Mafunzo ya JKT kwa kujitolea kwa mwaka 2016

Tuesday, October 25, 2016
Serikali Yakanusha Taarifa Iliyosambaa Katika Mitandao Ya Kijamii Kuwa Itaanza Kutoa Ajira


1.Ipo taarifa inayosambaa katika mitandao ya kijamii ikimnukuu Waziri wa Nchi -Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora) Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb), kuwa Serikali itaanza kutoa ajira, kupandisha Vyeo na kulipa Stahiki mbalimbali za Watumishi wa Umma mwezi Februari, 2017. Chanzo cha habari hiyo ni mtandao wa Jamii Forum kupitia mjadala ulioanzishwa na nkanga chief (JF-Expert Member) na baadaye kusambazwa katika mitandao mingine.

2. Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora inapenda kuwafahamisha Watumishi wa Umma na Umma kwa ujumla kuwa, taarifa hiyo haina ukweli wowote na ina lengo la kuupotosha

Umma. Hivyo watumishi wa umma na wananchi kwa ujumla wanaombwa kuipuuza taarifa hiyo na kuendelea na majukumu yao kama kawaida.


3.Serikali inasisitiza kuwa, suala la Ajira mpya na upandishaji Vyeo litafanyika kwa kuzingatia Bajeti ya Serikali ya Mwaka wa Fedha 2016/17. Malipo ya stahili za watumishi wa umma yatafanywa na Serikali kwa kuzingatia, Sheria, Kanuni na Taratibu zilizopo.

4. Ikumbukwe, Serikali ina utaratibu maalum wa kutoa taarifa kwa Umma, hivyo Serikali itatoa taarifa rasmi kwa Umma kupitia mamlaka husika.

5. Serikali kupitia taarifa hii inawaasa wananchi kuacha tabia ya kusambaza habari za uongo au zisizothibitishwa dhidi yake. Serikali haitasita kuwachukulia hatua za kisheria wale wote watakaobainika kuzusha na kusambaza habari za upotoshaji kuhusu shughuli za Serikali.
 
we huoni hyo barua ni page 1....ulitakiwa uulize page 2 ikwapi na sio kusema hyo taarifa ni uongo...[/QUOTE
toka lini barua ikawa na page mbili, eti barua ina namba 1,2,3 Braza usichanganye na watu huyo n Nkanga kaamua kubadili umbo na kuggbu hata sekretarieti ya ajira ilitangazo halipo.
 
shidah ya mleta uzi wa mara ya kwanza ambaye n Nkanga aliweka muda karibu sana et february so akaona aje atengue kauli yake coz mambo ni hadi june baada ya budget
My take Serikali haina pesa hadi kupelekea wauguzi kugoma kutokana na kutolipwa mishahara yao mienzi miwili
 
shidah ya mleta uzi wa mara ya kwanza ambaye n Nkanga aliweka muda karibu sana et february so akaona aje atengue kauli yake coz mambo ni hadi june baada ya budget
My take Serikali haina pesa hadi kupelekea wauguzi kugoma kutokana na kutolipwa mishahara yao mienzi miwili
Hii taarifa ya wauguzi source yake mkuu. Maana inatisha..
 
wanajukwaa mwenye ronja mambo yataipa lini maana dah
Mkuuu had Leo bado unataka matumaini!!!chakufanya fanya ya kufanya maana humu hakuna Mwenye jibu...ukiona analo basi sio habari tena kwamaana hata wewe utakua ushajua.ushauri Kula,kazi,pumzika.
 
Back
Top Bottom