Peter Agostino
Senior Member
- Sep 23, 2016
- 105
- 226
Mabasi yaendayo kasi maarufu kama mwendo kasi jijini Dar es salaam yalipoanza rasmi mwezi may mwaka huu kila mtu hususani wakazi wa maeneo ya Kimara na Mbezi alishangilia. Walifahamu sasa shida ya usafiri bye bye. Lakini kadiri siku zinavyozidi kwenda na serikali kutimiza azma yake ya kuziondoa daladala zingine zote ndogo ndivyo shida ya usafiri Mbezi na maeneo ya karibu nayo inavyozidi kuongezeka.
Shida hii inaonekana kuwaathiri zaidi wananchi wa kipato cha chini ambao inakuwa vigumu kuunganisha magari mawili kutokana na nauli kuwa kubwa. Watu walizoea kupanda basi moja kutoka Mbezi mpaka maeneo mengine ya katikati ya jiji ijapokuwa wakati mwingine kwa kusukumana na kusubiri muda mrefu stendi, lakini hilo wala haliwezi kumsumbua mwananchi wa kawaida ambaye kipato chake hakizidi dola 2 kwa siku. Ni bora achelewe kuliko kuteketeza fedha kidogo aliyokuwa nayo mfukoni kwa nauli.
Tatizo linalolalamikiwa na watu wengi wa maeneo haya ni kwamba, asubuhi mtu uwapo tuseme maeneo kama mbezi mwisho, kibanda cha mkaa, Kwa msuguri, Temboni na hata Kimara Suka, huwezi kupata gari kirahisi linalokwenda maeneo ya katikati ya jiji, badala yake unalazimika kupanda daladala ziendazo Kimara mwisho ndipo tena ukachukue Mwendokasi kwa shilingi 650. Bora basi ungepanda hata daladala la kawaida sh 300 mpaka Kimara mwisho, hivi karibuni tena hata hizo daladala hazionekani, unapanda mwendokasi linalotokea Mbezi, unalipa 400 na kisha wanakushusha Mbezi Mwisho unakata tena tikiti ya sh. 650 ili uende unakokwenda.
Watu wengi wanalilia angalao Serikali ingeliona hili na kuamua kati ya mambo haya 3, Magari hayo yasiishie Kimara Mwisho bali yaende mpaka Mbezi mwisho kwa nauli hiyohiyo moja au wapunguze nauli kidogo angalao mtu unapokwenda mjini usitoe zaidiya 1000 kwa safari ya kwenda tu peke yake, na tatu, ikiwezekana daladala za kawaida ziachwe chache ziendelee kufanya kazi kwa ajili ya watu wa hali za chini.
Mama mmoja anayefanya biashara ya kuuza mahindi ya kuchoma alikuwa akilalamika kwa masikitiko akielezea jinsi ambavyo faida yake ya mahindi inavyoishia njiani tofauti na siku za nyuma alipokuwa akipanda daladala za kawaida.
Anasema mahindi huyafuata Tandale akitokea Kimara Matosa na anapofika kituoni Kibanda cha mkaa husimama muda mrefu bila kuona gari mpaka anapoamua kupanda mwendokasi kwa sh.400 hadi Kimara, halafu hapo huchukua tena mwendokasi lingine kwa sh. 650. Anasema kwa siku mpaka anafika Matosa hutumia zaidi ya sh.3,000 pamoja na bajaji kutoka stendi kibanda cha mkaa mpaka anapofanyia biashara yake.
Shida hii inaonekana kuwaathiri zaidi wananchi wa kipato cha chini ambao inakuwa vigumu kuunganisha magari mawili kutokana na nauli kuwa kubwa. Watu walizoea kupanda basi moja kutoka Mbezi mpaka maeneo mengine ya katikati ya jiji ijapokuwa wakati mwingine kwa kusukumana na kusubiri muda mrefu stendi, lakini hilo wala haliwezi kumsumbua mwananchi wa kawaida ambaye kipato chake hakizidi dola 2 kwa siku. Ni bora achelewe kuliko kuteketeza fedha kidogo aliyokuwa nayo mfukoni kwa nauli.
Tatizo linalolalamikiwa na watu wengi wa maeneo haya ni kwamba, asubuhi mtu uwapo tuseme maeneo kama mbezi mwisho, kibanda cha mkaa, Kwa msuguri, Temboni na hata Kimara Suka, huwezi kupata gari kirahisi linalokwenda maeneo ya katikati ya jiji, badala yake unalazimika kupanda daladala ziendazo Kimara mwisho ndipo tena ukachukue Mwendokasi kwa shilingi 650. Bora basi ungepanda hata daladala la kawaida sh 300 mpaka Kimara mwisho, hivi karibuni tena hata hizo daladala hazionekani, unapanda mwendokasi linalotokea Mbezi, unalipa 400 na kisha wanakushusha Mbezi Mwisho unakata tena tikiti ya sh. 650 ili uende unakokwenda.
Watu wengi wanalilia angalao Serikali ingeliona hili na kuamua kati ya mambo haya 3, Magari hayo yasiishie Kimara Mwisho bali yaende mpaka Mbezi mwisho kwa nauli hiyohiyo moja au wapunguze nauli kidogo angalao mtu unapokwenda mjini usitoe zaidiya 1000 kwa safari ya kwenda tu peke yake, na tatu, ikiwezekana daladala za kawaida ziachwe chache ziendelee kufanya kazi kwa ajili ya watu wa hali za chini.
Mama mmoja anayefanya biashara ya kuuza mahindi ya kuchoma alikuwa akilalamika kwa masikitiko akielezea jinsi ambavyo faida yake ya mahindi inavyoishia njiani tofauti na siku za nyuma alipokuwa akipanda daladala za kawaida.
Anasema mahindi huyafuata Tandale akitokea Kimara Matosa na anapofika kituoni Kibanda cha mkaa husimama muda mrefu bila kuona gari mpaka anapoamua kupanda mwendokasi kwa sh.400 hadi Kimara, halafu hapo huchukua tena mwendokasi lingine kwa sh. 650. Anasema kwa siku mpaka anafika Matosa hutumia zaidi ya sh.3,000 pamoja na bajaji kutoka stendi kibanda cha mkaa mpaka anapofanyia biashara yake.
Mwandishi wa makala hii ni Mwanzilishi wa Blogu ya Jifunzeujasiriamali na mwandishi wa vitabu vya Self Help Books Tanzania
Karibu pia kwenye Darasa la kujifunza Michanganuo ya biashara liitwalo, (Tanzania Online School of Business Planning(TOSBP))
Karibu pia kwenye Darasa la kujifunza Michanganuo ya biashara liitwalo, (Tanzania Online School of Business Planning(TOSBP))