Elections 2010 Machozi ndani ya daladala

Mubezi

Member
Sep 27, 2010
71
23
Nikiwa kati ya WATU waliohudhuria mikutano ya kampeni hasa ya urais,nimeona mengi,nimesikia mengi,ahadi kemkem,tam,nzuri na zenye kuvutia na kama JK,SLAA au LIPUMBA mmoja wo akishinda na kutekeleza ahadi zake basi TANZANIA itakuwa kama Boswana au kama sio kuifikia Afica kusini. Sina sababu ya kuzitaja ahadi kwani wengi wenu mwazijua.

Ni saa 12:30 za jioni siku ya ijumaa,natoka ofisini kwangu JMOO nakwenda posta ili kupanda gari la kuelekea mbezi nyumbani kwangu(mbezi ya kimara).Abiria ni wengi kama kawaida,wezi wamo,ila kuna magari ya kwenda mbezi ya buku(elfu moja) naingia na muda si mrefu gari inajaa na kuondoka,wote tumekaa,foleni ni kama kawaida kwani inaanzia faya na uku gari ikiwa imewekwa radio moja ya chama tawala.Watu tupo kimya na aliyesimama ni konda tu.

Mara hiyo radio ikaanza kutangaza sera za mgombea uras wa chama tawala,ahadi nyingi,kile mara iki najua mwazijua sina shida ya kuzitaja ila ni moja tu ambayo nitaitaja ambayo imenipelekea kuandika UJUMBE huu kwenu,ni ile ya KUNUNUA BAJAJI 40 KWA WAMAMA WAJAWAZITO,hapo ni saa 1:30 za jioni na hatujavuka magomeni.

Mara baada ya huyo mgombea kutaja iyo ahadi,nikasikia sauti kuoka nyuma ya gari ikisema “ZIMA RADIO YAKO AU BADILISHA STESHENI”ni sauti ya kike tena mwanamama mjamzito.Dereva alizima radio,tukawa kimya kila mtu nahisi alikuwa anajiuliza kwanini huyu mama kasema radio izimwe au ibadilishe stesheni,ukimya ulitawala kama dk 15.Tukiwa tunaanza foleni ya ubungo pale mahakama ya ndizi au bigbrother, na ikiwa ni saa 2:07 za usiku,nikasikia sauti ya mwanamama mwingine(sio mjamzito) ikisema “KAMA MIMBA ZINGEKUWA ZINABEBWA KWA ZAM HUYU KIKWETE ASINGETAMKA MANENO HAYO”nikashtuka nikageuka nyuma nikakutana uso kwa uso na yule mama mwenye mimba,mimba yake ilikuwa ni kama ya miezi nane tena ilikuwa kubwa(namaanisha tumbo ni kubwa sana).

Tukiwa tupo stand ya mkoa na gari likiwa limesimama na ni saa 2:45 usiku kumbuka nimetoka posta saa 12:30 za jioni.Yule mama mjamzito akasimama akaanza kusema “MIMI SITOMPA KURA KIKWETE KWA JAMBO ILI,NILIKUWA NIMPE ILA KWA JAMBO KAMA ILI SIWEZI KUMPA”uku akilia na kutokwa na machozi,yule mama mwingine aliyesema “kama mimba zingekuwa zinabebwa kwa zam huyu kikwete asingetamka maneno hayo” akaanza kumbembeleza yule mama mjamzito akimsii akae.Nilimtazama kila mtu ndani ya gari sura zilibadilika zikawa sura za majonzi.

Nikatoka kwenye daladala(kimawazo) nikaleta taswila ya BAJAJI nikamuweka yule mama nyuma na mimi nikawa dereva,nikafikiria umbali wa kilometa 50 toka kijijini kwetu kule kanyigo kuja hospital,barabara imejaa mashimo,nikawaza tumbo la yule mama akiwa yuma na uchungu na babaji ikiwa inayumba kwenye mabonde ya barabara,”NILILIA” nilishutushwa na honi nyingi za magari ambazo zilikuwa zikilipigia daladal letu kwa kutotembea, kwani kila mtu alikuwa kwenye mawazo ya yule mama(naisi) na dereva alijisahau kwa kumuonea huruma yule mama.Nilikuwa karibu na dereva nikamuuliza vp?,akajibu “WE ACHA TU”uku akitoa leso na kufuta machozi na kuanza kuendesha gari.

Ni saa 3:07 usiku tupo kimara tunaanza foleni ya kimara stopover,watu wote wapo kimya akuna aliyeshuka mpaka sasa na konda kaka kwenye mlango ameinama,kila mtu kainama,uku wengine wakivuta mafua,na yule mama mjamzito akionekana ana asira na uku machozi yakimtoka yenyewe.Nikajiuliza ina maana watu wote tunakwenda mbezi?,pia huyu mama vp mbona kabadilisha kila mtu ndani ya daladala? Katumwa nini?.Nikasikia sauti ya baba mmoja kutoka katikakti ya gari akisema shusha konda hapo,konda akasema wapi?,baba akajibu hapo hapo,Mmmmmmmmm?,”Samahani konda nilikuwa nashuka bucha nimejisahau” alisikika yule baba akisema,Mmmmmmmmm?.Ndipo nilipoona kila mtu karudi katika hari yake ya kawaida na wengine wakashuka hapo kama watu sita hivi.Nikajiuliza je walikuwa wanawaza nini? Mpaka wapitishwe kituoni?.Je walikuwa katika taswila kama yangu?,au uchovu wa kazi?

Kati ya wale walioshuka pale njiani(sio kituoni) baba mmoja akasema akimwambia yule mama mjamzito “POLE SANA MAMA NA MIMI NAKUHAIDI SITOMPA KURA KIKWETE”akatelemaka.Tunavuka stopover na ni saa 3:30 usiku,kila mtu kaanza kusema lake”KIKWETE HANA AKILI”alisikika baba mmoja,”KIKWETE NI MGONJWA” alisikika dada mmoja,”WANAIGEIZA NCHI YA FAMILIA KWANI HAPA TUNATAWALIWA KIFALME” alisikika kaka mmoja.Ni saa 3:45 nashuka kibanda cha mkaa na niliposimama nikwaambia abilia “HUYO NDIO RAIS WENU HATA KIWA CHIZI SI MLIMCHAGU WENYEWE” nikajibiwa na konda “SHUKA UKO NA NENDA ZAKO”,Mmmmmmmm ata konda?

Nikiwa njiani nakwenda kwangu nikawa natafakari “JE YALE MACHOZI YA MAJI YALIYONDONDOKA NDANI YA DALADALA LEO”je ni ya bure tu?,na je “IPO SIKU YATALIPWA”?,na je “IPO SIKU YATAGEUKA KUWA NI MACHOZI YA DAM”? nisingependa ilo tafakari langu la mwisho litokee.

Je wewe unatoa machozi gani au maneno agani?,je machozi ya furaha? Au ya uzuni kama yule mama mjamzito?au maneno ya kumtukana rais wako kama wale watu kwenye daladala.Kazi kwako. Nikipata nauli kabla ya UCHAGUZI nitakwenda kanyigo nimuulize babu “JE BABU UMESHAWAI KUONA KICHUGUU CHA SENENE”?.
 
Wakati yeye anatembela V8 wateja wake anataka watembelee BAJAJ what a shame!
Angalau angesema tutanunua cruza mkonge,BAJAJ si za kwenye rami tuu
 
Kati ya wale walioshuka pale njiani(sio kituoni) baba mmoja akasema akimwambia yule mama mjamzito "POLE SANA MAMA NA MIMI NAKUHAIDI SITOMPA KURA KIKWETE"akatelemaka.Tunavuka stopover na ni saa 3:30 usiku,kila mtu kaanza kusema lake"KIKWETE HANA AKILI"alisikika baba mmoja,"KIKWETE NI MGONJWA" alisikika dada mmoja,"WANAIGEIZA NCHI YA FAMILIA KWANI HAPA TUNATAWALIWA KIFALME" alisikika kaka mmoja.Ni saa 3:45 nashuka kibanda cha mkaa na niliposimama nikwaambia abilia "HUYO NDIO RAIS WENU HATA KIWA CHIZI SI MLIMCHAGU WENYEWE" nikajibiwa na konda "SHUKA UKO NA NENDA ZAKO",Mmmmmmmm ata konda?

Nchi nzima ndivyo hivi sasa inavyomwona JK na D-Day atukabidhi nchi yetu bila zengwe
 
Wakati yeye anatembela V8 wateja wake anataka watembelee BAJAJ what a shame!
Angalau angesema tutanunua cruza mkonge,BAJAJ si za kwenye rami tuu
si ndo mnachositahili jamani! mnataka nini tena hadhi yenu ya bajaji tuu!
 
Mara baada ya huyo mgombea kutaja iyo ahadi,nikasikia sauti kuoka nyuma ya gari ikisema "ZIMA RADIO YAKO AU BADILISHA STESHENI"ni sauti ya kike tena mwanamama mjamzito.Dereva alizima radio,tukawa kimya kila mtu nahisi alikuwa anajiuliza kwanini huyu mama kasema radio izimwe au ibadilishe stesheni,ukimya ulitawala kama dk 15.Tukiwa tunaanza foleni ya ubungo pale mahakama ya ndizi au bigbrother, na ikiwa ni saa 2:07 za usiku,nikasikia sauti ya mwanamama mwingine(sio mjamzito) ikisema "KAMA MIMBA ZINGEKUWA ZINABEBWA KWA ZAM HUYU KIKWETE ASINGETAMKA MANENO HAYO"nikashtuka nikageuka nyuma nikakutana uso kwa uso na yule mama mwenye mimba,mimba yake ilikuwa ni kama ya miezi nane tena ilikuwa kubwa(namaanisha tumbo ni kubwa sana).

Tukiwa tupo stand ya mkoa na gari likiwa limesimama na ni saa 2:45 usiku kumbuka nimetoka posta saa 12:30 za jioni.Yule mama mjamzito akasimama akaanza kusema "MIMI SITOMPA KURA KIKWETE KWA JAMBO ILI,NILIKUWA NIMPE ILA KWA JAMBO KAMA ILI SIWEZI KUMPA"uku akilia na kutokwa na machozi,yule mama mwingine aliyesema "kama mimba zingekuwa zinabebwa kwa zam huyu kikwete asingetamka maneno hayo" akaanza kumbembeleza yule mama mjamzito akimsii akae.Nilimtazama kila mtu ndani ya gari sura zilibadilika zikawa sura za majonzi.

So sad...
 
yani mwaka huu...chichiem lazima waibe kura tu!vinginevyo wametolewa nje!!
 
hata mimi machozi yamenidondoka,naahidi sitompa kukwete kura yangu
 
Hata mm simpi kura yangu,nikifikiria kwa undani zaid yani ni unyanyasaji wa kinyinsia yy atembelee v8,mama zake waliomza awape bajaj ni ukatili mbaya sana kweli oct 31 jk imekula kwake
 
Nimekusoma mkuu. Hata mi machozi yamelenga machoni. Lakini nauliza, mbona ile makala yako ya mkutano wa moro na mama wa ndizi ulitumia kiswahili fasaha kuliko makala hii?
 
Am happy that Big percentage of Intellectuals Don't like him.
It has even be proven here. mwenye kutaka proof nitampa
 
Du! Kama move story ila ndo ukweli wenyewe.
Jk kubaki ikulu achakachue tu ila damu ikimwagika kila atapoenda itamfuata.
 
Hivi wajameni mi nilikuwa ninafikiria, mfano tukisema tujitolee kufotokopi hiki kisa ambacho ni cha ukweli kabisa na kusambaza nakala zake bure kwa wasomaji .....itakuwa tumetenda kosa???? ushauri jamani!!!!!!
 
Mubezi,

BIG UP sana kwa simulizi yako nzuri. Pamoja na kero za ahadi za kusimu, hili la kutoka Posta saa 12.30 jioni na unafika nyumbani (umbali usiozidi 30km) saa 4.30 halionekani kuwa ni tatizo ambalo wala halihitaji miujiza kulitatua, kabla ya matuta ya barabara ya morogoro, tulikuwa tunatumia si zaidi ya masaa mawili kutoka posta hadi Kibamba lakini tangu wakati ule sasa tunatumia mpaka masaa matano na katika ahadi zote za kuzimu hii bado si kero na haijaadiwa kutatuliwa
 
nimemfikira huyo mwanamke mwenzangu yupo kwenye foleni muda wote huo mfano tu uchungu ungempata ghafla na hayo mafoleni cjui ingekuwaje, khaa hii nchi inakera kweli, yaani unatoka ofcn saa 1:30 unafika nyumbani 9:45, mtoa thread umeandika kwa hisia kweli...inaumiza sana!
 
kumchagua JK ni kujiwekea laana juu ya nchi kwa niaka mingine mitano.Yeye benz 300ml kwenye lami. mama mjamzito bajaji 2mil. kwenye vumbi+mashimo.
 
Back
Top Bottom