Kyachakiche
JF-Expert Member
- Feb 16, 2009
- 983
- 207
Kuna jambo linalonitatiza kidogo. Jambo lenyewe ni mabati yaliyozungushwa kwenye uwanja mpya wa Taifa tangu kipindi unajengwa hadi sasa wakati ukuta umekwishakujengwa na makabidhiano baina ya serikali ya China na ya Tanzania yameshafanyika karibu mwaka mmoja uliopita. Je, kinachosubiriwa ni nini? Bati zenyewe zimeshakuwa na kutu, zinaharibu mandhari nzuri ya uwanja, na pia si salama wakati wa mkusanyiko wa watu wengi kama jana kwenye mchezo wa Ivory Coast na Tz ambapo kusukumana kulikuwa jambo la kawaida.