Madaktari wasema Zitto alisumbuliwa na kuchafuka tumbo

Na waandishi wetu Fredy Azzah na Fidelis Butahe
MBUNGE wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe ambaye jana aliruhusiwa kutoka katika Hospitali ya Aga Khan ya jijini Dar es Salaam alikolazwa kwa matibabu ya tumbo amedai kuwa matatizo hayo aliyapata baada ya kula chakula chenye sumu.“Namshukuru Mungu naendelea vizuri na nimesharuhusiwa kutoka hospitali, madaktari wameniambia ilikuwa food poisoning (chakula chenye sumu),” alisema Zitto.

Zitto ambaye hakuweza kueleza chakula hicho alikuwa wapi na kina sumu ya aina gani, alisema kuwa baada ya kugundua tatizo hilo, madaktari walimtaka kuwa makini na vyakula anavyokula.

“Sumu gani nimekula na ni wapi, mimi nadhani sio story (habari). Cha msingi kwa sasa naendelea vizuri na nimetakiwa kuwa makini na vyakula ninavyokula,” alisema Zitto.

Hata hivyo, kauli hiyo ya Zitto inapingana na madaktari wake waliosema kuwa mbunge huyo kupitia tiketi ya Chadema, alikuwa anasumbuliwa na mchafuko wa kawaida wa tumbo.

“Alikuwa anasumbuliwa na Gastro enteritis (mchafuko wa tumbo), tatizo hili linaweza kusababishwa na bacteria, virusi katika chakula, au kama chakula hakijapikwa vizuri,” alisema Dk Mustafa Bapumia.

Zitto alilazwa hospitalini hapo tangu Disemba 9 mwaka huu saa 3:00 usiku, baada ya kutoka kwenye mkutano wa ndani wa chama chake uliofanyika Bagamoyo mkoani Pwani ambako alivuliwa cheo cha Naibu Kiongozi wa Kambi ya upinzani bungeni.

Kuhusu hatua ya chama hicho kumvua Zitto wadhifa wake wa unaibu kiongozi wa upinzani bungeni, alisema kwa sasa bado hawezi kuzungumzia suala hilo kwa sababu hajapata taarifa rasmi kutoka chama chake mbali na kusoma suala hilo kwenye vyombo vya habari.

Hata hivyo, alieleza hakuwahi kuomba kupewa wadhifa huo, kwa hiyo endapo watu waliomwona anafaa kufanya kazi na kumpa wadhifa huo, wakiamua kumnyang’anya siyo tatizo kubwa kwake.

“Kwa sasa nadhani suala la afya yangu ndiyo muhimu zaidi. Ngoja kwanza nitoke hapa na afya yangu iimarike na kama kutakuwa kuna sababu ya mimi kuzungumza nitazungumza,” alisema Zitto:

“Lakini ikumbukwe kuwa mimi sikuwahi kuomba wadhifa huu…, kwa hiyo kama watu walionipa wameamua kunibadilishia, mimi sidhani kama kuna tatizo.”

Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe aliupolizwa na Mwananchi Jumapili juu ya Zitto kuvuliwa uongozi bungeni alisema kuwa chama kitatoa taarifa baadaye.



Source : Mwananchi

Mijitu mingine bana! Jitu lina kipindupindu linasema sumu!
 
gastroenteritis

gastroenteritis overview
gastroenteritis (also known as gastric flu or stomach flu, although unrelated to influenza) is inflammation of the gastrointestinal tract, involving both the stomach and the small intestine and resulting in acute diarrhea. It can be transferred by contact with contaminated food and water.

gastroenteritis causes
the inflammation is caused most often by an infection from certain viruses or less often by bacteria, their toxins, parasites, or an adverse reaction to something in the diet
many people who experience the vomiting and diarrhea that develop from these types of infections or irritations think they have "food poisoning," which they may, or call it "stomach flu,"
travelers to foreign countries or country side may experience "traveler's diarrhea" from contaminated food and unclean water.
Improper hand washing following a bowel movement or handling a diaper can spread the disease from person to person.
Gastroenteritis caused by viruses may last 1-2 days. On the other hand, bacterial cases can last a week or more.

prevention of gastroenteritis.
the best ways to prevent gastroenteritis are;


  • to always wash your hands with soap after going to the toilet and to disinfect toilets after use. It's also important to practice good food hygiene.



  • make sure you have any necessary vaccinations before you travel to other countries and drink bottled water (not tape water) where necessary when abroad.

source :internet

ni kipindupindu sio sumu
 
Gastroenteritis

Gastroenteritis Overview
Gastroenteritis (also known as gastric flu or stomach flu, although unrelated to influenza) is inflammation of the gastrointestinal tract, involving both the stomach and the small intestine and resulting in acute diarrhea. It can be transferred by contact with contaminated food and water.

Gastroenteritis Causes
The inflammation is caused most often by an infection from certain viruses or less often by bacteria, their toxins, parasites, or an adverse reaction to something in the diet
Many people who experience the vomiting and diarrhea that develop from these types of infections or irritations think they have "food poisoning," which they may, or call it "stomach flu,"
Travelers to foreign countries or country side may experience "traveler's diarrhea" from contaminated food and unclean water.
Improper hand washing following a bowel movement or handling a diaper can spread the disease from person to person.
Gastroenteritis caused by viruses may last 1-2 days. On the other hand, bacterial cases can last a week or more.

Prevention of gastroenteritis.
The best ways to prevent gastroenteritis are;


  • To always wash your hands with soap after going to the toilet and to disinfect toilets after use. It's also important to practice good food hygiene.



  • Make sure you have any necessary vaccinations before you travel to other countries and drink bottled water (not tape water) where necessary when abroad.

Source :Internet

Nimeipenda hii prevention of gastroenteritis.
 
Haikuwa tishio kwa maisha, kwa vile siyo sumu ya kupewa. otherwise, chadema malizeni ugomvi wenu wa ndani
 
Na waandishi wetu Fredy Azzah na Fidelis Butahe
MBUNGE wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe ambaye jana aliruhusiwa kutoka katika Hospitali ya Aga Khan ya jijini Dar es Salaam alikolazwa kwa matibabu ya tumbo amedai kuwa matatizo hayo aliyapata baada ya kula chakula chenye sumu."Namshukuru Mungu naendelea vizuri na nimesharuhusiwa kutoka hospitali, madaktari wameniambia ilikuwa food poisoning (chakula chenye sumu)," alisema Zitto.

Zitto ambaye hakuweza kueleza chakula hicho alikuwa wapi na kina sumu ya aina gani, alisema kuwa baada ya kugundua tatizo hilo, madaktari walimtaka kuwa makini na vyakula anavyokula.

"Sumu gani nimekula na ni wapi, mimi nadhani sio story (habari). Cha msingi kwa sasa naendelea vizuri na nimetakiwa kuwa makini na vyakula ninavyokula," alisema Zitto.

Hata hivyo, kauli hiyo ya Zitto inapingana na madaktari wake waliosema kuwa mbunge huyo kupitia tiketi ya Chadema, alikuwa anasumbuliwa na mchafuko wa kawaida wa tumbo.

"Alikuwa anasumbuliwa na Gastro enteritis (mchafuko wa tumbo), tatizo hili linaweza kusababishwa na bacteria, virusi katika chakula, au kama chakula hakijapikwa vizuri," alisema Dk Mustafa Bapumia.

Zitto alilazwa hospitalini hapo tangu Disemba 9 mwaka huu saa 3:00 usiku, baada ya kutoka kwenye mkutano wa ndani wa chama chake uliofanyika Bagamoyo mkoani Pwani ambako alivuliwa cheo cha Naibu Kiongozi wa Kambi ya upinzani bungeni.

Kuhusu hatua ya chama hicho kumvua Zitto wadhifa wake wa unaibu kiongozi wa upinzani bungeni, alisema kwa sasa bado hawezi kuzungumzia suala hilo kwa sababu hajapata taarifa rasmi kutoka chama chake mbali na kusoma suala hilo kwenye vyombo vya habari.

Hata hivyo, alieleza hakuwahi kuomba kupewa wadhifa huo, kwa hiyo endapo watu waliomwona anafaa kufanya kazi na kumpa wadhifa huo, wakiamua kumnyang'anya siyo tatizo kubwa kwake.

"Kwa sasa nadhani suala la afya yangu ndiyo muhimu zaidi. Ngoja kwanza nitoke hapa na afya yangu iimarike na kama kutakuwa kuna sababu ya mimi kuzungumza nitazungumza," alisema Zitto:

"Lakini ikumbukwe kuwa mimi sikuwahi kuomba wadhifa huu…, kwa hiyo kama watu walionipa wameamua kunibadilishia, mimi sidhani kama kuna tatizo."

Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe aliupolizwa na Mwananchi Jumapili juu ya Zitto kuvuliwa uongozi bungeni alisema kuwa chama kitatoa taarifa baadaye.



Source : Mwananchi

Nahisi Zito alikuwa tayari na mawazo ya kuwekewa sumu. Lakini ukweli ni kama alivyoeleza daktari. Ni jambo ambalo wengi tunakutana nalo ila huwa hatujui. Mathalani ni mara nyingi watu huwa anakula au kuchwa mara ghafla anapatwa na tumbu la kuhara au kuuma. Hiyo huwa ni food poisoning. Na hii ni sumu inatolewa/tengenezwa na bakteria wanaokuwa kwenye chakula kutokana na sababu mbali mbali ikiwemo mazingira yakuandalia chakula kutokuwa ya usafi wa hali ya juu, wahudumu au chakula hakikupata joto la kutosha n.k. Kwa hiyo zito aondoe kabisa wazo la kulishwa sumu. Sisi wataalam wa chakula haliyo ndo tunaiita foood poisoning.
 
Magazeti mnapotosha jamii tafakarini na kufanya uchunguzi wa kutosha kabla ya kuandika mambo yatakayojenga jamii na si kubomoa. Msiandike ilimradi muuze gazeti
 
Kauli hii ya Zitto inatia mashaka juu ya uwezo wake wa kufikiri kwa sababu hakuna uhusiano wowote ule wa ununuzi wa mitambo chakavu ya DOWANS na ile kesi...................................

TANESCO hawakuwa na ugomvi wowote ule na DOWANS baada ya kumalizika kwa mkataba wao sasa TANESCO ilitoka wapi kukimbilia mahakamani kuizuia DOWANS wasiondoke na mitambo yao?

Waliokuwa na mgogoro na DOWANS walikuwa ni TRA mbona TANESCO hawakuwaacha TRA kuzuia ile mitambo tajwa kwa minajili ya kudai fidia ya kodi yao ya karibu bilioni 9 waliokuwa wanawadai DOWANS?

TANESCO kuzuia mitambo ya DOWANS ulikuwa ni ufisadi ulioihusisha Mahakama Kuu yetu kwa sababu ni uzandiki kwa Mahakama kuafiki hoja za TANESCO wakati DOWANS walikuwa hawajakiuka mkataba wowote ule na TANESCO.......................

Yaelekea hivi sasa ZITTO hatupo kundi moja kwenye vita dhidi ya ufisadi.........mafisadi wamekwisha kumnunua ila sijui kwa bei ipi?

Tatizo ni kuwa hakuna aliye katika vita ya ufisadi isipokuwa MAFISADI WASIOVUMA wanapambana na MAFISADI WALIOKUBUHU...na sio kila mtu anayetaka kuwa bendera fuata upepo.......
 
Wewe una akili kweli au unaropoka ropoka tu kama umekunywa mataputapu eti hakuna kiongozi wa CDM aliyekwenda unajua kina nani walimpeleka hospitalini kama hujui kitu nibora ukauliza.

Ni kiongozi yupi wa Chadema aliyempeleka hospitali zaidi ya kupitia walipotoka Kempiski kusheherekea "ushindi" na sura zao zilizokosa aibu wala ubinadamu?

Yaani Makamu Mwenyekiti Said Arfi analazwa muda wa siku nne inachukua Waziri Mkuu Pinda kuja mara mbili na kumfanyia mpango wa matibabu halafu viongozi wako ndio wanajipitisha muda masaa machache baada ya kujua kuwa anasafirishwa kwenda nje kutibiwa bila hata kutaka kujulia gharama zozote wakati huohuo wanajiaanda kutumia mamilioni mengine kufanya SHEREHE nyingine ya kujipongeza punde tu baada ya kumtuhumu na kumhukumu na kuwaita Mbuzi bila ya yeye (wao) kuwepo kujitetea halafu mnaongelea demokrasia ama kupigani katiba msiyoweza hata kufuata ya kwenu?

Hizi siasa za chuki mnazotegemea kuwa ndiyo mbinu bora ya kuwaondoa CCM na wale wasiokubaliana na siasa mediocre zenu ni wazi zimeanza kuwaathiri ninyi kuliko hata hao mnaowakusudia.....Chuki zimewajaa hadi simple imani ya UTU acha ile ya uwanademokraisa imewashinda halafu mnataka kujifaragua kuwa mna imani na watanzania????

Thanks GOD kwa kutufungua macho na kuona yaliyomo ndani ya mioyo yenu hata kabla watanzania hawajafanya kosa la kuwakumbatia....
 
Back
Top Bottom