Mabachela/Kina mama wasio na wafanyakazi: msaada huu hapa

Mutensa

JF-Expert Member
Feb 20, 2009
421
90
Wapendwa,
si vibaya kushirikishana mambo ya maanjumati kutokana na uzoefu.
leo nimeamua kuwasaidia mabachela ili waache kula vyakulahafifu kwenye mama ntilie wajitengenezee misosi home haraka.
Basi tenga muda kwenye weekend nunua vitunguu vya kutosha, vitunguu swaumu, pilipili hoho, nyanya kiasi na vinginevyo vinavyokufaa kutokana na "taste".

Sasa utamenya nyanya nyingi tu, kata kata vitunguu kama vinne hivi na hoho za kutosha.
pima mafuta ya kutosha kupika nyanya hizi.

-- Kaanga vitunguu kama dk 2 halafu tia pilipili hoho
-- kaanga kwa dk nyingine 3-5
-- sasa mwaga nyanya zilizokatwakatwa
-- usiweke maji, endelea kuchemsha.
-- weka chumvu (na pilipili kama ni mpenzi).
chemsha mchanganyiko huu kwa kama dk 15 na baada ya hapo sauce itakuwa tayari. Ipua, subiri ipoe, halafu iweke kwenye chupa au bakuli lenye mfuniko.
Tunza kwenye fridge tayari kwa matumizi ya wiki nzima.

Namna ya kutumia mchanganyiko huu:
Mpaka hapo mchanganyiko hu utakusaidia kupika kwaharaka - iwe nyama, kuku, maharage, samaki au mboga yoyote - hauhitaji kukaangiza tena. Chukua kiasi cha huu mchanganyiko, weka kwenye mboga yoyote na chemsha. Utapata msosi wako mzuri sana fasta.
Kama una ipad yako, ingia jikoni - weka music au endelea kusurf mama yule jamaa wa zantel wakati huo msosi unajipa.
Kila la heri.

Hii sio shule ya kitabuni, its real life experience.


 
Wapendwa,
si vibaya kushirikishana mambo ya maanjumati kutokana na uzoefu.
leo nimeamua kuwasaidia mabachela ili waache kula vyakulahafifu kwenye mama ntilie wajitengenezee misosi home haraka.
Basi tenga muda kwenye weekend nunua vitunguu vya kutosha, vitunguu swaumu, pilipili hoho, nyanya kiasi na vinginevyo vinavyokufaa kutokana na "taste".

Sasa utamenya nyanya nyingi tu, kata kata vitunguu kama vinne hivi na hoho za kutosha.
pima mafuta ya kutosha kupika nyanya hizi.

-- Kaanga vitunguu kama dk 2 halafu tia pilipili hoho
-- kaanga kwa dk nyingine 3-5
-- sasa mwaga nyanya zilizokatwakatwa
-- usiweke maji, endelea kuchemsha.
-- weka chumvu (na pilipili kama ni mpenzi).
chemsha mchanganyiko huu kwa kama dk 15 na baada ya hapo sauce itakuwa tayari. Ipua, subiri ipoe, halafu iweke kwenye chupa au bakuli lenye mfuniko.
Tunza kwenye fridge tayari kwa matumizi ya wiki nzima.

Namna ya kutumia mchanganyiko huu:
Mpaka hapo mchanganyiko hu utakusaidia kupika kwaharaka - iwe nyama, kuku, maharage, samaki au mboga yoyote - hauhitaji kukaangiza tena. Chukua kiasi cha huu mchanganyiko, weka kwenye mboga yoyote na chemsha. Utapata msosi wako mzuri sana fasta.
Kama una ipad yako, ingia jikoni - weka music au endelea kusurf mama yule jamaa wa zantel wakati huo msosi unajipa.
Kila la heri.

Hii sio shule ya kitabuni, its real life experience.



Nitajaribu.............ila naona km unanisema hivi, mm sipendi ujue!!!!
 
Hey...huna haja ya ku quote the whole story!!!..................Hey...huna haja ya kuleta post yako km inakuuma mtu ku-quote

...reply tu inatosha!...........Hey...huna haja ya kunielekeza jinsi ya ku-reply

Huwa ina-kubore eeehhh..............
 
ahsante ila mm kutokana na matatizo ya ulcers huwa sipendi kutumia nyanya kwenye vyakula vyangu, nisipoweka nyanya source yangu hiyo itapoteza ladha? na je nikiweka kwenye friji haitachachuka na kunidhuru? maana huwa sili viporo samahani, nauliza kwa wenye uzoefu, hasa mzizi mkavu akipita humu jamani anisaidie
 
ahsante ila mm kutokana na matatizo ya ulcers huwa sipendi kutumia nyanya kwenye vyakula vyangu, nisipoweka nyanya source yangu hiyo itapoteza ladha? na je nikiweka kwenye friji haitachachuka na kunidhuru? maana huwa sili viporo samahani, nauliza kwa wenye uzoefu, hasa mzizi mkavu akipita humu jamani anisaidie

good question - kwa upande wa sauce ambayao haina nyanya sina uzoefu kusema ukweli. Ila kuhusu viporo - ni kuwa hii sosi haitumiki ikiwa imepoa, unatia kwenye fridge kwa ajili ya kuhifadhi isiharibike. haiwezi kuchachuka unles umeme umekatika kwa muda mrefu, itaharibika kama kitu kingine na hii ni kaa umeme umekosa zaidi ya masaa 8. Kwa matumizi, ukishaitengeneza sauce hii na ukawa tayari umepika maharage, basi unaweka tu hiyo sosi kwenye maharage na inakuwaiko tayari kwa msosi.
 
good question - kwa upande wa sauce ambayao haina nyanya sina uzoefu kusema ukweli. Ila kuhusu viporo - ni kuwa hii sosi haitumiki ikiwa imepoa, unatia kwenye fridge kwa ajili ya kuhifadhi isiharibike. haiwezi kuchachuka unles umeme umekatika kwa muda mrefu, itaharibika kama kitu kingine na hii ni kaa umeme umekosa zaidi ya masaa 8. Kwa matumizi, ukishaitengeneza sauce hii na ukawa tayari umepika maharage, basi unaweka tu hiyo sosi kwenye maharage na inakuwaiko tayari kwa msosi.

ahsante sana best, nashukuru kwa maelezo yako sasa nimepata mwanga,.
 
Back
Top Bottom