ya Makonda tunaweza kuitazama kwa angle nyingi lakini inauvua nguo mfumo wa haki nchini.

Kwa bahati mbaya ni kauli ya kweli kabisa. Ndio, ni kauli ngumu lakini ina akisi tatizo la mfumo wetu wa utoaji haki.Mahakimu mishahara ya milioni na nusu lakini wanautajiri uliopindukia huku wakiwa na anasa mitaani. Fedha za wenyenazo dhidi ya wasio nazo.

Anachosema Makonda ni kuwa bila kuwa na pesa na connection, sahau HAKI hasa kwenye mahaama. Yeye anaamini anazidiwa fedha na GSM ndio maana nyumba ya masaki kasamehe.

Ninachopingana na Makonda ni kuwa haki ipo serikalini, hii sio kweli. Wala serikali sio chombo cha kutoa haki, chombo cha haki ni mahakama/judiciary. Ni muhimili unaojitegemea.

Tunahitaji kujenga mfumo wa mahakama ulio huru na unaosimamia kweli na usioegemea upande wowote.

Rostam Aziz alisema kuhusu Mfumo wa Mahakama kuwa umeoza akaambiwa akanushe chap sasa Mwenezi anaonesha panapovuja na ndio Uhalisia.

Mfumo ambao haki siyo upendeleo bali ni fursa inayoweza kupatikana na kila mtu. Ni muhimu sasa, zaidi ya wakati wowote, kutafuta suluhu na kufanya mahakama zetu kuwa huru. Mbona Kenya wanaweza? Hawa si ni wenzetu tu wa eneo hili la Afrika Mashariki?

Makonda anasema mfumo wetu wa utoaji haki umeoza, inawezekana ni kweli. Basi turekebishe huo mfumo, tusiukimbie na kutengeneza mfumo mwingine. Hiyo sio solution.

Pia Soma:
- Paul Makonda: Maskini Ukizulumiwa Haki Usikimbilie Mahakamani" Mahakama Wajitafakari
 
Mahakama ni chombo Cha wenye pesa kuhalalisha dhuluma Kwa maskini, acheni upuuzi
Halafu Kuna watu walikuwa wanawaambia cdm waende mahakamani kama wameibiwa uchaguzi. Mwanaccm aliyeshiriki Moja kwa Moja kuharibu mfumo wa mahakama anaweka ushahidi kuwa mahakama sio sehemu ya kupatia haki!

Tulimshauri Jaji mkuu kitendo Cha wapinzani kutokufungua kesi mahakamani walidhihirisha mfumo wa mahakama ni bure na alipaswa kujiuzulu. Haya walioamua kuchafua mfumo wa mahakama ndio hao wanasema watu wasiende huko, utashangaa jaji mkuu ataendelea kukomaa ofisini.
 
Alichosema Makonda ni ukweli kwamba mtu masikini hana hela ya kumlipa wakili mzuri kwenye kesi yake. Na anaweza kupata wakili lakini huyo wakili pia akanunuliwa na upande wa pili ikawa balaa lilelile.

Na kama hauna wakili mzuri mahakama itasikiliza kesi na kuangalia Sheria inasemaje na unaweza kukosa Haki yako kwa mujibu wa Sheria.

Nyerere aliwahi kusema "Haki na Sheria ni vitu viwili tofauti"
 
Unasemaje na kutolea mfano wa kenya wakati hapo majuzi tu Rais wao Mh William Ruto alipinga maamuzi ya mahakama na kusema kuwa mahakama zinapindisha sheria na hivyo hata fuata amri zao?

Mimi nipo nasimama na mzalendo wa kweli wa Taifa letu ,msema kweli,kijana jasiri kusini mwa jangwa la sahara na Rais mtarajiwa kuanzia
2030 Mheshimiwaa Paul Christian Makonda.
 
Ukiwa na kesi na Serikali sahau neno HAKI ...labda uende kwenye mahakama za Africa Mashariki na kuendelea ....
Tanzania suala la Mahakama kuna uozo sana...sana tena
Kumbuka Mahakama ni Mwajiriwa wa Serekali Mahakimu Majaji wote wapo chini ya Serekali sasa hapo Mahakama ataiambia nini Serekali? Serekali ndio inaamua kipi kiwe na kipi kisiwe kwa hio Mahakama kwa Serekali ni kobogoyo hawezi kutafuna mfupa

Usisahau ni Simu moja tu
 
Paul Makonda, Mwenezi wa CCM akiwa anazunguka nchi nzima kwa misafara mirefu kuliko kiongzi yeyote na kusikiliza kero na kuwalalamikia CCM wenzake kwa kutofanya kazi .
Mwanzo alianza na kulalamikia CHADEMA, AKAJA KWA MBOWE SASA wana CCM wenzie.

Makonda amewaambia wananchi na kuwaagiza wasipeleke kesi mahakmani kwakuwa hawana hela kama yeye ili kununua haki na kwamba hata yeye alidhulumiwa nyumba masaki lakini akaona asiende mahakamani maana hatapata haki.
Juzi hapa Makonda alielimishwa na Mh AG Eliezer Feleshi ambaye kama watu hawajui FELESHI ndiye Mshauri mkuu wa Nchi ya Tanzania.
Sasa Makonda kampanda kichwani, Mahalkama na AG, wamekaa kimya.

Hii kauli ya Makonda tunaweza kuitazama kwa angle nyingi lakini inauvua nguo mfumo wa haki nchini. Na unfortunately ni kauli ya kweli kabisa. Ndio, ni kauli ngumu lakini inaakisi tatizo la mfumo wetu wa utoaji haki.
Anachosema Makonda ni kuwa bila kuwa na pesa na connection, sahau HAKI. Ninachopingana na Makonda ni kuwa haki ipo serikalini, hii sio kweli. Wala serikali sio chombo cha kutoa haki, chombo cha haki ni mahakama/judiciary. Ni muhimili unaojitegemea. Tunahitaji kujenga mfumo wa mahakama ulio huru na unaosimamia kweli na usioegemea upande wowote. Rostam Aziz alisema kuhusu Mfumo wa mahakama kuwa umeoza akaambiwa akanushe Chap Sasa Mwenezi anaonesha panapovuja na ndio Uhalisia
Mfumo ambao haki siyo upendeleo bali ni fursa inayoweza kupatikana na kila mtu. Ni muhimu sasa, zaidi ya wakati wowote, kutafuta suluhu na kufanya mahakama zetu kuwa huru.Mbona Kenya wanaweza? Hawa si ni wenzetu tu wa eneo hili la Afrika mashariki? Makonda anasema mfumo wetu wa utoaji haki umeoza, inawezekana ni kweli. Basi turekebishe huo mfumo, tusiukimbie na kutengeneza mfumo mwingine. Hiyo sio solution.

Tupende tusipende, Makonda amesema kweli. Na ajiandae kulipia gharama za kusema ukweli. Sio mahakama tu ambayo mambo hayaeleweki...ni karibu kila eneo. Wamemuacha muheshimiwa afanye kazi peke yake. Very disappointing
 
Kama kazi yake ni kutoa haki halafu hakitoi kina tofauti gani na genge la wahuni?
Kwahiyo kwa akili yako ya huko kihodombi inakutuma kwamba kama mahakama ni chombo cha haki kisipotoa ujichukulie sheria mononi?

Mwanamke mwenzako aliyeibiwa mume , akikuona na kukufananisha akakumwagia maji ukaungua sura na baadae ikaja kugundulika si wewe ila ni pacha wako ni sawa? au ilipaswa akukamate na kukupeleka mahakamani ili ujitetee na haki itendeke?

UVCCM sijui mmekuwaje!
 
Back
Top Bottom