Janja PORI
JF-Expert Member
- Jul 31, 2011
- 825
- 246
Kwanza kabisa nianze na swali, Kwa kasi hii ya mabadiliko katika mifumo mbali mbali hasa TRA, BRELA, BOT je kipindi cha nyuma tulikuwa hatuna watanzania wenye akili ? ama watu waliamua kuwa vipofu.
Kama msomi na mchumi katika vitu ambavyo amefanya Raisi Magufuli ambavyo sitasahau ni
1. MABADILIKO TRA
a) Asikuambie mtu sasa hivi TRA kuna vijana wadogo makini na wenye uchu wa kuimarisha uchumi wa nchi, MFUMO WA DIGITALI umerahishisha ukusanyaji wa kodi. Mfano sasa ukienda TRA lazima wahitaji mkataba wako, hapo inaamana direct mwenye nyumba nae atatafutwa kuhakiki amelipa kodi.
b) Process za Control Verfication ya VAT imemaliza tatizo la fake receipt na watu kutokulipa VAT
C) Process za Examination of returns and account ni kitu kilikuwa kinafanyika kwa makampuni makubwa naona sasa limerudi kwa makampuni yote Tanzania. Hii imesaidia sana TRA kupata pesa na wale wategaji, haya mabadiliko yatasababisha hata vijana kupata ajira sasa.
LAKINI BADO TRA MNA HAYA YA KUFANYA KUIMARISHA UKUSANYAJI WA KODI NCHINI
Kwa sasa hapa Tanzania unaweza ukakuta mtu aan mali za mpaka TSH 5 Billion lakini hana TIN number au analipa kodi ndogo sana au hajawahi kulipa kodi, hii inakuwaje chukulia mfano hapo chini wa MR X.
MR X amemaliza chuo lakini hajaingia kwenye ajira rasmi, ameachiwa mashamba na nyumba za kupangisha na baba ake, mashamba na nyumba zipo eneo ambalo halijapimwa, MR X anaweza amua uza mashamba kwa million 100 hadi 200 bila kulipa kodi, MRX atakuja kuchukua TIN number kwa ajili ya umiliki wa gari tu na sio TIN ya biashara. MRX atajenga nyumba atapangisha na ataendelea kuchukua kodi za wapangaji bila (WT) kwa kuwa ni ngumu kumpata. MRX anaweza akawa Tajiri bila kuwa na TIN ya biashara.
Lakini TRA ikianzisha mfumo wa kila mtu kuwa na TIN na kufile Return mwisho wa mwaka, ni rahisi kwa MRX kusema kwamba kwa mwaka huu nilipata pesa hiikutokana na kuuza shamba au kupangisha nyumba, nah ii inaweza kuwa rahisi TRA kuuliza MR X kama unaweza miliki gari na matretka mbon hulipi kodi.
Chukulia Mfano pia MRX amemaliza chuo amepata ajira isiyo rasmi, MRX anaweza fanya kazi kwa miaka 2 akapata mpaka million 30 akaamua kununua gari na kujenga nyumba lakini bila kulipa kodi yoyote, swali ni Je amewezaje kupata million 30 bila kulipia kodi, jibu ni rahisi, labda alifanya kazi akawa analipwa bila (WITHHOLDING TAX) au kulikuwa na WT sema yeye hajafile return za kila mwaka kuonesha sources za income.
Mwisho, Tax base itaongezeka endapo tutaweka mfumo wa kila mtu kufile return hata kama ni NIL return, hii itapelekea mapato mengi yakusanywe ambayo yalikuwa yanapotea.
Kwa kifupi ile notion kwamba hii ni TIN ya leseni tu sio ya Biashara lazima iondoke, mtu kama ana TIN lazima afile return kila mwaka hata kama ni NIL returns.
Kurahisha hili mfumo huo unaweza kuwa online.
Katika utafiti wangu katika baadhi ya ofisi, nimegundua baadhi ya watumishi kuwa wazuri lakini uelewa mpana wanakosa na hii ni kutokana na Mfumo ulivo TRA.
Mfano: Nilienda ofisi moja nkakutana na afisa senior tu, nkampa scenario kwamba nafanya Biashara, muda huhuo nafanya consultancy na muda huo huo na pokea kodi za nyumba za kupanga, nkamuuliza sasa je baada ya kupokea kodi ya nyumba na mpangaji amesha WT 10% mimi na haja ya kureporitia TRA, akajibu mpangaji akishalipa 10% ndo mwisho.
Ni muhimu sana kwa wafanyakazi waliopo na ambao wanaanza kupewa crach program kuhusu mambo mtambuka ya kodi, hii itawarahishia kuweza kufanya uchambuzi wa mambo.
Pia TRA ianzishe Continous learning programe mfano wafanyakakazi kujifunza mambo mapya kama Transfer pricing, Trade mark and royalties, land law and taxation, company management and Taxation etc. Na katika hili ni vyema wawezeshaji wawe ni watu kutoka private sector kuweza kubadilisha ujuzi.
Kwa Dar mfano mtu anaweza akawa na nyumba za kupanga 20 zote anapokea kodi cash na hakuna WT wala final return anazofanya. Na wengi baada ya kuona ukimiliki nyumba kama individual hakuna wa kukusumbua wengi hawawezi kuanzisha kampuni ya real estate utakuta ana nyumba 10 zote amepangisha na hakuna mpangaji analipa WT wala yeye kufile final return, hili ni eneo ambalo TRA wakitilia mkazo na litaongeza Tax base na mapato.
ASANTENI
Kama msomi na mchumi katika vitu ambavyo amefanya Raisi Magufuli ambavyo sitasahau ni
1. MABADILIKO TRA
a) Asikuambie mtu sasa hivi TRA kuna vijana wadogo makini na wenye uchu wa kuimarisha uchumi wa nchi, MFUMO WA DIGITALI umerahishisha ukusanyaji wa kodi. Mfano sasa ukienda TRA lazima wahitaji mkataba wako, hapo inaamana direct mwenye nyumba nae atatafutwa kuhakiki amelipa kodi.
b) Process za Control Verfication ya VAT imemaliza tatizo la fake receipt na watu kutokulipa VAT
C) Process za Examination of returns and account ni kitu kilikuwa kinafanyika kwa makampuni makubwa naona sasa limerudi kwa makampuni yote Tanzania. Hii imesaidia sana TRA kupata pesa na wale wategaji, haya mabadiliko yatasababisha hata vijana kupata ajira sasa.
LAKINI BADO TRA MNA HAYA YA KUFANYA KUIMARISHA UKUSANYAJI WA KODI NCHINI
- NINI KIFANYIKE KUKUZA TAX DATA BASE
- MFUMO WA UGAWAJI TIN KWA WATU WOTE WENYE MIAKA 18 NA KUFILE RETURN KILA MWAKA HATA KAMA MTU HAJAANZA BIASHARA
Kwa sasa hapa Tanzania unaweza ukakuta mtu aan mali za mpaka TSH 5 Billion lakini hana TIN number au analipa kodi ndogo sana au hajawahi kulipa kodi, hii inakuwaje chukulia mfano hapo chini wa MR X.
MR X amemaliza chuo lakini hajaingia kwenye ajira rasmi, ameachiwa mashamba na nyumba za kupangisha na baba ake, mashamba na nyumba zipo eneo ambalo halijapimwa, MR X anaweza amua uza mashamba kwa million 100 hadi 200 bila kulipa kodi, MRX atakuja kuchukua TIN number kwa ajili ya umiliki wa gari tu na sio TIN ya biashara. MRX atajenga nyumba atapangisha na ataendelea kuchukua kodi za wapangaji bila (WT) kwa kuwa ni ngumu kumpata. MRX anaweza akawa Tajiri bila kuwa na TIN ya biashara.
Lakini TRA ikianzisha mfumo wa kila mtu kuwa na TIN na kufile Return mwisho wa mwaka, ni rahisi kwa MRX kusema kwamba kwa mwaka huu nilipata pesa hiikutokana na kuuza shamba au kupangisha nyumba, nah ii inaweza kuwa rahisi TRA kuuliza MR X kama unaweza miliki gari na matretka mbon hulipi kodi.
Chukulia Mfano pia MRX amemaliza chuo amepata ajira isiyo rasmi, MRX anaweza fanya kazi kwa miaka 2 akapata mpaka million 30 akaamua kununua gari na kujenga nyumba lakini bila kulipa kodi yoyote, swali ni Je amewezaje kupata million 30 bila kulipia kodi, jibu ni rahisi, labda alifanya kazi akawa analipwa bila (WITHHOLDING TAX) au kulikuwa na WT sema yeye hajafile return za kila mwaka kuonesha sources za income.
Mwisho, Tax base itaongezeka endapo tutaweka mfumo wa kila mtu kufile return hata kama ni NIL return, hii itapelekea mapato mengi yakusanywe ambayo yalikuwa yanapotea.
Kwa kifupi ile notion kwamba hii ni TIN ya leseni tu sio ya Biashara lazima iondoke, mtu kama ana TIN lazima afile return kila mwaka hata kama ni NIL returns.
Kurahisha hili mfumo huo unaweza kuwa online.
- MFUMO WA RETURN UWE HATA KWA WAFANYAKAZI WANAOLIPA PAYE
- NIN KIFANYIKE KUBORESHA MFUMO WA UKUSANYAJI KODI
- UJUZI WA WAFANYAKAZI NA MAFUNZO YA MARA KWA MARA KATIKA FIELD ZINGINE
Katika utafiti wangu katika baadhi ya ofisi, nimegundua baadhi ya watumishi kuwa wazuri lakini uelewa mpana wanakosa na hii ni kutokana na Mfumo ulivo TRA.
Mfano: Nilienda ofisi moja nkakutana na afisa senior tu, nkampa scenario kwamba nafanya Biashara, muda huhuo nafanya consultancy na muda huo huo na pokea kodi za nyumba za kupanga, nkamuuliza sasa je baada ya kupokea kodi ya nyumba na mpangaji amesha WT 10% mimi na haja ya kureporitia TRA, akajibu mpangaji akishalipa 10% ndo mwisho.
Ni muhimu sana kwa wafanyakazi waliopo na ambao wanaanza kupewa crach program kuhusu mambo mtambuka ya kodi, hii itawarahishia kuweza kufanya uchambuzi wa mambo.
Pia TRA ianzishe Continous learning programe mfano wafanyakakazi kujifunza mambo mapya kama Transfer pricing, Trade mark and royalties, land law and taxation, company management and Taxation etc. Na katika hili ni vyema wawezeshaji wawe ni watu kutoka private sector kuweza kubadilisha ujuzi.
- KODI ZA MAJENGO HASA WITH HOLDING NA FINAL TAX
Kwa Dar mfano mtu anaweza akawa na nyumba za kupanga 20 zote anapokea kodi cash na hakuna WT wala final return anazofanya. Na wengi baada ya kuona ukimiliki nyumba kama individual hakuna wa kukusumbua wengi hawawezi kuanzisha kampuni ya real estate utakuta ana nyumba 10 zote amepangisha na hakuna mpangaji analipa WT wala yeye kufile final return, hili ni eneo ambalo TRA wakitilia mkazo na litaongeza Tax base na mapato.
ASANTENI