EMT
Platinum Member
- Jan 13, 2010
- 14,483
- 15,308
*Fedha anazolipwa mkandarasi zazidi za mradi
*Wananchi wakasirika, wataka kuandamana
Na Victor Bariety, Geita
UCHAMBUZI wa bajeti ya Halmashauri ya Wilaya ya Geita mkoani Mwanza uliofanywa na diwani wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), umewaliza baadhi ya wananchi waliohudhuria mkutano wa hadhara, mwishoni mwa wiki. Aidha, kundi kubwa la wananchi walioonekana kujawa na hasira waliamua kuondoka mkutanoni kwa kile walichosema kwamba wasingependa kuendelea kusikiliza mambo yanayowaumiza roho, yakiwamo ya makandarasi kulipwa fedha nyingi kuliko miradi wanayosimamia.
Uchambuzi huo ulifanywa na Diwani wa Kalangalala, Peter Donald, katika mkutano ulioandaliwa mahsusi kwa ajili ya kueleza sababu za madiwani wa Chadema kususa kikao cha kupitisha bajeti ya Halmashauri ya Wilaya ya Geita. Bajeti hiyo ya mwaka wa fedha wa 2011/2012 inadaiwa kupitishwa kibabe na Baraza la Madiwani wa Halmashauri hiyo Aprili 29, mwaka huu.
Mkutano huo ambao ni uzinduzi wa mikutano mingine inayotarajiwa kufanywa na madiwani wanane wa Chadema wilayani Geita, ulilenga kuwaeleza wananchi ufisadi uliopitishwa na madiwani wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) chini ya Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita, Joseph Musukuma.
Akihutubia maelfu ya wananchi katika Stendi ya Zamani mjini Geita, Donald, alichambua bajeti hiyo na kusema Musukuma aliamua kuvunja kanuni namba 5 na 7 za halmashauri ya wilaya hiyo chini ya kifungu namba 70 ya sheria namba 7 ya mwaka 1982 zinazoongoza halmashauri, mamlaka za miji na Serikali za Mitaa na kuamua kupitisha bajeti hiyo kibabe kwa kutumia wingi wa madiwani wa CCM.
Ndugu zangu, mimi siyo msomi sana, lakini ninavyoelewa mimi makadirio ya mradi mkandarasi anapaswa alipwe asilimia 10 kwa fedha ya mradi husika na si kulipwa mara tatu ya fedha ya mradi. Baada ya kusoma kwenye makabrasha tuliyopewa na kugundua uozo kama huo tuliamua kususia kikao hicho maana nafsi zetu zilitusuta na leo nitawaeleza yote yaliyomo kwenye bajeti hii ndugu zangu hii bajeti ni janga la kitaifa na ni aibu kwa Taifa zima, alisema diwani huyo.
Alisema wajumbe walipaswa kupata kumbukumbu za mkutano kabla ya siku saba, lakini kwa sababu wasizozijua walipata siku mbili kabla ya kikao, jambo ambalo ni kinyume cha kanuni. Alisema pamoja na asilimia 71 ya bajeti ya mwaka wa fedha wa 2011/2012 ya Sh 52,392,638,777 iliyoidhinishwa na Baraza hilo kwenda kwenye matumizi mengineo, kiasi kidogo cha fedha ndicho kimetengwa kwa shughuli za maendeleo; jambo alilosema ni wizi.
Alisema miradi ya machinjio na ujenzi wa soko la kisasa fedha zilizotengwa kwa ajili ya malipo ya makandarasi zinazidi gharama za miradi, huku mkandarasi wa mradi wa kuboresha miundombinu ya maji mijini na vijijini akitengewa asilimia 10 pekee ya malipo ya mradi huo. Hebu mjiulize ndugu wananchi, mradi wa machinjio ya kisasa ambayo ni pesa kutoka Mfuko wa Maendeleo (CDG) umetengewa Sh milioni 100, malipo ya mkandarasi ni Sh milioni 398.311, mradi wa ujenzi wa soko umetengewa Sh milioni 100, huku mkandarasi akitengewa Sh milioni 441.487. Huu siyo wizi? Alihoji.
Aliongeza, Mradi wa kuboresha miundombinu ya maji mijini na vijijini umetengewa Sh bilioni 2.573, mkandarasi yeye ametengewa Sh 179,175,600, sasa najiuliza huyu mkandarasi kwa nini yeye alipwe asilimia chache na wengine walipwe kubwa kama si kutaka kuwaibia wananchi? Baadhi ya wananchi walishindwa kujizuia na kujikuta wakitokwa machozi, huku wengine wakitaka yaandaliwe maandamano kulaani ufujaji huo wa fedha.
Awali, akifungua mkutano huo, Mwenyekiti wa Chadema Wilaya ya Geita, Mabula Kachoji, aliwataka wananchi kubadilika kwa kuikataa CCM kwa kile alichodai watu walewale, sera zilezile na mikakati ile ile tangu Uhuru mwaka 1961 hawawezi kuleta maendeleo.
Ufisadi mpya waanikwa
*Wananchi wakasirika, wataka kuandamana
Na Victor Bariety, Geita
UCHAMBUZI wa bajeti ya Halmashauri ya Wilaya ya Geita mkoani Mwanza uliofanywa na diwani wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), umewaliza baadhi ya wananchi waliohudhuria mkutano wa hadhara, mwishoni mwa wiki. Aidha, kundi kubwa la wananchi walioonekana kujawa na hasira waliamua kuondoka mkutanoni kwa kile walichosema kwamba wasingependa kuendelea kusikiliza mambo yanayowaumiza roho, yakiwamo ya makandarasi kulipwa fedha nyingi kuliko miradi wanayosimamia.
Uchambuzi huo ulifanywa na Diwani wa Kalangalala, Peter Donald, katika mkutano ulioandaliwa mahsusi kwa ajili ya kueleza sababu za madiwani wa Chadema kususa kikao cha kupitisha bajeti ya Halmashauri ya Wilaya ya Geita. Bajeti hiyo ya mwaka wa fedha wa 2011/2012 inadaiwa kupitishwa kibabe na Baraza la Madiwani wa Halmashauri hiyo Aprili 29, mwaka huu.
Mkutano huo ambao ni uzinduzi wa mikutano mingine inayotarajiwa kufanywa na madiwani wanane wa Chadema wilayani Geita, ulilenga kuwaeleza wananchi ufisadi uliopitishwa na madiwani wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) chini ya Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita, Joseph Musukuma.
Akihutubia maelfu ya wananchi katika Stendi ya Zamani mjini Geita, Donald, alichambua bajeti hiyo na kusema Musukuma aliamua kuvunja kanuni namba 5 na 7 za halmashauri ya wilaya hiyo chini ya kifungu namba 70 ya sheria namba 7 ya mwaka 1982 zinazoongoza halmashauri, mamlaka za miji na Serikali za Mitaa na kuamua kupitisha bajeti hiyo kibabe kwa kutumia wingi wa madiwani wa CCM.
Ndugu zangu, mimi siyo msomi sana, lakini ninavyoelewa mimi makadirio ya mradi mkandarasi anapaswa alipwe asilimia 10 kwa fedha ya mradi husika na si kulipwa mara tatu ya fedha ya mradi. Baada ya kusoma kwenye makabrasha tuliyopewa na kugundua uozo kama huo tuliamua kususia kikao hicho maana nafsi zetu zilitusuta na leo nitawaeleza yote yaliyomo kwenye bajeti hii ndugu zangu hii bajeti ni janga la kitaifa na ni aibu kwa Taifa zima, alisema diwani huyo.
Alisema wajumbe walipaswa kupata kumbukumbu za mkutano kabla ya siku saba, lakini kwa sababu wasizozijua walipata siku mbili kabla ya kikao, jambo ambalo ni kinyume cha kanuni. Alisema pamoja na asilimia 71 ya bajeti ya mwaka wa fedha wa 2011/2012 ya Sh 52,392,638,777 iliyoidhinishwa na Baraza hilo kwenda kwenye matumizi mengineo, kiasi kidogo cha fedha ndicho kimetengwa kwa shughuli za maendeleo; jambo alilosema ni wizi.
Alisema miradi ya machinjio na ujenzi wa soko la kisasa fedha zilizotengwa kwa ajili ya malipo ya makandarasi zinazidi gharama za miradi, huku mkandarasi wa mradi wa kuboresha miundombinu ya maji mijini na vijijini akitengewa asilimia 10 pekee ya malipo ya mradi huo. Hebu mjiulize ndugu wananchi, mradi wa machinjio ya kisasa ambayo ni pesa kutoka Mfuko wa Maendeleo (CDG) umetengewa Sh milioni 100, malipo ya mkandarasi ni Sh milioni 398.311, mradi wa ujenzi wa soko umetengewa Sh milioni 100, huku mkandarasi akitengewa Sh milioni 441.487. Huu siyo wizi? Alihoji.
Aliongeza, Mradi wa kuboresha miundombinu ya maji mijini na vijijini umetengewa Sh bilioni 2.573, mkandarasi yeye ametengewa Sh 179,175,600, sasa najiuliza huyu mkandarasi kwa nini yeye alipwe asilimia chache na wengine walipwe kubwa kama si kutaka kuwaibia wananchi? Baadhi ya wananchi walishindwa kujizuia na kujikuta wakitokwa machozi, huku wengine wakitaka yaandaliwe maandamano kulaani ufujaji huo wa fedha.
Awali, akifungua mkutano huo, Mwenyekiti wa Chadema Wilaya ya Geita, Mabula Kachoji, aliwataka wananchi kubadilika kwa kuikataa CCM kwa kile alichodai watu walewale, sera zilezile na mikakati ile ile tangu Uhuru mwaka 1961 hawawezi kuleta maendeleo.
Ufisadi mpya waanikwa