tatanyengo
JF-Expert Member
- Mar 30, 2011
- 1,134
- 280
Hivi karibuni Mkuu wa mkoa wa kilimanjaro Leonidas Gama alisitisha safari ya Kigari, Rwanda ya madiwani wa Hamashauri ya Moshi.Hilo limeungwa mkono pia na Waziri wa Nishati na Madini Prof. Muhongo Kwa hoja kwamba kiasi cha fedha ambacho kingetumika (Tsh 200) ni kikubwa ambacho kingetumika hata kuweka umeme katika shule zote za sekandari katika manipsaa hiyo.
Safari hiyo ya Kigari ilitarajiwa kufanyika kati ya tarehe 15/9/2012 hadi 20/9/2012 na ingewahusisha watumishi 57 lengo kuu lilikuwa kwenda kujifunza usafi. Mwaka jana wa fedha bajeti ya manispaa ya Moshi ilipungua kwa asilmia 40 na haijulikani mwaka huu itapungua kwa kiasi gani.
Maoni yangu.
1). Kama safari ilikuwa ni ya muhimu idadi ya wana msafara ingeweza kupungua ili kupunguza gharama - watu 57 ni wengi mno. Baada ya safari wachache hao wangeweza kurudi na kuwafundisha wenzao kuhusu masuala ya usafi.
2). Suala la usafi ni muhimu lakini siyo lazima twende tukajifunze nje ya nchi namna ya kufanya usafi.
3). Viongozi wetu wajifunze kuweka vipao mbele na kujali zaidi maendeleo ya wanachi kuliko maslahi binafsi.
Safari hiyo ya Kigari ilitarajiwa kufanyika kati ya tarehe 15/9/2012 hadi 20/9/2012 na ingewahusisha watumishi 57 lengo kuu lilikuwa kwenda kujifunza usafi. Mwaka jana wa fedha bajeti ya manispaa ya Moshi ilipungua kwa asilmia 40 na haijulikani mwaka huu itapungua kwa kiasi gani.
Maoni yangu.
1). Kama safari ilikuwa ni ya muhimu idadi ya wana msafara ingeweza kupungua ili kupunguza gharama - watu 57 ni wengi mno. Baada ya safari wachache hao wangeweza kurudi na kuwafundisha wenzao kuhusu masuala ya usafi.
2). Suala la usafi ni muhimu lakini siyo lazima twende tukajifunze nje ya nchi namna ya kufanya usafi.
3). Viongozi wetu wajifunze kuweka vipao mbele na kujali zaidi maendeleo ya wanachi kuliko maslahi binafsi.