Mchambuzi
JF-Expert Member
- Aug 24, 2007
- 4,850
- 9,405
Imekuwa jadi kwa baadhi ya magazeti yanayotoka Jumatano na Jumapili kuchapisha content nyingi sana kutoka humu JF. Binafsi nimeona content zangu lifted kama zilivyo, neno kwa neno, kwenye matoleo na magazeti kama manne tofauti. Wakishindwa kubadili angalau maneno ili yaendane na mawazo yao, na badala yake kuamua to lift neno kwa neno, ingekuwa jambo la busara sana kama waandishi hawa angalau wangetoa credit kwa jamiiforums, kwani huko ni kujengana kama media platforms. Hawana haja ya kutaja majina ya wachangiaji au watoa mada humu kwani wengi wetu tuna majina ya uongo, lakini angalau watoe credit kwa jamiiforums. Huo ni mtazamo wangu binafsi.